Nape: Ben Saanane amepotea, Clouds wamevamiwa, akina Roma wametekwa, Rais achukue hatua

Mtu akiogopwa sanaa na yeye akajihisi kwamba anaogopwa basi huota mapembe marefu sana kwenda juu
Mafundi wanaojenga mnara.wa babeli walifikiri wakioutsource shughuli hiyo ya ujenzi itawafichia aibu lakini mpaka sasa ndo mkandarasi anataka kukoroga zege kutumia makamasi
 
YAANI NAPE NI KWAMBA HANA DIPLOMASIA YA SIASA.HATA UNGEKUWA MAARUFU KIASI GANI, BADO SIO VIZURI KUMSEMA MWENYEKITI WAKO WA CCM KWA MAFUMBO KAMA ULIVYOFANYA.ISITOSHE YEYE NDIYE MH.RAIS WETU."UNAKUWA HUNA TOFAUTI NA AKINA SOFIA SIMBA SIKU ILE WALIPOIMBA WANA IMANI NA LOWASA WAKATI CHAIRMAN KIKWETE ANAINGIA UKUMBI WA MIKUTANO CKU ILE.MIMI NAONA NI BUSARA ZAIDI WALAO KWA KIPINDI HIKI MH.NAPE AKAJITAHIDI KUKAA KIMYA.MIMI NAONA UNAPOENDELEZA MALUMBANO KWA KISINGIZIO CHA UJASIRI, MWISHO WAKE NI WEWE KUJIBOMOA ZAIDI KISIASA ZAIDI YA KUJIJENGA.
 
Hana jipya huyu.Kama yeye aliyaona haya kwa nini asingeyasema muda mrefu?
Wenye akili nzuri tunaona huu ni USANII tu.
Kwa nini anayasema haya baada ya KUBABULIWA na mwenye mamlaka?
Lakini pia ni huyuhuyu aliyezuia kuona BUNGE live.
 
Nikiri tu, sijawahi kumfikilia Nape kama mtu mwenye akili nzuri. Ni msemaji na mkurupukaji, ameishi katika siasa lakini mpaka leo amekosa maturity katika siasa na huenda asiipate tena.

Yeye anataka kuonesha kwamba akina Mwinyi, Masilingi, Balali, Lowassa, Tibaijuka, Mahige, Kilango, Kagasheki, Mhongo, Mathayo, n.k eti walikuwa na makosa na ndo maana walivumilia kukaa kimya ila Nape hukuwa na kosa na hivyo hutakiwi kutulia na kuonesha ukomavu. Kwamba wewe ni precious! Mwanadamu hutakiwi kujiinua kupita kiasi, acha historia ikuinue. CCM ni chama kikubwa sana, walikuwepo na watazidi kuwepo chama kiko pale pale.

Nape unajikaanga kwa mafuta yako, siasa haiko hivyo. Ungekuwa umekomaa kisiasa ungewafata akina Nundu, akina Kilango, akina Migiro, akina Kitira n.k wakakushauri siasa ni nini na inataka nini. Hapa siongelei siasa za ulaya, naongelea siasa za kiafrika. Najua umepata bahati ya kuoneshwa mengi lakini umekengeuka na mengine ulishiriki wewe mwenyewe kusuka mipango dhidi ya waliokuwa wabaya kwako. Elewa, utahangaika na Magufuli lakini CCM hutoiweza kwasababu CCM si Magufuli. CCM ni taasisi na ina malengo yake.

Kumbuka, unaweza kumsumbua JPM lakini hutaweza kukitikisa chama chako. Umafia CCM ndo kwao na hizi ghiriba unazozifanya hata wewe uliwahi kuwafanyia wengine. Katika chama chenu kutoana kafara, fitina na zengwe ni masuala ya tangia enzi, tunakushangaa wewe unahamaki kitu gani. Kwamba hujawahi kujua zengwe ila leo ndo umeliona? Nahisi unachokitafuta wala hakiko mbali kwani inaeleweka, CCM kufika hapa ni kutokana na zengwe na zengwe ni sehemu ya "utaratibu wa chama" na wa chama kulinda "chama"

Tunakutakia mapambano mema!
Jamaa nimekukubali mno.......
 
Unapotapatapa kama hivi ni kazi bure....huwezi kumfanya lolote wala chochote rais, wewe ni maamuma tu, walishindwa wakongwe akina Eddo kwa Jk itakua mtoto wewe kwa JPM. Alopewa kapewa kaka. Tulia sindano ikuiingie.
 
Hatari ya kwanza ni kwamba vijana ni rahisi sana kutumiwa kwa maslahi ya wachache na pili vijana wetu sio wavumilivu na hawajajua kuwekeza katika siasa.vijana wetu wa'ioko kwenye siasa wanatawaliwa na grandiosity ya hatar
 
Mi nilijua kuna kipya ataongea kumbe ni hayo.....sasa hayo ndo alikua anaalika watu kwenye mitandao....anyway tuwekee alichokiongea kuhusu maendeleo ya jimbo lake...haya mengine hayana maana!
Kwako tuu.. Na mtazamo wako wenye akiki zako, Kwa wengine yanamaana sana.! Usiwe unaoenda sana kusemea watu vitu...
 
YAANI NAPE NI KWAMBA HANA DIPLOMASIA YA SIASA.HATA UNGEKUWA MAARUFU KIASI GANI, BADO SIO VIZURI KUMSEMA MWENYEKITI WAKO WA CCM KWA MAFUMBO KAMA ULIVYOFANYA.ISITOSHE YEYE NDIYE MH.RAIS WETU."UNAKUWA HUNA TOFAUTI NA AKINA SOFIA SIMBA SIKU ILE WALIPOIMBA WANA IMANI NA LOWASA WAKATI CHAIRMAN KIKWETE ANAINGIA UKUMBI WA MIKUTANO CKU ILE.MIMI NAONA NI BUSARA ZAIDI WALAO KWA KIPINDI HIKI MH.NAPE AKAJITAHIDI KUKAA KIMYA.MIMI NAONA UNAPOENDELEZA MALUMBANO KWA KISINGIZIO CHA UJASIRI, MWISHO WAKE NI WEWE KUJIBOMOA ZAIDI KISIASA ZAIDI YA KUJIJENGA.
Inaonekana huyu Bwana aliaminiwa sana na chama na akijiona kuwa bila yeye chama hakiendi, hivyo alilewa na sifa nyingi ndani ya chama na akadhani kuwa yupo juu kuliko hata mtu mwingine yeyote yule.
Kimsingi hawezi kushindana na m/kiti wake. Lazima ajue kuwa yule ni mwenyekiti lakini pia ni Amiri jeshi mkuu.
HEKIMA na BUSARA ni muhimu sana kwa sasa. Anakokwenda ni kubaya zaidi kuliko alikotoka.
 
Back
Top Bottom