Nape alalamika

Nape alalamika

Bilionea Asigwa

JF-Expert Member
Joined
Sep 21, 2011
Posts
16,582
Reaction score
28,734
Muheshimiwa Nape Nnauye amelalamikia mitandao ya kijamii na kudai CHADEMA ndio inawafundisha vijana kufanya siasa za matusi katika mitandao.

"Kuna wakati natamani kushiriki mijadala pamoja na wale ninaoamini kuwa ni vijana wenzangu ambao wengi wanapatikana katika hizi social medias.,lakini namna ya mijadala inavyoendeshwa,lugha zinazotumika hakika si za kistaharabu na hazina heshima.


Mijadala mingi hailengi kufikia muafaka na maelewano yaliyojaa ufafanuzi wa hoja na mifano badala yake watu hutukanana, hukejeliana na kudharauliana.,haya yananivunja moyo.,najaribu kujiuliza kuwa hivi haya ndio matunda ya upinzani katika nchi hii ya kijamaa iliyojaa heshima na utu..? hivi ni kweli hakuna wenye uwezo katika wapinzani wa kuhoji kwa hoja na kuyakinisha udadisi..?


Ni jambo baya na baya kuliko ubaya wote ambao upinzani mpya chini ya chadema umekuja nao.,kuwatuma vijana kutukana katika mitandao.,tumekuwa na upinzani kwa takriban miaka ishirini lakin hatukuyaona haya isipokuwa baada ya kuinuka kwa chadema.,hili linanishawishi kuamini kuwa wamekuja nalo wao.,nasikiliza kauli za viongozi wao waandamizi wakiwa hata kwenye bunge tukufu la jamhuri,napata hisia na imani kuwa haya yanayofanyika humu kwenye social medias yanatokana na wao moja kwa moja."
source:His facebook
 
Anataka akitema utumbo asichanwe,aende facebuku hapa hapamfai!full makavu
 
Nape hana adabu kabisa.
Hizo propaganda zake azipeleke kwenye magazeti ya uhuru na mzalendo.

Kabla hajawa fisadi ndani ya CCM alikuwa anakuja humu mitandaoni na kuongea vitu vya maana na tunampongeza leo anakejeli watu.

Halafu kwa mara nyingine tunamwonya tunajua huwa anachangia hoja kwa siri humu JF, ID zake humu JF tunazifahamu lakini tunaheshimu kanuni za JF hivyo hatutaki ku-expose na kama ataendelea na matamshi yake ya kejeli tutamwaga.
 
Sio kwamba nasapoti matusi toka kwayoyote ila naamini hata yale maandamano yanayosemakana niyawaisilamu (mimi siamini sana)Naona nikama maandamano yawaliochoka hali fulani ndio maana wanaandamana.Pia lugha wanazotumia vijana nadhani nistaili tu yakuonyesha wamechoka!Nasiamini kama woote ni CDM maana huwa hataji kadi namba zao zavyama!
 
Nafurahi sana amekiri kuwa chadema imeinuka.

Sent from my BlackBerry 9700 using JamiiForums
 
AAH ANGEKUJA HUKU JF TUKAMCHANA VILIVYO HAJUI KUWA CHAMA CHAKE ANACHOONGOZA NI FISADI, NA NDO CHAMA KILICHOLIANGAMIZA TAIFA HILI, NNAPE NJOO TUKUCHANE UPESI USITUANGUSHe, FISADI PIA MWIZ MKUBWA WEWE NA CCM YAKO
 
nape hajawahi kumlaumu Rostam Aziz .....'gutter politics'
 
Nape nenda kwanza kamwambie LUshindeeeeeeeeee na yule kaka yako wa kule Sheruiiiiiiiiii, anayekuwekea mshahara...........Migulu Nshemba
 
wanatukana kama LUSINDE!

Nape kweli wewe hamnazo kabisa,hv huwa unafikilia kabla ya kusema?au kwa kuwa CCM mmezoea kutufanya sisiwatanzania mandondocha wenu.unakumbuka alichokifanya Livingstone Lusinde kule Arumeru masharik?zama za watanzania kuwa wajinga zilishapita siku nyingi kaka pole kwa kuwa na mawazo mgando.
 
May be anatafuta huruma za watanzania kutaka kutuonesha hata yeye anatukanwa sio wapizani tuu..........
 
anataka apambwe na mapambo, kwanza hakuna aliyemtukana TATIZO KUBWA KWA VIONGOZI WA CCM, waliambiwa ukweli wao wanasema hayo ni matusi kwao.Kwa mfano chaguzi zao zote rushwa imetumika, hata na Mkuu wa nchi ambaye ni m/kiti wa CCM taifa amekiri hili, sasa hapo mtu akisema hiki ni chama cha mafisadi!!! tusi litakuwa ni lipi wakati kasema ukweli
 
Ajiulize kwanza kwanini wa TZ wote wana mpinga mtandaoni? na je kwenye mitandao ya jamii kuna vijana tuu?
Njaa na kuendekeza vimaslahi ni utumwa kwako.Hebu taja watu wanakutukanaje?
 
Nape ww si kijana kiumri sawa kimatendo ww ni nzee jiulize nyimbo ngapi unaziimba hupati washiriki matusi unayaona jf mbona hujamkemea lusinde ,mchemba,komba.umesahau kuwa hii nchi si ya kijamaa unalijua azimio la zenji,au hukuwapo Dodoma rushwa njenje. Vijana wa sasa si wale unaowajua, ww mwenyewe umetukana mara ngapi songea ,iringa kweli ndege wote waimbe akiimba bundi uchuro
 
anataka apambwe na mapambo, kwanza hakuna aliyemtukana TATIZO KUBWA KWA VIONGOZI WA CCM, waliambiwa ukweli wao wanasema hayo ni matusi kwao.Kwa mfano chaguzi zao zote rushwa imetumika, hata na Mkuu wa nchi ambaye ni m/kiti wa CCM taifa amekiri hili, sasa hapo mtu akisema hiki ni chama cha mafisadi!!! tusi litakuwa ni lipi wakati kasema ukweli
Ni kweli siasa za kizazi hiki viongozi wa CCM hawaziwezi ...wamezoea kusifiwa kwa kila jambo na kutokuambiwa ukweli...Zile habari za ZIDUMU FIKRA SAHIHI ZA MWENYEKITI wanataka kuziendeleza mpaka kizazi hiki
 
Tusubiri siku ya jmosi kama atapewa hiyo nafasi tena ya kuwa katibu mwenezi maana hata bosi wake amemchoka
 
Nape anapata wapi moral authority ya kuhoji lugha wanazotumia watu wengine? Kwa ustaarab gani aliounoshea huyu kijana kiasi kwamba anaamini yeye anaweza kuongelea lugha ya kistaarab? Na pia Nape anataka kuaminisha watu kuwa wanaopingana naye ni kutoka upinzani? Kwamba, all is well in Lumumba St, hakuna msugano kabisa, kila mtu anacheka ni mwingine!
 
Back
Top Bottom