2. KUKATAA KWA MAKUSUDI KUITIMILIZA NDOA:
Kama baada ya kufunga ndoa mmoja wa wafunga ndoa atakataa kuitimiliza ndoa anayekataliwa ana haki ya kuiomba mahakama kuvunja ndoa hiyo. Maingiliano yanayotambulika kisheria ni yale yanayofanyika siku ya ndoa na kuendelea na siyo kabla ya ndoa. Kukataa kuitimiliza ndoa kunakuwa sababu ya kubatilisha ndoa ikiwa mwenye kukataa hana sababu yoyote ya msingi na mwenye kukataliwa ametumia kila mbinu kumshawishi aliyekataa lakini ikashindikana kufanya tendo la ndoa.
SABABU YA KUTOA TALAKA MAHAKAMANI
Kabla ya kupeleka shauri au maombi mahakamani ya talaka, mwanandoa husika hana budi kufuata au kuzingatia hatua zifuatazo;
a) kufungua au kupeleka malalamiko kwenye
Baraza la Usuluhishi la Ndoa kwa mfano
Bakwata, kanisani,Utawi wa Jamii au
Baraza la Kata.
b) Baraza litasikiliza, na endapo litashindwa
mapatano au muafaka kati ya wanandoa hao,
21
basi baraza litatoa cheti ambacho kitaeleza kuwa limeshindwa kusuluhisha mgogoro wa ndoa na kuomba
mahakama kuendelea kutoa talaka.
c) Baada ya mwanadoa mmoja kupata cheti hicho basi atatakiwa atayarishe madai ya talaka akionyesha kuwa kulikuwa na ;-
ndoa halali,
kuna mgogoro kati yao,
watoto,
mali walizochuma wakati wa ndoa yao,.
Muombaji huyo ataiomba mahakama hiyo itoe amri ya
talaka,
mgawanyo wa mali zilizochumwa kwa nguvu za pamoja,mamlaka ya kukaa na watoto na matunzo yao,
gharama za madai / shauri.
Ili mahakama itoe talaka sababu kadha huangaliwa na mahakama. Sababu hizo ni mambo ambayo yatakayofanya ndoa ionekane kuwa imevunjika kiasi kwamba haiwezi kurekebishika tena, mambo hayo ni kama ifuatavyo;
a) Ugoni; hii ni zinaa ambayo hufanywa na mwanaume na mwanamke ambao hawajaoana.
Hii hutokea ambapo mwanaume ana mke wake au mwanamke ana mume wake, hivyo mmoja wapo anamwacha mke/mume na kufanya zinaa na mtu mwingine.
b) Ukatili; ukatili ni kuumiza nafsi nyingine, kuharibu mwili au kuwa na hofu ya kuumizwa.
c) Kulawiti; kulawiti ni kumwingilia mtu kinyume na maumbile,
d) Kichaa; ni kutokuwa na akili timamu, na hali hii lazima iwe imethibitishwa na madaktari bingwa wa akili.
e) Kuzembea wajibu kwa makusudi; haya ni majukumu ya mume, majukumu hayo ni kama haya; kumtunza mke kwa kumpa chakula, malazi na mavazi.
f) Uasi Ni hali ya mke au mume kuhama nyumba ya ndoa na kwenda kuishi mahala pengine bila sababu yoyote ya msingi,
g) Kutengana; kukaa mbalimbali kwa mume na mke kwa muda wa miaka isiyo pungua mitatu, kutengana kwao ni sababu tosha ya talaka.
HAKI NA WAJIBU KATIKA NDOA
Baada ya kufunga ndoa na ikaonekana haina kasoro yoyote, mke ana haki mbalimbali kisheria anazostahili kuzipata kisheria. Haki hizi ni kama;
- Matunzo; mke au wake wana haki ya kutunzwa na mume wao kwa kuwapatia mahitaji muhimu kama chakula, malazi, mavazi, matibabu, n.k kulingana na uwezo alionao mume.
- Kumiliki mali; mke ana haki ya kumiliki mali aliyoipata kabla na baada ya ndoa kama aliipata kwa
24
fedha yake mwenyewe. Mke ana haki ya kuingia mikataba, kushitaki na kushitakiwa. Makubaliano yaweza kufanywa na wanandoa hiyo jinsi ya kumiliki mali iliyopatikana kabla ya ndoa yao jinsi gani waimiliki. Kwa mali iliyopatikana wakati wa ndoa, mali hiyo ni mali ya wanandoa wote, kwa sababu imepatikana kwa mchango wa nguvu za pamoja. Hii haijalishi kuwa mmoja wa wanandoa (mke) hachangii pesa tasilimu au anakaa nyumbani na kufanya shughuli za nyumbani tu. Kufanya shughuli za nyumbani ni mchango mkubwa na ameokoa fedha nyingi. Umiliki wa mali kwa wanandoa haujalishi kuwa mmoja wapo amemiliki mali hiyo kwa jina lake au la. Sheria ya Ardhi inatamka wazi kuwa kama mwanandoa mmoja anamiliki mali kwa jina lake, na mwanandoa mwingine akachangia nguvu zake katika kuendeleza, kuboresha au kuzalisha mali hiyo basi anapata haki ya kumiliki mali hiyo.
- Haki ya kukopa kwa dhamana ya mume; jukumu la kutunza mke na watoto ni jukumu la mume au baba. Kwa msingi huo, endapo baba amesafiri, au ametoroka na baadaye matatizo yakajitokeza yanayohitaji fedha, basi mke ana haki ya kukopa fedha kwa jina la mume au kuweka rehani mali ya
25
mumewe.
- Haki ya kuishi katika nyumba ya Ndoa;
Nyumba ya ndoa ni nyumba ambayo mke na mume wanaishi wakati wa ndoa. Hata kama wanandoa wana nyumba nyingi, basi wanayoishi au kutumia kama makazi ndiyo nyumba ya wanandoa. Nyumba hii haiwezi kuuzwa, kuweka rehani au kuchukuliwa na mtu mwingine kama zawadi bila ya makubaliano ya wanandoa wote.(bila ridhaa ya wanandoa). Mwanandoa ana haki ya kuishi kwenye nyumba hiyo mpaka amri ya mahakama ya kuvunja ndoa, au kutengana itakapotolewa.
Hapa nimejaribu kuchukua baadhi ya vifungu kwenye sheria ya ndoa ya mwaka 1971, na vingi nilivyochukua ni vile vinavyoweza kumsaidia huyu mdada