Naombeni ushauri wenu

Naombeni ushauri wenu

Mmmh aise ndo mana nachukia wanaume saa zingine....
huo muda wa kumvulia mtu chupi..bora nimwagie mkaa wa moto huku chini,washezi sana aisee acha nilale wananitolea upako wangu wa church
 
Mmmh aise ndo mana nachukia wanaume saa zingine....

Wakati mwingine chuki juu ya wanaume haisaidii. Huyu GF wa pili ni kitu kipi kilichompelekea hata akanasa ujauzito??
Unajua kipenzi, wadada huwa wanajisahau sana haswa wanapokaribishwa na kuishi kwa mwanaume. Kosa namba moja ambalo mdada wa watu atalijutia ni kuamua kunasa mimba na mtu ambaye hakuwa naye kwenye ndoa.
 
Mapenzi ni game ambayo haina mshindi, unapoachwa au kulizwa jua kuna mwingine anashangilia ushindi elsewhere na hilo halijalishi jinsia.
Mapenzi ni mchezo unaohitaji wachezaji wawili ambao ambao huitaji kucheza fairly, mmoja akifanya faulo tu basi kaharibu mchezo.
Therefore, huitaji kuwachukia wanaume as long as there's someone special out there who was ment to be yo game partner...

Dahhh mwanamke mwingine Yuko kibra kuchinjwa/kutendwa. I hate you MEN but I can't avoid YOU.
 
endelea na huyo mwenye mtoto.Huyo wa kwanza anakuzingua tu.anataka akuharibie maisha.
 
Ndio watu wajifunze hapa kuwa zinaa nje ya ndoa ni hasara siku zote, sasa ushauri wwt hapa utakuwa mgumu tu, lkn ukiwa wewe ni mpenda haki basi yule uliempa mimba ndio ana haki zote za kutizamwa na wewe kimaisha na huyo anaekuja ni mwanao, sasa acha tama za kipuuzi, mshiaka mbili!!
 
kwa sababu hawataki both kuondoka,wamege wote mpaka yule atakaeona hawezi ndoa ya mitala atajiondoa mwenyewe

Watarogana au utakuta siku wamechomana visu so huu sio ushauri kabisa.
 
Wakati mwingine chuki juu ya wanaume haisaidii. Huyu GF wa pili ni kitu kipi kilichompelekea hata akanasa ujauzito??
Unajua kipenzi, wadada huwa wanajisahau sana haswa wanapokaribishwa na kuishi kwa mwanaume. Kosa namba moja ambalo mdada wa watu atalijutia ni kuamua kunasa mimba na mtu ambaye hakuwa naye kwenye ndoa.

Mpenzi unazungumza kama vile huyo dada hiyo mimba kajidunga mwenyewe, wewe huoni kama mwanamme mwenzio alirukia mapenzi kwengine ingalli anampenda mpenzi wake wa mwanzo, huoni kama huyo dada watu anaumizwa kuwa hahusiki na matatizo yao lakini anaishia kuumia yeye na mtoto wake, huoni kama huyo jamaa hata akiamua kuishi nae hatokuwa na mapenzi ya kweli, huoni kuwa juu ya kuwa ni mzazi mwenzie lakini ana nia ya kumtosa kijijini ili achukue uhuru wake, huoni kuwa hana hata sense of guiltinesss maana tatizo alilokuja nalo ni kuwa mamamtoto kagoma kuondoka, huoni kama amedhalilisha wanawake kwa kuwapanga kama samaki.......@ watu8
 
Last edited by a moderator:
Mpenzi unazungumza kama vile huyo dada hiyo mimba kajidunga mwenyewe, wewe huoni kama mwanamme mwenzio alirukia mapenzi kwengine ingalli anampenda mpenzi wake wa mwanzo, huoni kama huyo dada watu anaumizwa kuwa hahusiki na matatizo yao lakini anaishia kuumia yeye na mtoto wake, huoni kama huyo jamaa hata akiamua kuishi nae hatokuwa na mapenzi ya kweli, huoni kuwa juu ya kuwa ni mzazi mwenzie lakini ana nia ya kumtosa kijijini ili achukue uhuru wake, huoni kuwa hana hata sense of guiltinesss maana tatizo alilokuja nalo ni kuwa mamamtoto kagoma kuondoka, huoni kama amedhalilisha wanawake kwa kuwapanga kama samaki.......@ watu8


Ni kweli kipenzi uliyoyaandika yote yana maana, na sio kwamba huyu mwanaume mwenzangu sioni kama amekosea.
Kiukweli ni kwamba kakosea sio kidogo kwani ameshapoteza muda wa mwenzake pengine na ndoto za dada wa watu.
Mimi ni mwanaume lakini huwa nashangaa sana watu wa aina hii, ambao hufikia maamuzi ya kuzaa na mwanamke pasipo kuwa na uhakika wa matarajio yao.
Laiti kama angalikuwa anajua namna huyo mwanaye mtarajiwa atavyokuja mchukia, wala asingalikuwa na mawazo ya kuachana na mama kijacho.
 
