Naombeni mwongozo

rafiki salama?
umenielewa lakini?
sina shaka na treatment zangu kwa wadada, hata kama hunifahamu naomba nikuaminishe hilo.
hapa concern yangu ni moja tu, airtime ambayo nampa anipigie kukitokea dharura, na si kitu kingine.
huyu ni mdada wa nne kukaa naye. wa kwanza nilikaa naye kwa miaka 3 na wa pili miaka 9, mi5 akinisaidia kazi na mi4 nikimsomesha ili akitoka hapa aende akajitegemee akiwa na ujuzi wake, hili pia huna choice zaidi ya kuamini tu, lol!
watatu nimekaa naye miaka miwili na huyu sasa ndo mgeni. Hao watatu wote nilikuwa nimewatoa kijijini kwetu ambapo mpaka sasa wao wenyewe pamoja na wazazi wao tumekuwa kama ndugu, hawaachi kuja kunisalimu nikienda kijijini............
hapa naomba pia asome Miss Kim, Eiyer, Phlagiey, Toria, Mashaxizo na wengine
 
Last edited by a moderator:
Mimi nampa sababu huwa simpi hela ya matumizi sababu hakuna matumizi ambayo atayafanya, labda kama nimesafiri.
Masoko na maduka yapo mbali sana na nyumbani kwetu, sababu yeye hana usafiri basi nampunguzia kazi ya kuzunguka kwenda kununua mahitaji ya nyumbani, namletea kila kitu. Ndo maana nikaona hiyo hela ya airtime nimpe tu ingawa mimi mwenyewe ndo napiga sana simu nyumbani.
 
Mke wangu mwenyewe ana itikadi hizohizo...hii tabia inanikera kuliko zote duniani...!

Wanasahau maisha ya wanafamilia yapo mikononi mwa beki 3,anaweza akawapoteza wote wakati wowote...

Lazima tuishi nao kibinadamu...!
Ndo maana nikasema siwashangai wababa wanaosema hivi........
Kuanzia babangu mpaka mume wangu hawajawahi kujihusisha kabisa na maisha ya wasichana wa kazi, labda kama mama/mimi nimesafiri, ila kama tupo basi jukumu la wasichana ni la wamama.
changamoto tunazokutana nazo siwezi hata kuomba ushauri kwa mume wangu maana naye atanijibu kama ambavyo wewe, Eiyer na BAK mnanijibu, ndo maana nikaona nije kuomba mwongozo huku ambapo nitakutana na wamama ambao pia wanakutana na hizi changamoto.
BTW naomba sana munielewe, nazungumzia matumizi ya airtime ninazompa za dharura, siyo chakula, kazi wala malazi......
 
Last edited by a moderator:
najua kinacho kupa mashaka hasa ni usalama wa nyumbani kwako hasa ukiwa na mtoto, vocha mpe ila kiboko ya njia funga cctv pasipo yeye jua pia gharama yake ni kama laki nne ivi kwa maana ya kwamba utapata full matukio kama yafuatao
1. kama mtoto ana mtrit vibaya utajua
2.kama ana tabia ya kuleta vinjemba na kugeuza nyumba yako lodge utajua haraka
3.utajua matumizi ya simu yake kwa kusikia anaongea nn
4.kama mr anamkamua beki 3 nayo itakusaidia
5.kama anatabia ya upashukuna wa kuleta marafiki kwako utamjua
faida yake hata kama una panga chumba kimoja utapata taarifa za uhakika na kuzichukulia hatua fasta, nimefanya ivo adi beki tatu anaisi mie ni mchawi.....
 
Nimerelax rafiki
 
hii sasa kiboko........
Hiyo namba 4 ina maana hiyo cctv niifunge bila mr kujua? haya si yatakuwa majanga?
cc. Kaizer, The Boss, BAK, Eiyer, Mtambuzi, Tized ........
 
Last edited by a moderator:
Usimpe hela weka tu utaratibu wa kupiga kila siku mara mbili au tatu..au weka hela simu ya nyumbani sio yake

mkuu, 'simu ya nyumbani' ipi tena wakati cm yenyewe ndio hio anayokuwa nayo beki 3?
 

Exactly! Lakini ikitokea dharula atampataje 'mama'?
 
hii sasa kiboko........
Hiyo namba 4 ina maana hiyo cctv niifunge bila mr kujua? haya si yatakuwa majanga?
cc. Kaizer, The Boss, BAK, Eiyer, Mtambuzi, Tized ........
Habari rafiki.
Ku control matumizi ya simu kwa msichana ni magumu,ukimuwekea credit ataitumia tu hata kwa simu binafsi.
Kwangu kuna simu ya mezani,naweka credit hiyo tu na kuhakikisha ina charge ya kutosha ninapotoka. Akija bint mpya cha kwanza ni kumfundisha jinsi ya kuitumia na namba za kupiga ikitokea emergency.
Akija na yake au akinunua ataihudumia mwenyewe.
 
Last edited by a moderator:
Asante kwa kutaka muongozo.
Kwa mujibu wa kanuni za busara zinazoongozwa na uungwana ni kuwa;
Ma-boss wengine mna roho ya kutu!
Yaani unaona anapata saaana sio?
Kunya anye Kuku akinya Bata msala,
Jiulize boss wako wewe angekuwa ndio anapanga mikakati ya kukudhibiti kwenye vile vimianya vinavyokuingizia mapene ya ziada mbali ya mshahara ungeanza kulalama tena hapahapa.
Muache ajisikie nayeye yupo kazini bwana,
Mpe limit tu, Salio likifika kiasi fukani labda hakuna kupigia wengine ni wewe tu
Na wao wanahitaji kuwasiliana na dunia sio ukimuajiri ndio basi awasiliane na wewe boss tu.
Tunaendelea...
 
