Naombeni msaada wa ushauri nasaha

Naombeni msaada wa ushauri nasaha

na hakika wanasheria wana mbinu za kumsaidia.
Kupata mali kama ndoa ilikuwa ya miaka 12..


sina uhakika kwa hiyo nauliza.
kwa Tanzania mwanamke anaweza kumpa mume talaka???
ntashukuru kupata jibu Kiranga.

Kiswahili tunasema "mwanamke anaomba talaka yake" 🙂 Hawezi kumpa mwanamme talaka kwa sababu mwanamke hajaoa, kaolewa. Mfumodume.

Kisheria, wote wanaomba talaka.

http://tanzanet.org/downloads/laws/the_law_of_marriage_act_1971_(5_1971).pdf

(d) Separation and Divorce

Right to 99.

Subject to the provisions of sections 77, 100 and 101, any petition for separation or married person may petition the court for a decree of separation or divorce on the ground that his or her marriage has broken down,but no decree of divorce shall be granted unless the court is satisfied that the breakdown is irreparable.
 
Hawezi kwenda mahakamani tu na kusema nimekuja kufungua kesi ya madai ya talaka, so anachotakiwa kufanya ni either kwenda baraza la kata na kufungua kesi huko, kata wakishindwa watampa go ahead ya kwenda mahakamani au kanisani ambako nako wataendesha kesi za usuluhishi kanisa likishindwa sasa nao watampa baru ya kwenda mahakamani
 
thax dear,iyo board inaundwaje? tuanzie hapo...maana mume wake hamtaki ila ni mchaga anajikausha tu ili wasigawane mali wakati wamechuma wote kipindi wameoana hawakuwa hata na bodaboda

ndio zao,anajifanya anampenda mke kumbe anawaza mgao wa mali,ngoja na mm nipate mwongozo baba nanilii atanitambua!
 
Kwanza naomba mod usitoe uzi huu hapa
kuna dada alikuwa ameolewa amekaa na mume wake 12 years ndoa ya kikristo
hawakuwa na mtoto
mwaka 2010 mwanaume alimshutumu wife kutokuwa mwaminifu akamfukuza bila hata nguo,na kagoma kumrudisha hadi leo
walikuwa na vitu vingi nyumba maduka magari
mwanaume hataki kutoa talaka maybe anaona watagawana vitu ilasijui
sasa huyu dada anaomba ushauri afanyeje apate haki yake? ,maana nanateseka
mwanaume akiulizwa vipi anadai hana shida na mkewe bado anampenda ila sio kweli,hawaongei wala hajawai kumpa hata mia toka iyo jan 2010. Na huyo mwanaume hajaoa tena

.....mume hataki kutoa talaka na anadai hana shida na mkewe.

Vipi, nini msimamo wa mke?
Huenda ukanijibu (mume kamfukuza, hazungumzi nae nk)
Lakini kwenye baraza la wazee mke ndio ataonekana ameondoka, wkt mumewe bdo anamtaka.

Kwa msimamo wa huyo mume, mke yupo tayari kusuluhishwa na kurudiana na mumewe?
 
natamani kujua huyo dada alikuwa akijishughulisha na nini wakati akiishi na mumewe...
 
bibie.@Smile huyu mume anataka kumtesa tu mke wake hampendi huyo mke ushauri uliopo ni kuwa huyo Mwanamke aende Mahakamani kumshitaki mumewe ndipo atakapopata haki zake pasipo na njia hiyo hawezi kupata haki yake. Hakuna ndoa hapo wala hakuna mapenzi hapo.
 
Smile kuna hatua ana takiwa apitie ili aweze kupewa talaka, kwanza anatakiwa aende na madai yake kwenye baraza la usuluhishi wa ndoa na mume wake ataitwa kusuluhishwa mpaka waakikishe imeshindikana kusuluhisha ndio wana file devorce.
Kutoka nje ya ndoa inaweza ikawa sababu ya kupewa talaka lakini ushahidi utahitajika.
Kwa swala la mali kama walichuma wote watagawana na kama kuna mali mwanamke alizikuta pale kabla ya ndoa hizo zinabaki kuwa za mwanaume.
Mshauri aende kwanza mahakama ya mwanzo.

Lazima ziwepo sababu za kutosha za kuvunja hii ndoa!

Kwanza naomba mod usitoe uzi huu hapa
kuna dada alikuwa ameolewa amekaa na mume wake 12 years ndoa ya kikristo
hawakuwa na mtoto
mwaka 2010 mwanaume alimshutumu wife kutokuwa mwaminifu akamfukuza bila hata nguo,na kagoma kumrudisha hadi leo
walikuwa na vitu vingi nyumba maduka magari
mwanaume hataki kutoa talaka maybe anaona watagawana vitu ilasijui
sasa huyu dada anaomba ushauri afanyeje apate haki yake? ,maana nanateseka
mwanaume akiulizwa vipi anadai hana shida na mkewe bado anampenda ila sio kweli,hawaongei wala hajawai kumpa hata mia toka iyo jan 2010. Na huyo mwanaume hajaoa tena
 
Na akisema atumie njia ya kanisani itakuwa ngumu kupata talaka!
Wachungaji huwa hawkubali kuvunja ndoa kabisa.

