Nadhani ni vema CCM watafute namna nzuri ya kurudisha imani kwa wananchi na si hizi propaganda ambazo wananchi wa sasa wanaelewa nini kinaendelea, si rahisi sana kuwavuruga ukawa kwa sasa kwa kuwa tulioko huku mitaaani tunaona hawa wanachama wa hivi vyama wanavyojadili mambo kwa umoja, hata akiwapo mwana CCM hathubutu kujisema.
CCM bado hamjachelewa sana, humuwezi kupingana na muda kwani kuna wakati ukifika mabadiliko ni lazima, kumbukeni Baba wa Taifa alijua kuwa kwa wakati tuliopo huwezi kuzuia tena mfumo wa demokrasia ya vyama vingi, akaukubali bila kusubiri kuja kulazimishana.
Sasa ni wakati wa CCM kujenda misingi imara ya utaifa kupitia katiba mpya ili kuwa na mfumo mzuri wa kubadilishana madaraka pasipo vurugu kama nchi nyingi za ulaya, kuwe na misingi ya utaifa ambayo haitakiukwa na chama chochote kitakacho ingia madarakani, na kwa kuwa dola haitakuwa sehemu ya siasa (chama) ndo itakuwa mlinzi mkuu wa hiyo mifumo ya utaifa.
Tunajua kuwa hofu kuu ya viongozi wengi wa CCM ni kushitakiwa au kukosa namna nyingine ya kuendesha maisha yao nje ya CCM kuwa madarakani, kuondoa hofu ya kushitakiwa na kwa kuwa ndo tunataka kujenga nchi itakayo kuwa imara kiuchumi na kidola, tukubaliane kama taifa kusameheana dhambi zote za nyuma na baada ya kusameheana tuweke sheria kali zitakazoogopesha mtu kufanya ujinga na badala yake wananchi wote kuwa na uzarendo na nchi yao kama zilivyo Japan, china, korea ya kusini na nynginezo kiongozi hasubiri kuambiwa jiuzuru akishagundua kafanya madudu yeye binafsi au wale walio chini yake.
Ni mawazo yangu kwa kuwa naipenda nchi yangu Tanazania na natamani wakati mmoja tuwe tunatisha Duniani kiuchumi na kidola angalau kwa kiwango cha korea ya kusini.