nguruka wa kig0ma
JF-Expert Member
- Jan 16, 2020
- 2,946
- 2,929
Wakuu saalam!
Mimi ni mgeni jukwani, naomba ushirikiano.
Niende kwenye mada.
Nikirudi kifikra mpaka mwaka 2015 kwenye uchanguzi mkuu, tuliona utitiri wa watia nia, ikaitwa demokrasia.
Baada ya pale tukaanza ona vituko vingi, vichinjio Mara wengine wakawekwa korokoroni wakati wengine wanaendelea kutembeza vinjio kwenye mkutano mkuu.
Haikutosha mara paap, asiyetarajiwa akaokota dodo chini ya nguzo ya Tanesco.
Tukaona Lowassa kahamia upande wa pili.
Haikutosha, Lowassa akizindua kampeni kule Arusha, tukamuona Msukuma na chopa akishuka kumsaidia Lowassa kuzindua kampeni huku akiwa bado CCM, ilikuwa viini macho na mengine mengi.
Tia maji tia maji 2020 hii hapa, tumeanza ona vituko vingi. Toka mwaka jana mara sauti zimesikika kwenye mtandao wakimsema mkuu, haikutosha baadhi waenda piga magoti kushika miguu ya mkuu.
Wengine wakagoma, waitwa kwenye kamati.
NAPATA SHAKA NA HOFU KUU, isije ikawa vituko vyote hivi ni mapishi ili kuwapoteza wapinzani waone kina Membe, Kinana na Makamba watawapa nguvu za kushinda uchanguzi mwaka huu kama ulivyokuwa kwa Lowassa.
USHAURI KWA WAPINZANI:
Acheni kuchukua wanasiasa toka CCM, watengenezeni watu wapya ili kujenga Imani isiyo tindika kiupinzani.
Vijana wapo wengi Tena wasomi wakubwa.
KARIBU TUJADILI.
Sent using Jamii Forums mobile app
Mimi ni mgeni jukwani, naomba ushirikiano.
Niende kwenye mada.
Nikirudi kifikra mpaka mwaka 2015 kwenye uchanguzi mkuu, tuliona utitiri wa watia nia, ikaitwa demokrasia.
Baada ya pale tukaanza ona vituko vingi, vichinjio Mara wengine wakawekwa korokoroni wakati wengine wanaendelea kutembeza vinjio kwenye mkutano mkuu.
Haikutosha mara paap, asiyetarajiwa akaokota dodo chini ya nguzo ya Tanesco.
Tukaona Lowassa kahamia upande wa pili.
Haikutosha, Lowassa akizindua kampeni kule Arusha, tukamuona Msukuma na chopa akishuka kumsaidia Lowassa kuzindua kampeni huku akiwa bado CCM, ilikuwa viini macho na mengine mengi.
Tia maji tia maji 2020 hii hapa, tumeanza ona vituko vingi. Toka mwaka jana mara sauti zimesikika kwenye mtandao wakimsema mkuu, haikutosha baadhi waenda piga magoti kushika miguu ya mkuu.
Wengine wakagoma, waitwa kwenye kamati.
NAPATA SHAKA NA HOFU KUU, isije ikawa vituko vyote hivi ni mapishi ili kuwapoteza wapinzani waone kina Membe, Kinana na Makamba watawapa nguvu za kushinda uchanguzi mwaka huu kama ulivyokuwa kwa Lowassa.
USHAURI KWA WAPINZANI:
Acheni kuchukua wanasiasa toka CCM, watengenezeni watu wapya ili kujenga Imani isiyo tindika kiupinzani.
Vijana wapo wengi Tena wasomi wakubwa.
KARIBU TUJADILI.
Sent using Jamii Forums mobile app