Naombeni msaada kurudi bongo

Naombeni msaada kurudi bongo

Mkuu fanya hivi kusanya hela hadi ifike dola 6800 ambapo kwa miaka mitatu au minne itakuwa imefika. Hapo utakuwa na miaka 54 au 55 kisha kwenye dola 6800 sijui upo nchi gani tuseme dola 1800 nauli ya kurudi bongo kisha dola 5000 ambayo ni sawa a milion 12 ya kibongo nunua bajaji moko milioni 7 na boda 2 kila moja 2 million jumla milion 11. hiyo milioni moko panga chumba na sebule
laki moko miez 6 laki 6 nunua godoro jiko masufuria ndoo ndala. Kisha anza maisha. Kila boda 1 inakuletea buku 7 kwa siku au elfu 50 kwa wiki na ukiwa nazo 2 ni laki kwa wiki wiki 4 una laki 4. Hiyo bajaji unaweza ukampa mtu anakuletea elfu 15 hadi 20 kila siku ambayo ni laki hadi laki na 40 kwa wiki kwa mwez laki 4 hadi 6 na ukiendesha mwenyewe inazidi hiyo elfu 20 kwa siku au laki 6 kwa mwez. hapo ukijumlisha una laki 8 kwa kila mwezi kisha una make huku unaangalia upepo unaendaje uendelee na hiyo biashara au uwekeze sehem nyingine. Kila laheri
 
Sikati vitunguu wala maboxi. Naendesha mabasi ya mjini. Kama UDA ya zamani.
We rudi tu usitishwe na mtu, kwani maisha nipopote. Kabla ya kwenda huko naamini uliishi hapa, na ulienda kujaribu. Unaweza kuja kujaribu hapa tena ukatusua. Maisha yako hivyo na hayana bima. Life is how you make it.
Hao wanaokuambia uende kijijini, ni kijiji gani wanaishi free?! Gharama zitakuwepo na uta face life as is na utaanzia hapo na utaishi accordingly. Kwani sisi tunaishije, ni hivyo hivyo kwa kubaatisha na life inaenda.Kitu kibaya kwenye maisha ni kutaka kujiringanisha na watu wengine,au kushindana, na kujipa au kujivika status hewa. Kuwa wewe, anza kukimbiza life ni hihi dunia nzima. Hizi story za $1800 haitoshi kwani hiyo ndiyo utategemea for the rest of your life?! Utafika utaanzia hiyo, ndiyo itaisha na muda huo utakuwa umejua ABC za street. Hakuna kuogopa. Naona wachina wanakuja empty handed wanatuuzia sambusa buguruni lakini wanaishi. Rudi tu usiogope vitisho vya mtu. Mbona huko unaishi?! Haitakuwa the same lakini utaishi kama wengine, hii Bongo.
 
Habari wana jf.
Mimi ni mbongo ambaye nipo ughaibuni tangu 1992 na sijawahi kurudi bongo. Nilikuja huku kutafuta maisha na kusoma, lakini kutokana na gharama za maisha na gharama za elimu sikuweza kusoma. Sasa nina miaka 51 na natamani kurudi bongo. Elimu yangu ni ya form 4 ya pugu secondari 1988. Benki nina dola 1800 tuu. Jee naweza kurudi bongo na kuishi comfortably? Yaani kunywa maziwa, kulala pazuri, kutotumia madaradara kwa usafiri, kula chakula nzuri (siyo kula nafaka).
Kuna fursa gani huko kwa wazee kama mimi?
Naombeni msaada wenu
Kama umekaa miaka yote hiyo na unaandika kiswahili fasaha kiasi hiki ukija hutakosa, cha kufanya, kama vipi njoo 2020, tutakuwa na uhaba wa wabunge.
 
Watoto wako,wako in position kukusaidia?
Hahaha samahani huu sio ushauri mzuri, kutegemea watoto. Mpe ushauri wa yeye kusimama kivyake, kuwategemezi wa mtu sio ushauri.
Yaani wewe mtu akushauri, eti nenda kwa baba mdogo wako, au kwa shangazi yako?! Mpe namna ya ku survive like we all do. Maisha hayana hero, tunakimbia kimbia tu mwisho we all end the same place best.
 
Habari wana jf.
Mimi ni mbongo ambaye nipo ughaibuni tangu 1992 na sijawahi kurudi bongo. Nilikuja huku kutafuta maisha na kusoma, lakini kutokana na gharama za maisha na gharama za elimu sikuweza kusoma. Sasa nina miaka 51 na natamani kurudi bongo. Elimu yangu ni ya form 4 ya pugu secondari 1988. Benki nina dola 1800 tuu. Jee naweza kurudi bongo na kuishi comfortably? Yaani kunywa maziwa, kulala pazuri, kutotumia madaradara kwa usafiri, kula chakula nzuri (siyo kula nafaka).
Kuna fursa gani huko kwa wazee kama mimi?
Naombeni msaada wenu

You can’t be serious!! Yaani kwa dola 1800 unaandika utumbo huu with 51 years? Pathetic fool !!!
 
Habari wana jf.
Mimi ni mbongo ambaye nipo ughaibuni tangu 1992 na sijawahi kurudi bongo. Nilikuja huku kutafuta maisha na kusoma, lakini kutokana na gharama za maisha na gharama za elimu sikuweza kusoma. Sasa nina miaka 51 na natamani kurudi bongo. Elimu yangu ni ya form 4 ya pugu secondari 1988. Benki nina dola 1800 tuu. Jee naweza kurudi bongo na kuishi comfortably? Yaani kunywa maziwa, kulala pazuri, kutotumia madaradara kwa usafiri, kula chakula nzuri (siyo kula nafaka).
Kuna fursa gani huko kwa wazee kama mimi?
Naombeni msaada wenu
1usd=2300Tsh
1800Usd=4.41 Million
Bora ukae hko hko ukija hku utafikia Kaburini maana Maisha yapo tight. Pia kama toka mwaka 1992 umemake dolla 1800. Huku hupawez inaonekana ww n mtu wa Bata sana na Totoz. Lakn kama una mirad yako hku utaishi maisha mazur sana.
 
Hahaha samahani huu sio ushauri mzuri, kutegemea watoto. Mpe ushauri wa yeye kusimama kivyake, kuwategemezi wa mtu sio ushauri.
Yaani wewe mtu akushauri, eti nenda kwa baba mdogo wako, au kwa shangazi yako?! Mpe namna ya ku survive like we all do. Maisha hayana hero, tunakimbia kimbia tu mwisho we all end the same place best.

Best nimependa ushauri wako,mie namshauri km bado anao marafiki afikie kwa mmojawao,hio hela yote aweke kwenye biashara,ajiwekee muda let’s say miezi sita kuona km biashara itamfanya asurvive,mbivu na mbichi atajua baada ya miezi sita,akiona baada ya Miezi Sita hawezi Kukaa Tanzania then arudi alikokuwa.
 
Hata 51 sio mbaya... kama alijitunza vizuri na akanusurika na maradhi, 51 mtu anakuwa na nguvu za kutosha!

Mkuu Anithape, aidha sasa or never manake, kama akiba yenyewe ndo hiyo, ina maana unakuja bila pesa ya kuanzia na kwa maana nyingine mtaji wako ni nguvu na akili zako! Kwa umri ulionao sina shaka bado una nguvu za kutoka na akili inachemka na kwahiyo unaweza kufanya jambo!
Hii ndio comment bora sana kwangu. Hakika 51 sio umri mkubwa sana, brother yangu alirudi na 48 hakuwa na mke wala mtoto, wala nyumba wala chochote, makaratasi yake ya Hadi Master alipoteza, amefight yuko vizuri sasa, ameoa, amejenga na ana watoto watatu sasa maisha yanasonga.
 
Huu uzi unanikumbusha dogo mmoja 25 yrs analilia kukaa nyumbani..Ishu ni kuwa na malengo yaan with that $1800 hata mwezi hautaisha utakumbuka maisha ya huko.
 
Back
Top Bottom