Diwani
JF-Expert Member
- Oct 25, 2014
- 2,672
- 2,697
Bila shaka mu wazima na shughuli za maendeleo wana jamvi.
Ni takribani miaka mitatu sasa tangu nimekabidhiwa nyumba ya urithi, nyumba iliyokuwa chini ya uangalizi wa walezi wangu kwa muda mrefu.
Jengo la nyumba ni chakavu, nina lengo la kuikarabati ili niipandishe thamani ya ukaazi kwa wapangaji, mimi sikai hapo. Fursa niliyoona ni kwamba, nyumba ipo karibu na makazi ya daharia (hostels) za wanafunzi, kwa utafiti wangu, hitaji la vyumba kwa wanafunzi ni mkubwa aidha baada ya kukosa vyumba, ama baada ya muda wa kukaa kufika.
Mzunguko wangu wa kipato bado mdogo, kwa tathmini ya haraka, marekebisho yanaweza kufika kiasi cha 10 Milioni mpaka 12 Milioni; pesa ambayo sitaweza kuipata kwa shughuli nifanyayo.
Sina mpango wa kuiuza (kama lingekuwa shauri) nina mpango wa ukarabati, naomba msaada wa namna gani, naweza pata kiasi hiko nilichokadiria, na wapi (kwa maana ya taasisi ipi ya fedha). Asanteni
Karibu
Ni takribani miaka mitatu sasa tangu nimekabidhiwa nyumba ya urithi, nyumba iliyokuwa chini ya uangalizi wa walezi wangu kwa muda mrefu.
Jengo la nyumba ni chakavu, nina lengo la kuikarabati ili niipandishe thamani ya ukaazi kwa wapangaji, mimi sikai hapo. Fursa niliyoona ni kwamba, nyumba ipo karibu na makazi ya daharia (hostels) za wanafunzi, kwa utafiti wangu, hitaji la vyumba kwa wanafunzi ni mkubwa aidha baada ya kukosa vyumba, ama baada ya muda wa kukaa kufika.
Mzunguko wangu wa kipato bado mdogo, kwa tathmini ya haraka, marekebisho yanaweza kufika kiasi cha 10 Milioni mpaka 12 Milioni; pesa ambayo sitaweza kuipata kwa shughuli nifanyayo.
Sina mpango wa kuiuza (kama lingekuwa shauri) nina mpango wa ukarabati, naomba msaada wa namna gani, naweza pata kiasi hiko nilichokadiria, na wapi (kwa maana ya taasisi ipi ya fedha). Asanteni
Karibu