NAOMBENI USHAURI WA KINA KUHUSU HILI.

NAOMBENI USHAURI WA KINA KUHUSU HILI.

Niache 2

Member
Joined
Aug 7, 2017
Posts
69
Reaction score
34
Habari Za Wakati Huu Wanajf!
Ni Matumaini Yangu Mu Wazima.

Niende Kwenye Point, Natokea Kijiji Fulani Wilayani Monduli, Na Hatukuwa Na Shule Ya Msingi Hivyo Tulilazimika Kutenga Eneo Na Baadaye Kuchangia Katika Ujenzi Wa Shule.
Tulifanikiwa Kujenga Madarasa Mawili Na Tukapata Wafadhili Nao Wakajena Madara Manne Na Toilet.

Sasa Hawa Wafadhili Wanakuja Kwa Kugha Nyingine Na Wanaomba Hii Shule Waifanye English Midium Kwa Madai Ya Kusema Watoto Kwa Hichi Kijiji Hawatalipia Chochote(yaani Watafadhiliwa) Ila Wengine Watalipa.

Point,! Kijiji Kimejigawa Hivyo Kuna Mdahalo Sasa Maana Kuna Wanaokubali Na Wanaokataa Je Wajf,tuwape Waifanye English Medium Ama Hapana?

Naombeni Ushauri Wa Kina Tafadhali,
 
Hilo nalo ni la kuomba ushauri, umewahi kuona wapi watoto wa viongozi au matajiri wanasoma shule za kata, hiyo ni bahati mmepata mfadhili wa kuwajengea English media kijijini, jibaneni msomeshe watoto wenu
 
Muwaruhusu waifanye English medium, itakua bora zaidi kwa watoto wenu. English medium kijijini si haba!

Cha msingi ni kwamba mnatakiwa kua na mwanasheria atakaesimamia zoezi zima la makabidhiano pamoja na mikataba.

Kwakua wataendesha shule kibiashara, hata serikali ya kijiji inaweza kunufaika kwa kupata fungu.

Ni wazo zuri kuwapa hao jamaa hiyo shule, ila kuweni macho kwenye ishu ya mikataba!
 
Hilo nalo ni la kuomba ushauri, umewahi kuona wapi watoto wa viongozi au matajiri wanasoma shule za kata, hiyo ni bahati mmepata mfadhili wa kuwajengea English media kijijini, jibaneni msomeshe watoto wenu
HUjui nchi hii inavyoendeshwa ...
Mfadhili alikuja sehemu (jijini Mwanza pembeni) akapewa ardhi kwa kuwadanganya wananchi kwamba watoto wao watasoma kwenye hiyo shule bure.
Hadi sasa ninapoandika hii kitu, hakuna hata mtoto mmoja alowahi kupokelewa hapo. Hii ndiyo Tanzania kama ulikuwa hujui, jua leo.
 
JIulizeni maswali haya:-
Shule itakuwa chini ya umiliki wa nani? Mfadhili / wanakijiji / serikali (usajili)
 
HUjui nchi hii inavyoendeshwa ...
Mfadhili alikuja sehemu (jijini Mwanza pembeni) akapewa ardhi kwa kuwadanganya wananchi kwamba watoto wao watasoma kwenye hiyo shule bure.
Hadi sasa ninapoandika hii kitu, hakuna hata mtoto mmoja alowahi kupokelewa hapo. Hii ndiyo Tanzania kama ulikuwa hujui, jua leo.
Soma vizuri maelezo yangu bila kukurupuka wapi nimesema wasome bure sanasana wajibane
 
Ni wapi hujaelewa ili nikueleweshe. Nimechangia kwa kutoa mfano hai - hujaelewa unataka nikueleweshe kwa njia gani?
Kwamba mwekezaji aliwaahidi kuwa watasoma English media bure na wao wakakubali na kutegemea kusoma bure
 
Back
Top Bottom