My friend, haya mambo huwa yana laana mbaya sana katika maisha. Asikudanganye mtu, kama mpenzi wako wa kwanza alikukataa na akaonywa na wazazi wake akagoma, kwa hakika huyo hana sifa ya kuwa mke. Ipo siku atafanya jambo lingine baya na gumu kwenye ndoa, na hatashaurika.

Na zaidi ya yote, ni vema sana kutoruhusu nafasi ya kuwa na mtoto wa nje ya ndoa. Kitendo cha kumtelekeza huyu uliyezaa naye na kuamua kumuoa aliyekukataa awali, ni kuruhusu kuwa na mtoto nje ya ndoa, ambaye yumkini huyu utakayemuoa hatakuwa tayari hata kumuona, sijui kama utakuwa unajisikiaje kuona mtoto wako anateseka huko aliko? Je kama huyu aliyekukataa akiamua kuzaa na yeye nje ya ndoa na kukuambia kwamba mbona hata wewe una mtoto nje ya ndoa, utafanyeje? Mara nyingi sana wanaume huwa tunawaacha wanawake innocent na kuoa wanawake wakorofi ambapo mwisho wa siku tunakumbuka na kujutia sana maamuzi yetu. Ningekuwa mimi ningemuoa huyo mwenye mtoto dispite ubaya wake wa sura, umbo au mapungufu mengine. Maana hujui ni kwanini Mungu kakuletea huyo.

Hujiulizi ni kwanini huyo mpenzi wako wa zamani hakutokea kupata mimba kwa miaka yote uliyoishi naye? Ukimfukuza huyu na kumuoa huyo mwingine halafu ukakuta hazai utafanyeje? Wapo wengi sana wamezijutia ndoa zao kutokana na maamuzi kama haya yako. Unamwacha mtu uliyezaa naye eti kwa kwua labda hana elimu, eti hana sura nzuri na mengine mengi ambayo hayadetermine mke bora? Hiyo itakugharimu. Mimi napendekeza kama huyu uliyezaa naye ana mapungufu, basi jaribu kuyarekebisha, na uishi naye huyo.
 
Kaka, nakushauri ufuate ushauri wa LUKOLO maana kamaliza kila kitu. Ukimrudia huyo aliyekukataa wewe utakuwa unajichimbia kaburi lako mwenyewe. Kama huamini fanya hivyo then naamini utakuja jf tena ukileta malalamiko ya huyo aliyekukataa maana huwajui wanawake wewe*sasa ndo unataka uwajue.
 
Nilikuwa na mchumba wangu wa siku nyingi,tukajuana tabia,tukaridhiana akanitambulisha kwao nikamtambulisha kwetu wazazi wetu waliridhia na kutuombea mema ili tujipange tuje tufunge ndoa. baadae tukaja kupishana na huyu mchumba wangu akanitamkia kuwa niwe huru nimtafute tu msichana mwingine.

wazazi wake wakadokezwa taflani ya mahusiano yetu wakamkalisha chini na kumwomba afikirie kabla ya kuchukua maamuzi.akasema nabaki na msimamo wangu. baada ya miezi kama miwili nikampata dada mmoja nikaingia nae kweny mahusiano na bahati nzuri hyu msichana akapata ujauzito bila ya kufunga ndoa.

Baadae yule msichana wa kwanza akaja kuniomba msamaha na ndugu zake wakanisihi sana kuwa tusiachane.kwa kweli nipata wakati mgumu sana kimawazo na ukweli msichana anabusara, hekima,mpole,na mwaminifu sana lakini nikasema itakuwaje na huyu msichana mwenye mimba?kabla sijafanya maamuzi nikawashirikisha wazazi wang ili wanipe ushauri.wazazi wakaniuliza mm mwenyewe nimemwona yupi ni bora zaidi ya hawa wawili? nikawajibu ni huyu wa kwanza hata kama tulipishana.nikapata wakati mgumu sana kumweleza dada mwenye ujauzito ambae baadae akajakujifungua mtoto wa kike.

Ili nimweke wazi msimamo wangu. ingawa nilijua nimemkosea sana.kama binadamu nilikiri makosa yangu kwake.nilipomweleza kwa mara ya kwanza akakataa akasema hataki kusikia hilo.kwa kweli iliniuma sana roho ya huruma ilinijia hasa baada ya kujua yeye hana makosa ingawa anamapungufu yake ingawa si sawa na ya yule wa kwanza ingawa wote wana mapungufu yao ya kibinadamu.

Lakini ndugu zangu ukweli toka nafsini mwangu nahitaji na nampenda zaidi na nataka kumwoa mwanamke yule wa kwanza kwani nilikaa nae nikamweleza kila kitu kilichotokea akasema yaliyopita si ndwele tugange yajao.kwa kuwa huyu mwenye mtoto alikuwa yupo nyumbani ili kuangalia ustawi wa mtoto sasa nataka nimrudishe kwao ili nitimize ndoto zangu za kuwa na mke wa nafsi yangu.mwanamke mwenye mtoto hataki kurudi nyumbani.nifanyeje?

Naombeni mawzo yenu yenye hekima ili amani ipatikane kwake na kwangu pia. WA SALAAM NDUGU ZANGU.

email_open_log_pic.php

Kuna maswali mapana sana ya kujiuliza as a man!!
1.(a)kwann yule wa kwanza alikuacha na (b)kwann alirudi tena (c)vp huyu aliekusitiri wakati wa taabu hadi mimba!!
2.nn kipaumbele chako katika mahusiano as a man!!!!!
 
Wanaume pls if u can't make her your wife don't make her a mother...

Nna uhakika huyo dada hukumpenda alikua tu stress remover wako sema ukabug kupiga kavu

Ila kwa vile u are talking about your lifetime happness mwambie utakua responsible kwa mtoto in each n everything then oa atakaekupa happness,hamna haja ya kuoa kwa kigezo cha mtoto then ukaishi maisha ya stress matokeo yake ndoa yako ikiwa na miez miwili tu utaanza kutoka nje so don't even think about it

Zingatia kumtimizia huyo mtoto wako needs zake zote asije akateseka coz hana kosa lolote kwa hiyo mikorogo yenu
 
Kama najiona vile kwenye hiki kisa.
Nahofu mtoa uzi labda ni rafiki yangu ameamua kuweka jambo hili wazi kwa ID mpya.
Jamani mie nahusika moja kwa moja na habari hii.
 
Ndugu jamaa na marafiki wamekushauri mambo mengi na mazuri pia. lakini wapo wanaokutangazia laana endapo utamwacha huyo mwanamke uliyemzalisha. Laiti kama Mungu angenipa uwezo ningeungana nao lakini sina mamlaka.

Any way. amua mwenyewe. Hata hivyo huyo anayekufanya umtelekeze mwanao si alikukataa mwenyewe mbele ya wazazi wake?

HIVI UNAJUA YA GHARAMA MTOTO KULELEWA NA MAMA WA KAMBO?

HATA HIVYO, NIKUPE TAARIFA KWAMBA HUYO MWANAMKE ALIYEKUKATAA KIPINDI HICHO ALIMPATA MTU MWINGINE, HUYO MTUA HUENDA KWA SABABU MOJA AU NYINGINE AMEMTEMA NDO MAANA ANARUDI KWAKO.

FANYA MAAMUZI KWA KUTAFAKARI KWA KINA OUTCOMES ZA MAAMUZI YAKO KWA FYUCHA YA MWANAO.

WEWE NI MWANAUME USIPELEKESHWE NA UPEPO.
 
Hapo nilibold, nawaza kipuuzi tu,
  • Mwenzako alionyesha msimamo kwa maamuzi aliyoyafanya hata kama hayakuwa sahihi, iweje wewe unayetegemewa kuwa baba wa familia ukakosa msimamo na kuyumbishwa kirahisi hivi?
  • Utaweza kweli kuilinda na kuitunza familia yako kwa matendo kama haya?
  • Ukimkubali tena na yeye akaja kupata mwingine akaamua kukumwaga, utafanyaje?
  • Maisha ya mwanao, umeyafikiria?
  • Huyo mwanamke uliyempa mimba na kumzalisha akaolewe na nani?
  • Uliharakisha nini kwenda kumpata mwingine?
Nina mashaka (ingawa sipendi iwe hivyo) kuwa huenda wewe ndo wale baadhi ya wanaume ambao wakisha oa na kuishi na wake zao, hawana la kusema, wanaburuzwa kama mazoba.

Mwenzako alipoulizwa na wazazi wake alisema anabakia na msimamo wake, wewe je? Tafakari, chukua hatua!

Asante, to be aman means to be adiff thing in desicion making most important is to be wise
 
kama najiona vile kwenye hiki kisa.
Nahofu mtoa uzi labda ni rafiki yangu ameamua kuweka jambo hili wazi kwa id mpya.
Jamani mie nahusika moja kwa moja na habari hii.
kwa hiyo umeamuaje
 
Back
Top Bottom