Naondoa upendo rasmi kwa mama yangu wa kambo

Naondoa upendo rasmi kwa mama yangu wa kambo

huenda tatizo lipo kwako.
- unajisikia wewe ni mtoto wa kiume ndio maana baba yako anakupenda zaidi ya wengine.
- unaamini baba yako hana maamuzi yake pasipo kushawishiwa na "mama wa kambo"
- unadhani kwa vile umesoma kuliko wengine basi mambo yako yatanyoka kuliko wao.

kama niko sahihi kwa hayo niliyosema hapo juu nakushauri uanze kufanyia kazi yafuatayo
- amini kwamba baba yako anakupenda kwa vile ni mwanae na si kwa sababu wewe ni mtoto wa kiume
- mdhihirishie baba yako kwamba unawapenda nduguzo na utashirikiana nao siku zote. hii inaweza mfanya abadili
mawazo yake kuhusu mgawanyo wa mali zake
- tambua kwamba kusoma ni muhimu japokuwa sio uhakika wa mambo kukunyokea maishani. wapende nduguzo
bila kujali elimu yao.

hata hivyo nikupe pole kwa changamoto ulizopitia. nakuombea baraka na mola akuonyeshe pale ulipokosea ili uweze kupanyosha na pale ulipokosewa ili paweze rekebishwa.

Naomba nieleweke Mimi sina shida ya mali ninachotaka ni kupata ushirikiano na familia.
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Mimi ni kijana nina ndugu zangu tunakutana kwa baba ambao ni 7 wakike 5 wanaume ni 2...

...Lakini nikaamu kurudisha mahusiano kwa mama yangu wa kambo na ndugu zangu si unajua damu nzito.Lakini kitendo alichofanya huyu mama ndicho kinachokata mahusiano rasmi mimi na yeye.

Kwani amemshawishi baba yangu kagawa mali kwa ndugu zangu bila kunishirikisha mimi.
Kwa kweli imeniumiza sana,nimemueleza mama yangu mdogo kwa kweli machozi yamemtoka.

Ushauri: je, nifanyeje na pia mimi ndo nimepata bahati ya kusoma ndugu zangu wote wamekataa shule.

Naomba nieleweke Mimi sina shida ya mali ninachotaka ni kupata ushirikiano na familia.

kama nia ni kupata ushirikiano na familia ni vyema ukaondoa kukasirika baada ya kutoshirikishwa mawanyo wa mali. na ukiondoa hilo basi sababu ya msingi ya kukata mahusiano na mama yako wa kambo inapotea na hivyo roho ya kurejesha mahusiano itakutawala. ukifanya hivyo naamini utafanikiwa kurejeshaa mahusiano na ndugu zako. Mwenyezi Mungu akutangulie ufanikiwe katika hilo.
 
Bado nina upendo na ndugu zangu najua lengo la huyu mama ni kuleta mpasuko katika familia lakini mimi nitazidi kujisogeza kwao ingawa sitaki kujihusisha na kitu chochote kinachohusu mali.Ingawa imeniuma kwani mimi ni binadamu sina moyo wa chuma nina moyo wa nyama.
Unachozungumza nakielewa kwa kina . Kuhusu uhusiano na hao ndugu zako muombe tu Mungu wawe waelewa kwani walio wengi huwa wanafiki na hasa hujenga urafiki wakiangalia maslahi yao, wapo watakaofanya urafiki nawe ili kuona unasema nini juu ya kilichotokea. Tena ndugu wa aina hii ijapokua si wote hufuata mawazo ya mama yao na wewe huonekana adui .

Kwa bahati mbaya wazazi kadhaa hukosa hekima kwani hapakua na shida ya kukupa nawe sehemu yako hata kama ni ndogo. Wazazi wanaopitia humu na wenye watoto mchanyanto wajitahidi kuzuia majeraha dizaini hii kwani kasoro hii husababisha vizazi na vizazi kuwekeana chuki.

Ni kweli hupaswi kutegemea urithi lkn ni haki yako kurithi sababu haturithi kwa sababu hatuna uwezo bali tunarithi kwa sababu ni warithi sina namna ya kuiweka hii. Kama mzazi utakua na hekima basi ni bora kuwaweka watoto pamoja na si kuwabagua. Migogoro ya aina hii wanaomumia zaidi ni watoto hasa wenye uhitaji kwani walionyimwa urthi hujiweka kando na kushindwa kuwasaidia wahitaji. Jamii ibadilike tuweke mazingira bora kwa tutakao waacha.

Najua kutenganishwa na nduguzo ni kitu kinachouma Mungu akutie nguvu tu uweze kuchukuliana nao
 
Unachozungumza nakielewa kwa kina . Kuhusu uhusiano na hao ndugu zako muombe tu Mungu wawe waelewa kwani walio wengi huwa wanafiki na hasa hujenga urafiki wakiangalia maslahi yao, wapo watakaofanya urafiki nawe ili kuona unasema nini juu ya kilichotokea. Tena ndugu wa aina hii ijapokua si wote hufuata mawazo ya mama yao na wewe huonekana adui .

