Naomba ushauri wako kuhusu wembamba nilionao

Naomba ushauri wako kuhusu wembamba nilionao

Dangerm

Member
Joined
Aug 11, 2014
Posts
87
Reaction score
9
Nawasalimu Wote

Mimi Ni Kijana Mwenye Umri Wa Miaka 20, Kiumbo Mimi Ni Mwembamba Sana Mpaka Nashindwa Kabisa kuanzisha Uhusiano Wa Kimapenzi Na Mwanamke.

Sometimes Nikikaa Na Vijana Wenzangu Wananicheka Sana Kuhusu Umbo Langu La Mwili, mara Wananiambia Hivi("We Jamaa Ni Sindano Sana".

"We Jamaa Ukipata Demu Hata Bao Moja Hufikishi".

"We Jamaa Ni Mlenda Sana".

"Hivi Una Demu Kweli?"
Yaani nakuwa Confused Sana Kisaikolojia mpaka Nashindwa Kujiamini Ninavyokuwa Mbele Ya Kundi La Watu.

Naomba Ushauri Wenu Nifanyeje Ili Watu Waweze Kunitambua Kwamba Na Mimi Ni mtu mbele ya watu?
 
Hakuna mtu ambae anaweza kukutambua kabla ya wewe hujajitambua

Tatizo ulilonalo linawakabili wengi sana,watu tunadhani heshima na ubinadamu wetu unaongezwa au kukamilishwa na watu wengine,yaani unakuta mtu bila ya kusifiwa hajaona kama yeye ni mtu au binadamu,matatizo haya yanaletwa na malezi yetu

Kabla ya watu kukubali jikubali kwanza wewe mwenyewe,kumbuka ukiwa mwembamba au mnene au uwe na umbo lolote lile bado watakusema tu,usidhani kuwa kuna aina ya umbo ambalo ni "zuri" kama unavyofikiria,Mungu amekuumba kamili na huhitaji mtu mwingine akuongezee sifa yoyote ile ili uwe kamili kwani tayari wewe ni kamili

Anza kujiamini kuanzia leo na kataa mawazo dhaifu ya kujiona hujakamilika kuanzia leo,jipende kwanza kabla ya watu wengine hawajakupenda kwani ukiweza kujipenda hata dunia nzima ikuchukie bado utabaki unajiamini na utajiona wewe ni binadamu kamili

Achana na mawazo ya rafiki zako,wewe waone kama wanatania tu wakati wanakuambia hivyo na usizingatie kabisa maneno yao!
 
Naomba Ushaur Wenu Nifanyeje Ili Watu Waweze Kunitambua Kwamba Na Mimi Ni "MTU MBELE YA WATU?"

Anza kufanya mazoezi ya kujenga mwili. Unaweza ukayafanya nyumbani lakini ukitafuta gym itakuwa ni bora zaidi.

Sambamba na mazoezi hayo anza kula kwa wingi sana vyakula vyenye viwango vikubwa vya protini kama nyama ya ng'ombe, egg whites (sijui Kiswahili chake), samaki, kuku, na kadhalika.

Pia, kama huko uliko unaweza kupata weight gainer (protein supplement) basi anza kutumia pia.

Ili uweze kuona matokeo yanayoridhisha itabidi ukomae kwelikweli na hayo mazoezi pamoja na kula chakula cha kutosha.

Kama una calorie counter basi anza kuweka kumbukumbu ya calories unazokula kila siku na jaribu (kama hali yako inaruhusu) kuingiza mwilini calories nyingi zaidi ya zile unazozitoa kwa sababu ili ujenge mwili itakubidi uwe na akiba ya calories mwilini.

Kwa dondoo zaidi waweza kunicheki PM.
 
Nawasalimu Wote,,!
Mimi Ni Kijana Mwenye Umri Wa Miaka 20, Kiumbo Mm Ni Mwembamba Sana
Mpaka Nashindwa Kabisa KUANZISHA Uhusiano Wa Kimapenz Na Mwanamke,,
Sometimes Nikikaa Na Vijana Wenzangu Wananicheka Sana Kuhusu Umbo Langu
La Mwili,,mara Wananiambia Hivi...("We Jamaa Ni Sindano Sana",, "we
Jamaa Ukipata Demu Hata Bao Moja Hufikish",,,,"we Jamaa Ni Mlenda
Sana",,,,"hivi Una Demu Kweli?",,,,,,..)
Yaan Nakuwa Comfused Sana Kisaikolojia Mpaka Nashindwa Kujiamini
Ninavyokuwa Mbele Ya Kundi La Watu,..

Naomba Ushaur Wenu Nifanyeje Ili Watu Waweze Kunitambua Kwamba Na Mimi
Ni "MTU MBELE YA WATU?"

utanenepa we bado mdogo si ndo umetoka jkt? we si 4m 6 leaver? ukienda chuo boom litakunenesha dogo
 
Jiamin tu, mbona kawaida tu, hlf unaweza ukawa na mwil mkubwa hlf kitandan ukawa zero, me binafs n mwembamba ila mziki wng anaujua Shem wk, confidence ndo ki2 cha mcng kuliko vyote
 
Jiamin tu, mbona kawaida tu, hlf unaweza ukawa na mwil mkubwa hlf kitandan ukawa zero, me binafs n mwembamba ila mziki wng anaujua Shem wk, confidence ndo ki2 cha mcng kuliko vyote

Ila tusemage tu na ukweli mwanaume aliejaajaa hua anavutia kichiziii
Jitahidini hata vifua muwe navyo vipana sasa mwanaume anakua na kifua cha panzi ndio nini sasa
 
una maanisha ww ni mwembamba kama betina??????? au Pres. Kagame? au chini ya hao wawili?
nifup au mrefu?

maana yangu kama ni mfupi then wembamba wanahaki ya kukutania na ndio maana ww hujiamin.

ila kama ni mrefu na mwembamba wanakuoneaa donge wakudhoofishe na ww umekubali
 
Ila tusemage tu na ukweli mwanaume aliejaajaa hua anavutia kichiziii
Jitahidini hata vifua muwe navyo vipana sasa mwanaume anakua na kifua cha panzi ndio nini sasa

Dina mwenzio ana stress apo za wembamba nawe wazidi kumtia joto sio vizuri shosti......
 
Jaribu kula vyakula vya protein kwa wingi kama walivoshauri wengine, na kama ndo huaga unakula na hali bado haibadiliki basi weye rizika tu!!
 
Ila tusemage tu na ukweli mwanaume aliejaajaa hua anavutia kichiziii
Jitahidini hata vifua muwe navyo vipana sasa mwanaume anakua na kifua cha panzi ndio nini sasa

Unachosema kwel lkn wengne ndo nature ya miili yao pia wengne wana matatizo ya kiafya xo hawawez kujaa big shoo
 
Dina mwenzio ana stress apo za wembamba nawe wazidi kumtia joto sio vizuri shosti......

Nilisahauuuu abebe chuma pia ale vizurii amuige daimond si alikua chembamba haswaaaa
 
Tyta hebu weka picha ya wembamba tuone
 
Last edited by a moderator:
kaa hivyo hivyo wala usijibadilishe, wembamba ndiyo deal siku hizi. .....hao wanaokucheka watakuwa na mavitambi yao so wanajifariji tu. wembamba wa reli na gari moshi linapita. tena ukiwa mwembamba ndo dushee linakuwa na size ya kutosha, ukiongeza kitambi tu na dushee itasinyaa...tupo wanawake wengi tunapenda wanaume wembamba kwanza hawajambi jambi ovyo....
 
Back
Top Bottom