Napata changamoto kubwa katika kupanga mambo yangu

Napata changamoto kubwa katika kupanga mambo yangu

Members ya JF Nawasalim.

Mimi ni kijana. Umri wangu haujavuka miaka 30. Naomba Ushauri wenu katika hili....

Kwa kipindi kirefu nimekuwa kwenye jitihada binafsi za kubadilisha sehemu kubwa ya tabia zangu ambazo mimi mwenyewe ninaziita "mbaya" lakini changamoto kubwa ni kuwa sijafanikiwa. Bado najiona nipo vile vile.. bado najiona ni mtu anaehitaji kujifunza mengi na kubadilisha mambo mengi.

Mfano, Nina kazi ambayo namshukuru sana mwenyezi Mungu. Maana naona ni muujiza mimi kuipata. Kazi hii japo nilianzia ngazi ya chini kabisa "Volunteer" niliipata hata bila kuwa na vigezo sahihi kielimu ukiachilia "experience" ambayo nimeipata hapa hapa ofisini na ni majuzi tuu ndio nimefanikiwa kupata cheti sahihi cha shule. Na bado nasoma.

Kama ilivyo ofisini na nyumbani. Changamoto kubwa nayopitia ni kushindwa kwa asilimia kubwa kupanga mambo yangu. Sehemu kubwa ya maisha yangu kwa kila siku imetawalwa na "Frustrations". Iam always late.

Japo ninamshahara Mzuri, lakini nina madeni karibu nusu ya mshahara wangu. Na hii imetokana na ile tabia yangu ya kutaka mabadiliko ya haraka baada ya kujiona nimechelewa na hivyo kuanza kufanya vitu ambavyo naviita vya kimaendeleo kwa haraka na kupelekea kujikuta naingia kwenye madeni ambayo baadae nimekuja kugundua kuwa, nayalipa kwa miezi mingi sana. Kiasi kwamba hata kabla sijamaliza kuyalipa linatokea lingine ambalo kwa kujitizama nafasi yangu na mshahara wangu, naona nilipaswa kuwa nalo miaka mitatu au miwili iliyopita. Hapo nitafanya kila namna nipate pesa ninunue....

Tizama hii. ......

Nimefanya kazi miaka mitano sasa. Lakini sasa ndio nimemaliza mwaka tokea nitoke nyumbani na kwenda kupanga"

Ndani ya mwaka huo huo mmoja ambao hiyo miaka minne nyumbani sikuwahi kuwaza wala kuweka hakiba ya pesa kwaajili ya kujakujitegemea. Niliwaza tuu kisha siku moja nikaamka nikatafuta mahala pakukaa nikalipa kodi na kuhamia. Hata nyumbani siku aga..... habari hii ni ndefu.

Kwa kifupi napata wakati mgumu sana kupanga na kutimiza mipango yangu. Mambo mengi ambayo nayaona ndio ya msingi sifanyi. Tatizo kwangu ni nini? Na ni vipi nitaweza kujitoa hapa nilipo? Kila siku mimi ninaanza. Sijawahi kuendelea. Sijawahi kuyafikia malengo yangu.

Vingi nilivyonavyo naona kama sikuvistahili.... hasa nikijiangalia tabia zangu na matendo. Kwanini najidharau? Kwanini naona kama sikuvistahili? Nje am very respectful lakini ndani najiona ni mtu mwenye changamoto kubwa ya kujibadilisha na kuwa aina ya mtu ambae siku zote nimekuwa nikitamani kuwa.

Napenda kuwa mtu wa mazoezi, napenda kuwa na mwili wa kimazoezi. Napenda sana kuwa msomi hasa niliyebobea kwenye masuala ya manunuzi. Napenda kuwa mcha Mungu wa kweli na sio mnafiki. Nisizini huku nikimsifu Mwenyezi Mungu, niseme uongo, nioe Mke Mmoja. Tujaliwe watoto. Nijenge nyumba ya kuishi na familia yangu. Niwepo kwaajili ya Familia yangu, Ndugu zangu, marafiki na Jamii inayonizunguka. SITAKI KUWA WALA KUSHIRIKI UNAFIKI.

Changamoto kubwa ni vipi nitayaweza haya yote kwa Matendo? Kila napopanga. Asubuhi naamka na kupangua. Ya Msingi nayasogeza "Kesho" ambayo sijawahi kuifikia.

Am breaking down. Am worried. How do I survive this?
Ili ufanikiwe inabidi uwe na roho mbaya hata kwako mwenyewe.
Hakikisha hudaiwi hata sente mo jah.
1.kula yako isizidi buku 2 deilee.
2.NUnua unga kwa jumla.
3.Tumia mboga za majani tu, ni nzuri kwa afya.
...Ukipata mshahara nunua sabuni mche (buku) sabuni unga (jelo) dawa mswaki (buku jelo),mafuta ya kula na sembe.
Unapotoka pima nauli yako tu halafu tembea na ten kama emergency.
Usichangie harusi, usifanye safari zisizokuwa na kichwa wala matako,hakikisha baada ya kazi straight ghetoni mwako, kampani yako kubwa iwe radio, fuatilia vipindi mbalimbali.
....baada ya miezi kumi njoo hapa utupatie mlisho nyuma.
 
It's never too late to start over. If you are not happy with a kind of life your living there is a room for change. I would say getting closer to your creator, bow that's the only way you can be content. Also there’s no faster way to improve than to have someone work with you on your goals.
Hebu nieleweshe Mkuu. I do pray but after my prayer is done nifanye nini? Nimedevelop woga kiasi kwamba hata nikipata changamoto kidogo tuu kiofisi na over react. Sometimes nayasikia mapigo yangu ya moyo yakiongezeka speed. Hapo naanza kuhisi labda naweza patwa na heart attack.

Kwanini nakuwa hivi?
 
njoo nikupangie bajeti ila ujiaNdae mlo m1 kw ck,, bia unaistaafu,,,, vimada marufuku,,,,,, 4Gb utazisikiaga kwa wenzio,,,, nyumba ya kupanga yenye kibatar,,,, kutembelea / kusalimia marafik / ndg ndo mwisho,,, kazini unapanda daladala 1 kM kuna inayofuata unapaswa utembee,,, [marufuku kupanda mabasi y mwendo kasi] mda wa kazn utakula ofa ya msOsi wa ofisin hakuna kununua maji utakunywa ya bomban,,,,,, nguo 7 tu sulual2 tishrt 5,, viatu mtumba 1 yeboyeb1,,,, kunyoa mara 1 kw mwez,,,,, mafta y kupaka babycare,,,, sabun OMO hyohyo unaogea na kufulia----------- MPAKA HAPO ULIDHIKE NA KILE UNACHO KITAFTA,,,. malengo hayaji kwa kujiluxiary mkuu.
Hahahahahahahahah we mbaya aisee

Ila vijana wanaoanza kazi kwa Mara ya kwanza wana mbwembwe sana .

Wanataka kila kitu.

Kitanda cha chuma ,sofa,fenj,jiko la gesi,brenda ,TV na king'amuzi sabuwufa, yaaani chumba kinajaa makorokoro utadhani stop

Hapo anataka nguo nzuri ya dukani mitumba hataki tena.

Kiatu cha dukani

Kama ndo msichana anasuka mitindo ya nywele kila siku ya 10000

Ajaze vocha simu anataka Samsung galaxy note 5 au iPhone hahahahhahah

Hajalipa kodi

Anakula baga na piza pale kfc au mgahawa wa maana .

Hajapigwa mzinga na ndugu jamaa na marafiki.

Hajaumwa[emoji14]

Michango ya harusi .

Bado hajanywa bia

Njoo sasa kwenye salary basic inasoma 530017/= take 410000/=

Hahahahahahah kijana huyu matokeo yake anaishia kuwa mtu ea madeni.wala hajawahi kufaidi mshahara wake mzima hata siku moja

Mvumilivu hula mbivu
 
Pole saana, Wala hujachelewa ndugu kutimiza malengo yako.

Jambo moja zuri juu yako ni kuwaabadiliko yameanzia nafsini au ndani yako (intristc motivation) hilo ndio jambo kubwa pale unapotaka kubadilika.

Unahamu ufike hatua Fulani nzuri ila tatizo lako ni how you go through hapo unapopataka.

From your explanation hapo inaonesha huweki malengo na time to achieve it, it seem ukifikiria jambo unataka hapo hapo ulipate. That is no. Hatuendi hivvyo

Lazima kila jambo ulipe muda ili kulitimiza barabara... Ulipo amua kupanga ni lazima kwanza ujipange ufanye utafit wapi utaenda kukaa, pana changamoto gani, nn kinahitajika utakipata vp?... Sio tuu umefikiria then kesho unaenda...lazima uingie kwenye madeni

Vile vile hakikisha unachokipanga kinakuwa feasible...kinakuwa within your ability to implement and achieve hata kama sio 100% but at least kiwango Fulani cha kuridhisha. Ukipanga jambo nje ya uwezo wako utaishia kuwa na frustrations.

Weka vipaombele, lipi Liwe lakwanza lipi lifate....huwez kutekeleza yote kwa pamoja ila unaweza yafanya yote kwa kujipa vipaombele...ndio maana umekuwa na deni then unaingia katika maden mengine. Mwishowake you just lose focus.

Kitu kingine unatakiwa uridhike hapo juu umesema swala la kwamba hujawahi kufanya maendeleo, hujawah kufikia malengo yako, while pengine unasema ulikopa kufanya maendeleo... Dah unajichanganya mwenyewe kumbuka maendeleo sio abrupt ni slow process na kwa hatua, moja baada ya nyingine. Ridhika na hizo ndogo sali omba upige nyingine. Usipo kuwa na moyo Wa kuridhika Haata ukifanya nn utajiona hauja piga hatua

Lastly...unamalengo mengi saana unataka uwe mwana mazoez..hilo jepes tenga muda anza taratibu na mazoez mepesi.

Unapenda kuwa msomi mbobezi hilo pia ni swala LA muda na kujipa bidii katika masomo unayosoma.

Unapenda kuwa mcha Mungu, sio mnafiki, muongo Wala mzinifu. Haya yote yanawezekana kama ukimpa Mungu maisha yako ukikataa tamaa za mwili Sali saana...kuwa na hofu ya mungu....

Good luck
Asante Mkuu.

Wakati mwingine nahisi labda nakosa descipline. Maana nikiweka malengo ya kusave mathalani 450,000/- kwa mwezi unakuta mwisho wa huo mwezi nina 50,000/- tuu.

Yaani inakuwa ni as if nikipanga ndio matatizo ya kiuchumi yanaongezeka. Kuna kipindi nikaamua kutosave. Nikasema kwa siku nitatumia 10,000/- lakini baada ya wiki nikifanya tathmini najikuta nimetumia 150,000/-.

Nahisi kuna kitu nimemiss. Am looking for it. Somewhere somehow kuna mambo nafanya ambayo sio sahihi.

Nisiwe Muongo. Nina miaka mingi sijaingia kanisani. Huwa nachoka kufuata zile formalities za kanisani. Natamani mchungaji aongee kuhusu maisha na namna ya kushinda changamoto za maisha.

Nilianza kwenda kwenye morning glory. Mwanzoni nikawa nafurahi lakini as days pass on nikawa naboeka na baadhi ya mafundisho. Ikawa nikienda jumatatu kama sikulipenda somo siendi tena until other week Monday.

Mwisho nikaacha kabisa. Nikaanza kusoma vitabu vya self empowerment. Nakuwa active for a while then all over the sudden narudi pale pale.

Nikawa na subscribe YouTube channels za motivational speeches nyingine nimezidownload. But nimeishia kuzikariri.

Nimekuwa mtu wa kushauri watu mambo mazuri but I can't do the same for my self.

Najisikia vibaya. But sijakata tamaa. Nina miaka mitano muajiriwa but Leo hii account yangu ina 100,000/- nikiwaza roho inaniuma maana naona wenzangu wanavyopata tabu mtaani.

Mimi nina kazi but naona nimeshindwa kujiendeleza.

Kuna kipindi nilikuwa natembea na mpaka laki mbili mfukoni. Nanunua nguo isiponiyosha nawapa wadogo zangu. Nilipenda zaidi kufanya wengine wafurahi kuliko Mimi mwenyewe.

Nilikuwa najisikia vibaya kumpa omba omba shillingi mia. Nikitoa hela ndogo sana ni elfu mbili. Nilikuwa najisikia furaha nikiona wakifurahi na kunishukuru. But in long run sikuweza kujiwekea chochote.