Kwa bahati mbaya wazazi kadhaa hukosa hekima kwani hapakua na shida ya kukupa nawe sehemu yako hata kama ni ndogo. Wazazi wanaopitia humu na wenye watoto mchanyanto wajitahidi kuzuia majeraha dizaini hii kwani kasoro hii husababisha vizazi na vizazi kuwekeana chuki.

Ni kweli hupaswi kutegemea urithi lkn ni haki yako kurithi sababu haturithi kwa sababu hatuna uwezo bali tunarithi kwa sababu ni warithi sina namna ya kuiweka hii. Kama mzazi utakua na hekima basi ni bora kuwaweka watoto pamoja na si kuwabagua. Migogoro ya aina hii wanaomumia zaidi ni watoto hasa wenye uhitaji kwani walionyimwa urthi hujiweka kando na kushindwa kuwasaidia wahitaji. Jamii ibadilike tuweke mazingira bora kwa tutakao waacha.

Najua kutenganishwa na nduguzo ni kitu kinachouma Mungu akutie nguvu tu uweze kuchukuliana nao

Ubarikiwe
 
lamsingi muombee baba yako kwanza, nahisi hatumii mawazo yake tena. mzazi ukiwa na uhusiano mzuri na mtoto tena wewe ni mkubwa na umesoma angeweza tu kushauriana na wewe na ukaridhia ye awape wadogo zako bila kukupa hata sumuni kiroho safi, lakini hicho kilichotendeka kwenu ni zaidi ya mgawanyo wa mali. jaribu tu kuirudisha hiyo hali lakini kwa busara na taratibu.hao ni wadogo zako.muombee baba yako kwanza afunuliwe awekwe huru ili familia yenu isiwe na mpasuko
 
lamsingi muombee baba yako kwanza, nahisi hatumii mawazo yake tena. mzazi ukiwa na uhusiano mzuri na mtoto tena wewe ni mkubwa na umesoma angeweza tu kushauriana na wewe na ukaridhia ye awape wadogo zako bila kukupa hata sumuni kiroho safi, lakini hicho kilichotendeka kwenu ni zaidi ya mgawanyo wa mali. jaribu tu kuirudisha hiyo hali lakini kwa busara na taratibu.hao ni wadogo zako.muombee baba yako kwanza afunuliwe awekwe huru ili familia yenu isiwe na mpasuko

Asante ndugu kwa mchango wako.Natamani iwe hivyo ila ndugu zangu nahisi hawako tayari kwa hilo.
 
Kama wao walikimbia shule kama unavyosema, baasi wewe ndo una mali kubwa kuliko wewe,huo mtaji wa elimu baba yaki aliyokupa utumie vizuri.
Mi nilishawahi kuambiwa na mdingi "Urithi ninaokupa ni elimu" duu mzee ikabidi nikomae mpaka nilipofikia, nashukuru, ulikuwa ni urithi sahihi.
 
Acha mawazo ya kijinga mzazi wako jukumu lake ni kukutunza ili ujitegemee na sio kukupa urithi wa mali amekupa elimu ina tosha, mtu kaamua kugawa mali zake alizotafuta, sasa akuombe ushauri wa nini! Amezitafuta mwenyewe sasa wewe unamiuza kichwa eti hakukushirikisha! Je kutafuta ulimsaidia? Nyinyi ndio mnaombe wazazi wenu wafe mpate urithi. Tafuta mali zako kama alivyotafuta mzazi wako.
 
Ushukuru MUNGU umesoma;
.............. mwendee mzee wako na rungu, mwambie apangue huo mgao la sivyo ama zako ama zake............
 
Mwenye tatizo ni babako. Kwani angeugomea ushauri wa huyo mama, ingekuwaje? Hata hivyo, jitahidi usimwekee kinyongo yeyote ndani ya familia itakusaidia sana. Ujue mikasa ya namna hiyo haijakupata wewe tu ndugu.
 
Siku zote usihesabu mali ya wazazi wako kama ya kwako pamoja na kwamba mzazi hurithisha wanaye mali...

Umepata urithi mwema usiotolewa na mzazi nao ni elimu, ni wakati sasa wa kuitumia...
Urithi wa mtoto ni elimu tu. Mengine gelesha tu. Urithi unaleta uvivu wa kufikiri na maendeleo na mtu yeyote anayeshabikia urithi ni wa kuogopwa zaidi ya ukoma katika karne hii.
 
lamsingi muombee baba yako kwanza, nahisi hatumii mawazo yake tena. mzazi ukiwa na uhusiano mzuri na mtoto tena wewe ni mkubwa na umesoma angeweza tu kushauriana na wewe na ukaridhia ye awape wadogo zako bila kukupa hata sumuni kiroho safi, lakini hicho kilichotendeka kwenu ni zaidi ya mgawanyo wa mali. jaribu tu kuirudisha hiyo hali lakini kwa busara na taratibu.hao ni wadogo zako.muombee baba yako kwanza afunuliwe awekwe huru ili familia yenu isiwe na mpasuko
Unaongea kwa upande wa mama ila kwa sie wanaume mke ana nguvu sana. Mke akimchukia mtoto na sie tunafuata. Hivyo kwa hali hiyo anatakiwa amwombee Mama yake wa kambo afunuliwe ili baba yake abadilike.
 
Mtaji wa maisha yake ni Elimu yako. Utafanikiwa. Ulisikia msemo Mali bila daftari hupotea bila habari. Ndugu zako wamekataa masomo wakapenda Mali basi hii methali inawahusu! Songa Mungu atakupigania.
 
Komaa mwenyewe mkuu...start from the bottom mzee. Hizo mali za wazee ndio zinaponzaga watu. Kama mimi hata nisingefungua mdomo wangu kuulizia.
 
Yameongelewa mengi mazuri pole ndugu mwisho kujazia waeleze ukweli kwamba walichofanya hujapenda labda kuna sababu kuu utaelezwa na kuona haina haja ya kukasirika,mimi mtu yeyote akinikwaza namueleza ukweli siangalii umri ila busara inatumika kuongea na baba na mama,mateso wengi tumepitia yanatupa kovu ila ukweli unabaki ni ndugu zetu.Pole sana
 
Mimi ni kijana nina ndugu zangu tunakutana kwa baba ambao ni 7 wakike 5 wanaume ni 2 mimi mama yangu amefariki nikiwa na miaka 5 nimelelewa na ndugu tofauti.

Nilipofikia umri wa kuanza shule baba yangu alinichukua ili niwe nae karibu,lakini mateso niliyokuwa nayapata kwa huyu mama hayaelezeki.

Baba yangu alikuwa ananipenda kuliko watoto wake wote kwa sababu ndio nilikuwa mtoto wake wa kiume mkubwa.Nilipofika darasa la nne baba yangu mdogo alinichukua baada ya kuona mateso yamezidi na pia baada ya mkewe kumshauri kufanya hivyo.

Kwa kweli pale kwa baba yangu mdogo nilikaa kwa raha yule mama yangu mdogo alinilea kwa upendo wote,nimesomeshwa mpaka namaliza chuo,kwa kweli mungu amuweke huyu mama ili afaidi mafanikio.

Lakini nikaamu kurudisha mahusiano kwa mama yangu wa kambo na ndugu zangu si unajua damu nzito.Lakini kitendo alichofanya huyu mama ndicho kinachokata mahusiano rasmi mimi na yeye.

Kwani amemshawishi baba yangu kagawa mali kwa ndugu zangu bila kunishirikisha mimi.Kwa kweli imeniumiza sana,nimemueleza mama yangu mdogo kwa kweli machozi yamemtoka.

Ushauri: je, nifanyeje na pia mimi ndo nimepata bahati ya kusoma ndugu zangu wote wamekataa shule.
Mnapoleta mada km hizi muwe mnaainisha na hayo mateso. Hii ni dhana mbaya sana ambayo inaendelea kwenye jamii yetu kuhusu mama wa kambo. Kitu ambacho ww hukijui ni kwamba,yule mama alikufundisha vizuri zaidi pengine kuliko hata watoto wake ndo maana hata shule umesoma.

Wamama wa kambo huwa na wakati mgumu sana wa kulea watoto wa aina yako,jamii imejenga mtizamo hasi kuhusu hawa akina mama! Hata wewe kauli zako tu zinaonyesha umeumizwa na hayo mawazo potofu. Umeandika huyo mama kamshauri baba yako,kwa nn hukumlaumu baba yako moja kwa moja!?? Sioni kabisa maantiki ya malalamiko yako, wewe umesoma wadogo zako hawajasoma,baba kaamua kuwapa urithi we bado unaona wivu! Hiyo mali ni ya baba yako ana hiari ya kumpa yoyote we tafuta za kwako…
 
Eti unalilia mali ya baba...!? Kubwa zima ila akili kidogo, sasa baba ako asipokufa mapema je!?

Kakae na ww tafta zako au na baba ako aliridhi ndio mana na ww unataka!? Na ukiridhi vitu vya baba yako, je watoto wako wataridhi kipi hasa cha jasho lako!?

Nahisi na baba mdogo wako akitoa mgao wa mali utautaka mana ulimpa heshima ya mzaz..!!
 
Back
Top Bottom