Napata maumivu ya kichwa yasiyopona kwa takriban mwezi sasa

Napata maumivu ya kichwa yasiyopona kwa takriban mwezi sasa

Naxria abdalla

Senior Member
Joined
Feb 28, 2025
Posts
158
Reaction score
281
Natumai nyote mu wazima wa afya.

Nimekuwa nikisumbuliwa na maumivu ya kichwa yasiyopona kwa takriban mwezi sasa. Kila siku, ikifika muda fulani, kichwa huuma sana na kunikosesha raha.

Nimetumia dawa nyingi bila mafanikio.

Je, huu ni wakati muafaka wa kupima macho ili kuona kama tatizo linaweza kuwa macho yangu?

Huenda nikapata afueni.
 
Wewe ni mdada sio? Vipi vipimo vya Homoni umefanya? Estrogen ikishuka inasababisha migraines sio ya kawaida. Unaumwa na kichwa ukilala kipo, ukiamka kipo. Ukimeza dawa kikitulia ni dakika tano kinaanza tena.
Mara ya mwisho kwenda hosptal doctor amenipa hadi dawa za allergy na za kuspray kwenye pua amesema kuna kitu ameona labda nayo inasababisha hali ya kuumwa kichwa nimetumia lkn bdo,labda nirudi kupima ivo vitu ulonambia
 
Mara ya mwisho kwenda hosptal doctor amenipa hadi dawa za allergy na za kuspray kwenye pua amesema kuna kitu ameona labda nayo inasababisha hali ya kuumwa kichwa nimetumia lkn bdo,labda nirudi kupima ivo vitu ulonambia
Sawa dear. Pia kama huwa haupati mafua kwa muda mrefu sana wanasema huwa inasababisha pia kichwa kuuma.
 
Mara ya mwisho kwenda hosptal doctor amenipa hadi dawa za allergy na za kuspray kwenye pua amesema kuna kitu ameona labda nayo inasababisha hali ya kuumwa kichwa nimetumia lkn bdo,labda nirudi kupima ivo vitu ulonambia
Pole Mamii...!!Hicho Kitu Alichoona Ni Kitu Gani??Alikiona Kimiujiza Au Ni Majibu Kutoka Kwenye Vipimo?
 
Mda mwemgine kinauma apa mbele kwenye komo,mda mwengine upande wa kulia na mda mwengine upande wa kushoto
Ok nenda hospitali nzuri ukamuone Daktari bingwa, itapendeza akiwa wa ufahamu na ubungo.

Headaches ina sababu nyingi, inaweza kuwa migraines, cluster headache, au kuna ugonjwa mwingine wowote.
 
Kwann kina muda maalumu kuuma unatakiwa ujiulize hili swali
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom