Naombeni ushauri kuhusu huyu mdogo wangu

Naombeni ushauri kuhusu huyu mdogo wangu

Bi mkubwa nimeongea nae juzi tu tena nilkuta 5 missed calls zake nikampigia tukasalimiana na nikamkumbushia kuhusu suala la mdogo wangu kwenda chuo akasema haina shida kabisa sasa leo yan sjui ata imekuaje na sielewi.

Napanga nikitoka Kwenye mishe zangu nimpigie nimsikilize anasemaje tena.
Vizuri pia mfunze dogo asimkwaze mama

Pia unaeza kuta dogo hana subira ukute kila saa yeye anamkumbushia chuo chuo mpaka mama wawatu anashindwa kupumua anaona hamjibu hamna shule

Be patient ila hakikisha unaenda law school.
 
Nakubaliana nawewe mkuu japo nilishaomba Law School nikapangiwa Intake ya July na hela tayari ipo ila bado naifanyia mizunguko kwenye biashara.

Itabidi nifuatilie kama kuna consequences zozote za mimi kutoripoti Law School Mwaka huu ili nijue nafanyeje mana apa nina stress ata uwezo wa kufikiri umepungua
Haina shida yoyote kuna bwa mdogo wangu aliomba 2018 akapata hakwenda. Akaomba 2021, akakubaliwa, akajiunga.
 
Kwa upande wa mama yangu tumezaliwa wawili tu yaani mimi na huyu mdogo wangu ila mama na mzee walishatangulia mbele za haki [mama kafariki nikiwa na miaka mi3 na mzee nikiwa na miaka 13 ]

huyu mdogo wangu Yeye yupo nyumbani anakaa na mama mkubwa ( step mother )

Sasa mimi ni Juzi tu nimemaliza chuo kwa mbinde sana mana nmejitegemea kila kitu miaka yote mitatu mpaka namaliza, sikuwa na wakumwelekezea shida zangu zozote ingawa kwa upande wa Baba tupo watoto 16 na sisi ndio wa mwisho na hawa ndugu zetu wote kila mtu ni mambo safi kweli ( kweli kutoa ni moyo 🥲)

Sasa huyu mdogo wangu kanitumia Hii meseji nimepatwa na stress sana wakati ni Juzi tu nmeongea na huyu mama mkubwa wangu tukakubaliana kuwa atampeleka mdogo wangu chuo ila ntakua nampa back up kwa vitu vidogo vidogo kama matumizi ya apa na pale.

Mimi saiv ndo nmeanza biashara bado hata sijafikia ile level ambayo nimejiwekea malengo nifikie lakini nakumbana na majukumu mazito kama haya.

Binafsi apa nilkua napambana nipate hela niingie Law school mwezi July lakini izo dalili naona kabisa zikififia🥲

Kinachoniuma ni mdogo wangu af ni mtoto wa kike na tumezaliwa wawili tu, Naombeni ushauri nifanye nini ili nijue namjibu vp huyu mdogo wangu in a positive way

View attachment 2469632
Mungu atafanya njia pasipo na njia. Ila ukiwa huna pesa unaweza ukammaindi mtu kwa ajili ya mwandiko wake.
 
Huyo dadako sasa ndio msomi hasa, anajua kujali muda, yanini kuandika miherufi mirefuuuu wakati in short tu inaeleweka?
Jitahidi asome yuko vizuri time is money
Mimi leo nimeamkia Hospitali mana Tangu Tarehe 2 najiskia hovyo nilzani ni hangover za pombe za sikukuu kumbe nilkua na Malaria.

Mimi mwandiko wako ndo utaniongoza nikujibu au nisikujibu.
Sipendi miandiko ya kitoto
 
Subira yavuta kheri
Hakuna barabara iliyonyooka
Ili ufanikiwe lazima upitie milima , kona na Mabonde. Lakini kufika ni lazima hata kama kuna kuchelewa ndani

Lakini ujue haya mambo huwa hayamkuti mbuzi wala kenge ni Binadamu kama mimi na wewe.

Enewei
Hata mimi sipendezwi na mtu anayetumia X badala ya S au C badala ya S naudhika kuliko maudhi yenyewe
Hata mbuzi na kenge yanawapata sema hatujui
 
Ndio inabidi umfundishe hiyo biashara ili ukienda kusoma aiendeleze kisha ukishamaliza law school unakuja kumpokea kijiti na yeye anakwenda chuo.
Forget about Step mother,forget about step brothers wewe ni mtu mzima sasa yaani chukulia ndio umeshaanza majukumu hivyo wewe ndio kaka,wewe ndio baba,wewe ndio mjomba kwa huyo mdogo wako.
Hiyo changamoto yako ni ndogo sana maana huyo mdogo wako naye ni mtu mzima anafundishika kirahisi.
Mimi nilianza kusomesha wadogo zangu kuanzia primary level wakamaliza,sekondary baadhi wakamaliza na kuna mmoja bado anaendelea na sekondary,wengine walimaliza kwenda chuo na wengine wanahitaji kwenda chuo sasa hivi ila ninachoshukuru Mungu likitokea jambo la dharura au shughuli yeyote wananisaidia mawazo na usimamizi kwenye utekelezaji mimi natoa mchango wa kipesa.
So nina uzoefu mkubwa wa hili jambo ninalokushauri.

Sent from my SM-C7000 using JamiiForums mobile app
Asante kwa ushauri mkuu ila kuhusu hii biashara nayofanya mdogo wangu haiwezi maana foundation yake nimeijenga kwa kunizunguka mimi [hope unanielewa]

Kuna biashara nilkua nataka kuanzisha mwezi February ila nilkua nataka kumwachia mchumba wangu ndo aiendeshe na tushapanga kila kitu bado tu location aanze kazi.

Sasa nipo njia panda maana kubadili gia hewani kumuweka dogo Kwenye biashara badala ya mchumba ni kizungumkuti.
 
Kwa upande wa mama yangu tumezaliwa wawili tu yaani mimi na huyu mdogo wangu ila mama na mzee walishatangulia mbele za haki [mama kafariki nikiwa na miaka mi3 na mzee nikiwa na miaka 13 ]

huyu mdogo wangu Yeye yupo nyumbani anakaa na mama mkubwa ( step mother )

Sasa mimi ni Juzi tu nimemaliza chuo kwa mbinde sana mana nmejitegemea kila kitu miaka yote mitatu mpaka namaliza, sikuwa na wakumwelekezea shida zangu zozote ingawa kwa upande wa Baba tupo watoto 16 na sisi ndio wa mwisho na hawa ndugu zetu wote kila mtu ni mambo safi kweli ( kweli kutoa ni moyo 🥲)

Sasa huyu mdogo wangu kanitumia Hii meseji nimepatwa na stress sana wakati ni Juzi tu nmeongea na huyu mama mkubwa wangu tukakubaliana kuwa atampeleka mdogo wangu chuo ila ntakua nampa back up kwa vitu vidogo vidogo kama matumizi ya apa na pale.

Mimi saiv ndo nmeanza biashara bado hata sijafikia ile level ambayo nimejiwekea malengo nifikie lakini nakumbana na majukumu mazito kama haya.

Binafsi apa nilkua napambana nipate hela niingie Law school mwezi July lakini izo dalili naona kabisa zikififia🥲

Kinachoniuma ni mdogo wangu af ni mtoto wa kike na tumezaliwa wawili tu, Naombeni ushauri nifanye nini ili nijue namjibu vp huyu mdogo wangu in a positive way

View attachment 2469632
Hujasema hicho chuo ni level gani, certificate ,diploma ama degree?

Hujasema pia chuo gani anataka kwenda kusomea hyo Nursing ili upewe muongozo nk
 
We si mfanya biashara
Nadhan kaanzishe kituo cha kusaidia watoto yatima.. sasa hapa unataka ushauri gan wakat kilakitu kimeishaa? Huna zoada

Binadamu wote tumeumbwa na kaubinafsi cha kujiangalia wewe kwanza then wengne baadae.
 
God can help you......
Mungu huwa hashughuliki na wajinga.. Mtu yoyote mwenye tabia ya kutofanya mambo madogo kwa ukamilifu hata kwa makubwa ni vile vile..
Kuna mtu kimasighara masighara nikapita kushoto.
 

Attachments

  • 20230105_130417.jpg
    20230105_130417.jpg
    185.2 KB · Views: 8
Hujasema hicho chuo ni level gani, certificate ,diploma ama degree?

Hujasema pia chuo gani anataka kwenda kusomea hyo Nursing ili upewe muongozo nk
Mimi sina ufahamu na mambo ya afya mkuu ila anataka akasomee nursing from the scratch mana ndo kazi anayoipenda
 
Back
Top Bottom