Asante rafiki......
Mimi nipo bomba, sijui wewe
 
ha haaaa, nina adabu sana kwa boss wangu....
Akinipa hela ninunue vitumbua nafanya hivyo, ya pipi vile vile......
Ila bahati mbaya boss wangu hanipi hela ya kumpigia simu, natumia hela yangu ya mshahara
 
Ukimchunguza sana bata hutamla,shukuru hayo maana ungesikia vitimbwi nya wadada wakazi sio mchezo sasa ww unataka aanze kukupigia yataendelea na mengine utapata taabu ndugu
 
umeni-judge kwa vitu nisivyovifanya......
hayo maandishi meusi ambayo umeyakimbia ndo nimesema mimi huwa nafanya, hayo mengine ni maelezo tu na nimeweka clear kuwa sifanyi hayo

Fixed Point!
We differ on how we understand and how we translates!

Maandisi yakiekewa red yanamaana yake!
Nilichojibu niliegemea kwenye maandishi yako mwenyewe! Kwa lugha nyepesi 1 (first red) + 1 (second red) = 2 (nilichokujibu) instead of 5 (ya maelezo yako underline) that is how lawyer makes inference from specific to general!

Hiyo haina maana kwamba ndivyo ufanyavyo! Hiyo ni tafsiri tu! Sikujui, hivyo sina uwezo wa kukujudge! Naomba unielewe kwa hilo!

And if umehisi nimekukosea naomba unisamehe!
Love you so much my dada!

I like the way you argue!
Pamoja sana!
 
Pole kwa changamoto best yangu.

Binafsi naamini sana kwenye kuzungumza na kukumbushana. Inaposhindikana kwenye kuzungumza ndio unatafuta njia nyingine mbadala.

Hawa wadada ni watu wetu wa muhimu sana, na tunawatoa kijijini (sote tunajua ukijiji ulivo na mtu pengine anakuwa hajawahi kutoka nje ya familia kwa muda) kwa hio akiongea kwa simu na nduguze/familia anafurahi kupita maelezo. yaani hata kama umekaa pembeni ukimwangalia... you feel the excitement... kwa mantiki hio sitegemei awe mtunzaji mzuri wa hela kwenye simu. au pengine ukimpa vihela ataenda tu kununulia vocha awasiliane na wa nyumbani... ila baada ya muda wanazoea. au pengine unampa hio hela anaenda kununu vitu vingine kwa maana wengi wao huwa hawapewi hata mia nje ya mshahara wao n.k n.k

Ningekushauri tu wewe mpe hio hela kwa maelezo ya kukutafuta anapokua na dharura, mfundishe pia namna ya kukutumia tafadhali nipigie n.k. Mweleze tu umuhimu wa kukujulisha dharura yeyote anayokua nayo halafu muache huru na kila akikubeep /plz call me, mpigie kwa wakati muoneshe kuapreciate. Next time mpe 2000 (mwambie 1000 atumie kwa matumizi yake ya simu na nyingine akupigie angalau mara moja moja anapokua na kitu cha kukuambia. kila anapokupigia muoneshe furaha yako ya yeye kukupigia ili kuendelea kujenga saikolojia yake kwenye kwa namna unavyojali simu yake etc.. over time she is there. Ukimuwekea sheria ya aina yeyote ndio utamwaribu maana itafika mahali hela imeisha afu kinatokea kitu anasema hela si imeisha... nakaa kimya (na ukiangalia kweli 1000 yote aliitumia kuongea na wewe)

Kingine pia waweza fanya kila akikupigia, kata umpigie wewe... inamjengea kitu kingine japo unampa hio 1000 lkn bado hutaki iishe kwako...

All the best... njia bora ya kukaa na hawa dada zetu ni kucheza na saikolojia zao.. ukiwa mkali ukaweka sheria sheria zako... wanakunasisha wewe mwenyewe bila kujua. Na anapokosea hatakiwe AGOMBEZWE.. inabidi aeleweshe aelewe na inapobidi ndo agombezwe na kuonywa....... Nafahamu mtu sehemu nakoishi (single lady) ameshafukuza wadada zaidi ya sita mwaka huu pekee... labda huyu anataka aletewe malaika.. and am sure hata malaika atamfukuza tu in few weeks.

Hawa tunawatengeneza tutakavyo. hatutegemei umtoe mtu kijijini aje afiti perfectly kwenye mazingira ya umjini kirahisi na kwa muda mfupi.. so uvumilivu, kuelekezana, kuzungumza ni muhimu sana.

Hongra kwa kuwajali. Barikiwa.

hii sasa kiboko........
Hiyo namba 4 ina maana hiyo cctv niifunge bila mr kujua? haya si yatakuwa majanga?
cc. Kaizer, The Boss, BAK, Eiyer, Mtambuzi, Tized ........
 

Watu wanadhani ma hausgel hawatakiwi kuwa na social life kama watu wengine
 
ha haaa, asante best.....
umejitahidi saaaanaaaaa kuni-counsel, lol!
Barikiwa pia
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…