Bora aende kwenye baraza la usuluhishi lakini nikiangalia hapa hii ndoa haiwezi kuvunjwa maana inaonekana hakuna sababu mathubuti na huyu mwanaume atakomaa ana mpenda na watazungushwa sana.
Smile kisheria talaka haitolewi kwa kuomba tu "nipe talaka yangu" kama ilivyo kwa baadhi ya desturi. Inabidi huyo dada aanze divorce proceedings kwa kuchukua hatua za mwanzo kabisa za baraza la upatanishi wa ndoa (Marriage Conciliation Board). Huko mwanaume ataitwa na wanabaraza watawapatanisha, kwa vile mume anasema bado anampenda mkewe watatakiwa kurudiana. Wasiporudiana au kuelewana basi baraza litatoa certificate kwa mwanamke kuonesha kuwa wameshindwa kuwapatanisha ni hivyo aliyepeleka shauri anaweza kwenda mahakamani ku-file for divorce (kanisani utaratibu huu huwa ni mgumu). Pia mwanaume akikataa kwenda kwenye baraza kusikilizwa baraza litatoa hati ya kushindwa kupatanisha kwa mlalamikiwa kutohudhuria vikao vya baraza.

Akipata hiyo hati ataenda mahakamani na kufungua shauri la kudai talaka. Katika maombi yake ya talaka atadai mgawanyo wa mali walizochuma na mumewe katika kipindi cha ndoa yao.

Hebu learned brother Rutashobolwa kuja huku msaidie Smile mawazo ya kisheria.
 
Last edited by a moderator:
Hizi ndoa jamn,kama kungekua na uwezekano wa kulegeza viapo wangelegezaga tuuu mana wanandoa wengi hawapo tayar kwa SHIDA...ila kwa RAHA wote wamo
 
Duh! Wamekaa kama mme na mke katika kipindi cha muongo mmoja na miaka miwili! Na hawajabahatika kupata mtoto! Na ukizingatia ni ndoa ya Kikrsto! Na katika maneno ya mwisho kabisa mbele ya kadamnasi yote ya kanisa waliambia hivi Ndoa iliyofungwa na MUNGU mwanadamu asitenganishe! ama kweli hapa sasa ni wale magwigi wa sheria ndiyo tunawahitaji hapa tumnusuru huyu rafiki yake Ndugu yetu Smile;

Copy;

PakaJimmy;
Mr Rocky;
Rutashubanyuma;
Mtumishi Wetu;
Dark City


Hawa member tajwa wanaweza wakampatia mwanga Ndg yetu Smile;

LiverpoolFC Muumba hapendi wanaharamu.jisomee Malachi 2: 15-17
 
thax dear,iyo board inaundwaje? tuanzie hapo...maana mume wake hamtaki ila ni mchaga anajikausha tu ili wasigawane mali wakati wamechuma wote kipindi wameoana hawakuwa hata na bodaboda

Hayo mabaraza ya usuluhishi yapo chini ya wizara ya ... na ustawi wa jamii ..... yapo kila mkoa/wilaya. Hivyo anaweza kuanzia hapo. Makanisa pia yana hayo mabaraza lakini huwa wagumu sana kutoa certificate ya kushindwa kusuluhisha.

Akisha anza huo utaratibu wa kisheria hakutakuwa na kujikausha wala nini! Hawezi kusema anampenda mke wake huku hataki kuishi nae!
 
Na akisema atumie njia ya kanisani itakuwa ngumu kupata talaka!
Wachungaji huwa hawkubali kuvunja ndoa kabisa.

Bora aende kwenye baraza la usuluhishi lakini nikiangalia hapa hii ndoa haiwezi kuvunjwa maana inaonekana hakuna sababu mathubuti na huyu mwanaume atakomaa ana mpenda na watazungushwa sana.

Ni kweli kama lengo ni talaka huwa ngumu sana kupitia kanisa.

Huyo mwanaume hawezi tu kusema anampenda mke wake wakati hataki kuishi nae. Wamekuwa katika separation kwa miaka 2, hawashiriki katika tendo la ndoa sasa atang'ang'aniaje kuwa anampenda? Inabidi huyo dada ajieleze vizuri kwanini anaona ndoa yao ni irreparably broken and thus warranting divorce.
 
kumbe Rutashubanyuma na mwaJ mnajua hii mambo ya sheria ntawatafuta soon.
 
natamani kujua huyo dada alikuwa akijishughulisha na nini wakati akiishi na mumewe...
wanas maduka alikuwa anauza duka lao kubwa tu yeye na mumewe
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom