hahaha ila peku tamu jamani lol
Halafu wewe ukiwaga serious una mapwoint kweli.
Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums
Nilikuwa na mchumba wangu wa siku nyingi,tukajuana tabia,tukaridhiana akanitambulisha kwao nikamtambulisha kwetu wazazi wetu waliridhia na kutuombea mema ili tujipange tuje tufunge ndoa. baadae tukaja kupishana na huyu mchumba wangu akanitamkia kuwa niwe huru nimtafute tu msichana mwingine.wazazi wake wakadokezwa taflani ya mahusiano yetu wakamkalisha chini na kumwomba afikirie kabla ya kuchukua maamuzi.akasema nabaki na msimamo wangu. baada ya miezi kama miwili nikampata dada mmoja nikaingia nae kweny mahusiano na bahati nzuri hyu msichana akapata ujauzito bila ya kufunga ndoa.baadae yule msichana wa kwanza akaja kuniomba msamaha na ndugu zake wakanisihi sana kuwa tusiachane.kwa kweli nipata wakati mgumu sana kimawazo na ukweli msichana anabusara, hekima,mpole,na mwaminifu sana lakini nikasema itakuwaje na huyu msichana mwenye mimba?kabla sijafanya maamuzi nikawashirikisha wazazi wang ili wanipe ushauri.wazazi wakaniuliza mm mwenyewe nimemwona yupi ni bora zaidi ya hawa wawili? nikawajibu ni huyu wa kwanza hata kama tulipishana.nikapata wakati mgumu sana kumweleza dada mwenye ujauzito ambae baadae akajakujifungua mtoto wa kike. ili nimweke wazi msimamo wangu. ingawa nilijua nimemkosea sana.kama binadamu nilikiri makosa yangu kwake.nilipomweleza kwa mara ya kwanza akakataa akasema hataki kusikia hilo.kwa kweli iliniuma sana roho ya huruma ilinijia hasa baada ya kujua yeye hana makosa ingawa anamapungufu yake ingawa si sawa na ya yule wa kwanza ingawa wote wana mapungufu yao ya kibinadamu.lakini ndugu zangu ukweli toka nafsini mwangu nahitaji na nampenda zaidi na nataka kumwoa mwanamke yule wa kwanza kwani nilikaa nae nikamweleza kila kitu kilichotokea akasema yaliyopita si ndwele tugange yajao.kwa kuwa huyu mwenye mtoto alikuwa yupo nyumbani ili kuangalia ustawi wa mtoto sasa nataka nimrudishe kwao ili nitimize ndoto zangu za kuwa na mke wa nafsi yangu.mwanamke mwenye mtoto hataki kurudi nyumbani.nifanyeje? naombeni mawzo yenu yenye hekima ili amani ipatikane kwake na kwangu pia. WA SALAAM NDUGU ZANGU.
![]()
Ukisikia kulikoroga ndo huku
uko tayari kumtesa mwanao sababu ya 'kumuabudu' huyo mwanamke
ndo maana wengine tumeamua kuwa watawa ewa kujitegemeaDahhh mwanamke mwingine Yuko kibra kuchinjwa/kutendwa. I hate you MEN but I can't avoid YOU.