Naomba ushauri wenu

Naomba ushauri wenu

andazi

Member
Joined
Jun 7, 2025
Posts
47
Reaction score
209
Nahitaji ushauri wa watu wenu ndugu zangu wenye busara.

Ninaishi Canada kwenye nyumba ya serikali (HLM) pamoja na mke wangu na watoto wangu wawili. Baba yangu ana miaka 46. Nilimchukua aishi kwangu kwa sababu alikuwa ana maisha magumu, lakini tangu ameingia kwangu maisha yamekuwa magumu sana.

Tabia zake zimekuwa changamoto kubwa:

Ni muongo kupita kiasi, hasemagi ukweli hata nikimwomba nimsaidie kupata kazi.
Ni mvivu wa kazi, hajawahi kuendelea na kazi yoyote. Wiki 3 sasa hana kazi wala kipato.
Anadanganya kuwa anaenda kazini kumbe anazurura tu mitaani.
Ni mlalamikaji, mbishi, na anakasirika haraka.
Ni mbeya na ana historia ya kuleta migogoro ndani ya familia. Kwasababu ya uongo wake
ALimkataa mama yangu 2017 tena kwa talaka cha ajabu yeye ndo anateseka zaidi na wakati aliaminisha jamii kuwa mama yangu ndo mbaya
Ana tabia ya kutumia watu, akishapata mahali pa kula na kulala, anajisahau kabisa.
Anapenda kula sana, na gharama za chakula zimepanda sana. Zamani nilikuwa natumia $200–$300 kwa mwezi, sasa tunatumia $700+.
Hatoi chochote kwenye matumizi, mimi ndiye nabeba kila kitu.

Kwenye nyumba ya serikali (HLM) siruhusiwi kuishi na mtu mwingine yeyote ambaye hajatajwa kwenye mkataba. Hii inaniweka kwenye hatari ya kufukuzwa na kupoteza makazi yangu pamoja na familia yangu.

Ukweli mwingine mgumu ni kwamba baba yangu amezoea kufukuzwa kila mahali anapokwenda kwa sababu ya tabia zake. Akiachiwa aishi kwa watu, harudi tena kwao mpaka apate shida. Baridi ikianza ndipo anarudi kuomba msaada.

Nimejaribu kila njia za kumwonya, kumueleza, kumsaidia, kumuelekeza, lakini haelewi kabisa. Kila siku ni uongo, visingizio, lawama na kuonyesha ubabe. Ukimwambia jambo analalamika au kuchukia.

Sasa nimefika mwisho nataka kumfukuza ila kuna wakati huruma unanijaa moyoni tu

Ila Nina hofu kwa watoto wangu, mke wangu, ikiwa tutapoteza nyumba yetu kwa kuvunjiwa mkataba na serekali sisi ndo tutaangaika zaidi . Lakini pia ninajua huyu ni baba yangu mzazi, na akitoka kwangu atakuwa hana pa kwenda

Swali

Nifanye nini katika hali kama hii?
Nimfukuze kwangu kwa ajili ya usalama wa familia yangu, au niendelea kumvumilia huku familia yangu ikiteseka?

Naomba ushauri wenu
 
Ikiwa Ulishajaribu: Kumwambia, Kumweka karibu na Kumshauri bila kumdhalilisha mbele za watu/ familia yako.
Na bado: ni muongo, mbishi n.k
, basi mtafutie malazi(shelters) yaani sehemu za msaada wa wahamiaji / wanaume wasio na makazi/ nyumba za wazee. Baada ya kumpeleka mpatie kwa kiasi kidogo cha pesa ya kwanza ya kujikimu.

Unaweza kumwambia kwamba sababu ya yeye kuhitajika kutoka hapo ni kwamba "sheria ya HLM hairuhusu mtu ambaye hajatajwa kwenye mkataba wa kupangisha nyumba hii, kuendelea kuishi hapo zaidi ya siku kadhaa... "

Ila bado unajukumu kubwa la kumnasihi kwa hekima, muwe wawili tu na kuona kama atajirudi, kumfukuza BABA ni hatua nzito sana.
 
Wacha uzwazwa, uli mchukua mzee ili apate pumziko sio kukusaidia kulipa bill.
Tatizo naishi kwenye nyumba ya serekali na wakijua anaishi hapa nitakuwa nimepoteza nyumba yangu ya kwasababu mkataba utavunjwa kwa kutoheshimu mkataba pili hajishauriagi yeye ni uongo tu ata nikimwambia mambo ya kujenga maisha yake anakuona kama adui yake vile
 
Ikiwa Ulishajaribu: Kumwambia, Kumweka karibu na Kumshauri bila kumdhalilisha mbele za watu/ familia yako.
Na bado: ni muongo, mbishi n.k
, basi mtafutie malazi(shelters) yaani sehemu za msaada wa wahamiaji / wanaume wasio na makazi/ nyumba za wazee. Baada ya kumpeleka mpatie kwa kiasi kidogo cha pesa ya kwanza ya kujikimu.

Unaweza kumwambia kwamba sababu ya yeye kuhitajika kutoka hapo ni kwamba "sheria ya HLM hairuhusu mtu ambaye hajatajwa kwenye mkataba wa kupangisha nyumba hii, kuendelea kuishi hapo zaidi ya siku kadhaa... "

Ila bado unajukumu kubwa la kumnasihi kwa hekima, muwe wawili tu na kuona kama atajirudi, kumfukuza BABA ni hatua nzito sana.
Ndugu yangu yeye sio criminal hapana uku canada ukiwa criminal ndo.utakuwa umepoteza maisha yake alipoteza vyeti vyake kama green card na kadi zingine nimejaribu kumshauria lakini wapi na hii sio mara yake ya kwanza anaishi ivi toka 2022 anafanyaga ukimpa tu nafasi ya kulala anasau shida zake zote ana kwasababu ana nafasi ya kulala 😪😪 ni mambo mengi ya aibu ambayo siwezi kuweka hapa
 
Ni mtu mzima mwenye upeo mdogo! Kama kweli ni Baba yako mzazi pamoja na yoote mengine ilifaa kuyabakisha kwa staha ya mzazi. eti anakula sana je wazijua tabu zako ulizo mpatia ukiwa mtoto na yeye angepata wasaa wa kuzielezea?! Behave
 
Tatizo naishi kwenye nyumba ya serekali na wakijua anaishi hapa nitakuwa nimepoteza nyumba yangu ya kwasababu mkataba utavunjwa kwa kutoheshimu mkataba pili hajishauriagi yeye ni uongo tu ata nikimwambia mambo ya kujenga maisha yake anakuona kama adui yake vile
Kama ulijua sheria si rafiki, why uhangaike kumleta huko?.

UKisema mzee means ako 50-60+, Sasa ana jenganje huko mbele?.

wewe sema uli taka bill assistance, na mzee nae kaona isiwe tabu wacha ageuke nyoka pori😁
 
Tatizo naishi kwenye nyumba ya serekali na wakijua anaishi hapa nitakuwa nimepoteza nyumba yangu ya kwasababu mkataba utavunjwa kwa kutoheshimu mkataba pili hajishauriagi yeye ni uongo tu ata nikimwambia mambo ya kujenga maisha yake anakuona kama adui yake vile
Hili la hofu ya kufukuzwa kwenye nyumba is an afterthought and a pretext ya kumfukuza baba yako. Ulipoamua kumleta uishi naye ulikuwa kwenye nyumba hiyo hiyo. What changed?

Umemuelezea baba yako kwa namna ambayo inatweza utu wake na nafasi yake kama baba. Nashindwa hata nianzie wapi kukushauri.
 
Mpeleke akaombe nyumba yake ya serikali, na kwa umri wake ana weza kupata pesa ya kula toka serikalini.
 
Bila shaka ww ni mchaga
kwel mshua anazingua pakubwa sana ila kumsema et anakula sana wala sio unyama
kumbuka kakulea tang ukiwa 0 year mpk sasa una familia na unaish mambele
unajua ulipokua mdg ulikua na tabia gn ambazo hajawah kukwambia?
tafuta alternative ambayo haitomfanya ahisi unamtenga
 
Kama ulijua sheria si rafiki, why uhangaike kumleta huko?.

UKisema mzee means ako 50-60+, Sasa ana jenganje huko mbele?.

wewe sema uli taka bill assistance, na mzee nae kaona isiwe tabu wacha ageuke nyoka pori😁
Nilimchukuwa kwa nia ya kumsaidia ila dah ni vigumu mno tena sana nilitaka aje ni mtafutie kazi kwasababu nilikuwa tayari nina connexion ya kazi na baada ya hapo ni mtafutie nyumba ila mipango yote hii imekwamishwa kwasababu ya kutokuelewa kwake tu
Hili la hofu ya kufukuzwa kwenye nyumba is an afterthought and a pretext ya kumfukuza baba yako. Ulipoamua kumleta uishi naye ulikuwa kwenye nyumba hiyo hiyo. What changed?

Umemuelezea baba yako kwa namna ambayo inatweza utu wake na nafasi yake kama baba. Nashindwa hata nianzie wapi kukushauri.
Nilikuwa naishi hapa mambo yalikuwa ivi kikawaida yeye anafanyaga kikiwa kipindi cha baridi ndo anatafutaga sehemu ya kukaa na sehemu zote ambazo alikuwa anakaa kote alifukuzwa kwasababu ya tabia yake ya uongo tu sasa kipindi iki nikamwambia mke wangu kuwa tumkaribishe baba hapa kwasababu ili nipate kumsaidia kupata kazi na sehemu ya kulala mke wangu akubali kumpokea baba nyumbani lengo langu lilikuwa akija tu nimtafutie kazi na akiwa na kazi ni mtafutie chumba cha mda miezi 6 kuendelea ila cha hajabu sasa mtu ambaye nilimpokea ili nije kumsaidia hasaidiki hata kidogo kwanza alikuwa hana document yeyote nimejaribu kumbembeleza vipi alete document ili ni msaidie kumpata kazi ana nidanganya kuwa ana kazi na kila siku anaendaga uko ambako anaitaka kazini kwake ila ukweli ni kwamba ana shinda ndani ya station za bus tu na yote haya anafanya kwasababu moja ya tatizo lake ni kukubali kuwa ameshindwa asaidie au kukubali kuwa hana
APatiwe atakudanganya mpaka utachoka
 
Mrudishe Malawi aje kuongeza nguvu tuwatoe waimla kwenye kiti.
 
Nahitaji ushauri wa watu wenu ndugu zangu wenye busara.

Ninaishi Canada kwenye nyumba ya serikali (HLM) pamoja na mke wangu na watoto wangu wawili. Baba yangu ana miaka 46. Nilimchukua aishi kwangu kwa sababu alikuwa ana maisha magumu, lakini tangu ameingia kwangu maisha yamekuwa magumu sana.

Tabia zake zimekuwa changamoto kubwa:

Ni muongo kupita kiasi, hasemagi ukweli hata nikimwomba nimsaidie kupata kazi.
Ni mvivu wa kazi, hajawahi kuendelea na kazi yoyote. Wiki 3 sasa hana kazi wala kipato.
Anadanganya kuwa anaenda kazini kumbe anazurura tu mitaani.
Ni mlalamikaji, mbishi, na anakasirika haraka.
Ni mbeya na ana historia ya kuleta migogoro ndani ya familia. Kwasababu ya uongo wake
ALimkataa mama yangu 2017 tena kwa talaka cha ajabu yeye ndo anateseka zaidi na wakati aliaminisha jamii kuwa mama yangu ndo mbaya
Ana tabia ya kutumia watu, akishapata mahali pa kula na kulala, anajisahau kabisa.
Anapenda kula sana, na gharama za chakula zimepanda sana. Zamani nilikuwa natumia $200–$300 kwa mwezi, sasa tunatumia $700+.
Hatoi chochote kwenye matumizi, mimi ndiye nabeba kila kitu.

Kwenye nyumba ya serikali (HLM) siruhusiwi kuishi na mtu mwingine yeyote ambaye hajatajwa kwenye mkataba. Hii inaniweka kwenye hatari ya kufukuzwa na kupoteza makazi yangu pamoja na familia yangu.

Ukweli mwingine mgumu ni kwamba baba yangu amezoea kufukuzwa kila mahali anapokwenda kwa sababu ya tabia zake. Akiachiwa aishi kwa watu, harudi tena kwao mpaka apate shida. Baridi ikianza ndipo anarudi kuomba msaada.

Nimejaribu kila njia za kumwonya, kumueleza, kumsaidia, kumuelekeza, lakini haelewi kabisa. Kila siku ni uongo, visingizio, lawama na kuonyesha ubabe. Ukimwambia jambo analalamika au kuchukia.

Sasa nimefika mwisho nataka kumfukuza ila kuna wakati huruma unanijaa moyoni tu

Ila Nina hofu kwa watoto wangu, mke wangu, ikiwa tutapoteza nyumba yetu kwa kuvunjiwa mkataba na serekali sisi ndo tutaangaika zaidi . Lakini pia ninajua huyu ni baba yangu mzazi, na akitoka kwangu atakuwa hana pa kwenda

Swali

Nifanye nini katika hali kama hii?
Nimfukuze kwangu kwa ajili ya usalama wa familia yangu, au niendelea kumvumilia huku familia yangu ikiteseka?

Naomba ushauri wenu
WEwe ni andazi unajitengenezea chai
 
Back
Top Bottom