Apologise lady
JF-Expert Member
- Sep 16, 2013
- 5,980
- 3,115
Fanya kazi zako kwa bidii, na usiwe na kinyongo na yaliyotoke. hii dunia tunapita tu mambo ya urithi ni ubatili tu.
acha kupoteza muda wewe upendo usilazimeishe acha uje automatic that all
Namuomba mungu anipe subira na uvumilivu katika kipindi hiki kigumu na pia anipe moyo wa kutokata tamaa katika utafutaji.
kaka uzuri umeshawajua rangi zao zote
nakushauri ishi nao kwa tahadhari sana ndugu zako
tena usijilazimishe wakupende ht kidogo hao wabaya sana
we cha msingi mradi una pakuanzia pigania vya kwako
wasaidie unapoweza hizo mali kitu gani bwana
utapata tu tena za kwako mwenyewe za jasho lako zinanoga hatariii
achana na msaga sumu huyo anajishtukia mana anajua watoto wake sifuri so anajiwahi
kua nae makini huyo israeli bro
nna situation km yako but i know how to play with their tunesAsante ndugu
Mimi ni kijana nina ndugu zangu tunakutana kwa baba ambao ni 7 wakike 5 wanaume ni 2 mimi mama yangu amefariki nikiwa na miaka 5 nimelelewa na ndugu tofauti.
Nilipofikia umri wa kuanza shule baba yangu alinichukua ili niwe nae karibu,lakini mateso niliyokuwa nayapata kwa huyu mama hayaelezeki.
Baba yangu alikuwa ananipenda kuliko watoto wake wote kwa sababu ndio nilikuwa mtoto wake wa kiume mkubwa.Nilipofika darasa la nne baba yangu mdogo alinichukua baada ya kuona mateso yamezidi na pia baada ya mkewe kumshauri kufanya hivyo.
Kwa kweli pale kwa baba yangu mdogo nilikaa kwa raha yule mama yangu mdogo alinilea kwa upendo wote,nimesomeshwa mpaka namaliza chuo,kwa kweli mungu amuweke huyu mama ili afaidi mafanikio.
Lakini nikaamu kurudisha mahusiano kwa mama yangu wa kambo na ndugu zangu si unajua damu nzito.Lakini kitendo alichofanya huyu mama ndicho kinachokata mahusiano rasmi mimi na yeye.
Kwani amemshawishi baba yangu kagawa mali kwa ndugu zangu bila kunishirikisha mimi.kwa kweli imeniumiza sana,nimemueleza mama yangu mdogo kwa kweli machozi yamemtoka.
Ushauri je nifanyaje na pia mimi ndo nimepata bahati ya kusoma ndugu zangu wote wamekataa shule.