Kila siku naanza kubadilika. Kila siku kasema Leo ni siku yangu. But jioni utanikuta alone nikijilaumu kwa kutumia hela vibaya ama kuutumia muda wangu vibaya.

Sitaki kuamini kuwa it's an internal issue, but slowly naanza kukubali.

Nilipanga kila Sunday morning niwe nakimbia maana weekdays nakuwa busy na kazi pamoja na shule ila ikifika jumapili Asubuhi najisemea acha nilale maana wiki nzima nilikuwa busy mazoezi nitaenda jioni. Nitaamka saa nne nifue, nioge nile hapo ni saa tisa ikifika jioni hamu ya mazoezi imekata natamani nikae niangalie movie ndani ya nafsi nasema nawaza how to improve my self.

It has been rotating like that. Everyday back again at the point of departures. Yaani it's like a treadmill
 
acha haraka haraka uvumilivu ndio muhimu na acga kukurupuka kufanya vitu fulani...pangiia kila mwezi angalau ufanye kitu fulani .....usiharakishe mali kwa pupa...pangilia
 
Kwanza weka mambo haya akilini kwako na kumbuka kila mara unapotaka kufanya mabadiliko
1. Any change to behavior should be incremental. Hakikisha unajua unabadilisha nini, kwa muda gani, unaaniza wapi na target yako ni nini. Kisha fanya hayo mabadiliko kwa kujiongezea targets only after completing one increment.
2. Discipline. Hii sio katika kufanya mabadiliko tu bali iwe katika personality yako. Kuwa hasa na discipline katika mambo uliyoyafanyia maamuzi. Acha kujipa moyo kwa shortcuts. No hard work goes in vain na nothing comes without hard work.
 
Asante Mkuu.

Wakati mwingine nahisi labda nakosa descipline. Maana nikiweka malengo ya kusave mathalani 450,000/- kwa mwezi unakuta mwisho wa huo mwezi nina 50,000/- tuu.

Yaani inakuwa ni as if nikipanga ndio matatizo ya kiuchumi yanaongezeka. Kuna kipindi nikaamua kutosave. Nikasema kwa siku nitatumia 10,000/- lakini baada ya wiki nikifanya tathmini najikuta nimetumia 150,000/-.

Nahisi kuna kitu nimemiss. Am looking for it. Somewhere somehow kuna mambo nafanya ambayo sio sahihi.

Nisiwe Muongo. Nina miaka mingi sijaingia kanisani. Huwa nachoka kufuata zile formalities za kanisani. Natamani mchungaji aongee kuhusu maisha na namna ya kushinda changamoto za maisha.

Nilianza kwenda kwenye morning glory. Mwanzoni nikawa nafurahi lakini as days pass on nikawa naboeka na baadhi ya mafundisho. Ikawa nikienda jumatatu kama sikulipenda somo siendi tena until other week Monday.

Mwisho nikaacha kabisa. Nikaanza kusoma vitabu vya self empowerment. Nakuwa active for a while then all over the sudden narudi pale pale.

Nikawa na subscribe YouTube channels za motivational speeches nyingine nimezidownload. But nimeishia kuzikariri.

Nimekuwa mtu wa kushauri watu mambo mazuri but I can't do the same for my self.

Najisikia vibaya. But sijakata tamaa. Nina miaka mitano muajiriwa but Leo hii account yangu ina 100,000/- nikiwaza roho inaniuma maana naona wenzangu wanavyopata tabu mtaani.

Mimi nina kazi but naona nimeshindwa kujiendeleza.

Kuna kipindi nilikuwa natembea na mpaka laki mbili mfukoni. Nanunua nguo isiponiyosha nawapa wadogo zangu. Nilipenda zaidi kufanya wengine wafurahi kuliko Mimi mwenyewe.

Nilikuwa najisikia vibaya kumpa omba omba shillingi mia. Nikitoa hela ndogo sana ni elfu mbili. Nilikuwa najisikia furaha nikiona wakifurahi na kunishukuru. But in long run sikuweza kujiwekea chochote.

Kila siku naanza kubadilika. Kila siku kasema Leo ni siku yangu. But jioni utanikuta alone nikijilaumu kwa kutumia hela vibaya ama kuutumia muda wangu vibaya.

Sitaki kuamini kuwa it's an internal issue, but slowly naanza kukubali.

Nilipanga kila Sunday morning niwe nakimbia maana weekdays nakuwa busy na kazi pamoja na shule ila ikifika jumapili Asubuhi najisemea acha nilale maana wiki nzima nilikuwa busy mazoezi nitaenda jioni. Nitaamka saa nne nifue, nioge nile hapo ni saa tisa ikifika jioni hamu ya mazoezi imekata natamani nikae niangalie movie ndani ya nafsi nasema nawaza how to improve my self.

It has been rotating like that. Everyday back again at the point of departures. Yaani it's like a treadmill
u need a strong woman to help you my friend
 
njoo nikupangie bajeti ila ujiaNdae mlo m1 kw ck,, bia unaistaafu,,,, vimada marufuku,,,,,, 4Gb utazisikiaga kwa wenzio,,,, nyumba ya kupanga yenye kibatar,,,, kutembelea / kusalimia marafik / ndg ndo mwisho,,, kazini unapanda daladala 1 kM kuna inayofuata unapaswa utembee,,, [marufuku kupanda mabasi y mwendo kasi] mda wa kazn utakula ofa ya msOsi wa ofisin hakuna kununua maji utakunywa ya bomban,,,,,, nguo 7 tu sulual2 tishrt 5,, viatu mtumba 1 yeboyeb1,,,, kunyoa mara 1 kw mwez,,,,, mafta y kupaka babycare,,,, sabun OMO hyohyo unaogea na kufulia----------- MPAKA HAPO ULIDHIKE NA KILE UNACHO KITAFTA,,,. malengo hayaji kwa kujiluxiary mkuu.
Nielekeze namna ya kusimamia bajeti nayojiwekea. Nipe ujanja wa kuwakwepa ndugu, jamaa na marafiki ambao mara kwa mara wakikwama wamekuwa wakiniomba msaada. Nielekeze ni vipi naweza ithibiti njaa yangu. Ni vipi naweza kula mlo mmoja na bado nikawa productive in a day. How do I develop such a descipline?
 
Peer/Society pressure is what makes you wanna do a million things at once. You keep up with that "I'm late" bs, and you will always play catch up. You know your goals, so draw your master plan.

Financial discipline. I got a pretty messed up one too, and I'm still working on it. But for you, stop giving in to the outside pressure will be a good start.

As for your spiritual conflicts; just be true to yourself first. God made everybody in his own image, so you're the closest thing to your God. Do what you think is right, and you'll be right before the main man.

The rest, don't stress. Will come with age and time, long as you stay in the right track.
Umesema kweli. Ninayotabia ya kukilinganisha na wenzangu. Na sikuzote naona wao wako mbele yangu hivyo kujiona natumia vibaya muda wangu na hela zangu.

Asante sana. I will start to careless about others and more about my self. But again. I will start... kila siku Mimi naanza kitu kipya.

Mungu ni Mwema.
 
Wewe jamaa itabd nikutafute... Yani matatizo uliyonaayo ni kama umeniandia mm.. Nashukuru michango Yani nami najfunza.
 
How do I do that?
umewahi kufunga milango yako ukakaa chini ukajitafakari peke yako kwa muda?
wewe ni nani, unataka nini na kwa muda gani na utakipata vipi?

jaribu kujiuliza hivo peke yako.. jitahidi kujishauri wewe binafsi kabla hujashauriwa

anaejua mapungufu yako ni wewe mwenyewe.
jifunze kusema na moyo wako/jiongeze
usipende mambo yako binafsi kuomba omba maushauri ya watu!!
unatakiwa wewe mwenyewe uwe mshauri wako mkuu.
ukikwama ndipo unapoomba ushauri badala ya hapo unauchuja na unapata jibu kamili
 
I think u shld start by stopping any kind of addiction that u have
 
I have been there, wake up call ilikuwa mtoto wangu wa kwanza alipozaliwa. Nilibadilika kabisa. Shida yangu kubwa ilikuwa safari zisizokuwa na msingi, nilikuwa nikitoka kazini siku ya ijumaa lazima nisafiri kwenda what ever the cost. Likizo nilichukua ili nipige misele. Nilipoteza muda mwingi na pesa nyingi kama vingetumika vizuri ningekuwa mbali sana. Watu wengine tunahitaji major event kwenye maisha kutoka kwenye mashimo tunayojichimbia wenyewe.
 
Back
Top Bottom