Kuwa msomaji mzuri wa vitabu na makala zenye tija.
Kwakuwa umesema upo chouni, hakikisha kwenye presentations mnazopaswa kufanya kama kundi, wewe unapata nafasi ya kuwasilisha mada pale mbele.
Ukiwa darasani pia, changia ama uliza maswali. Ila usifanye ili tu upate uwezo huo, hakikisha unachouliza kina tija, uliza kwa ustaarabu na angalia na nature ya walimu wako pia.
Shiriki katika mijadala na makongamano yanayofanyika hapo chuoni kwenu. Katika mijadala hiyo, soma juu ya mada husika, kisha omba nafasi ya kuchangia ama kuuliza swali nk
Jiunge na umoja wa wanafunzi uliopo hapo shuleni, mfano AISEC, UNA, nk. Ukiwa humo shiriki kikamilifu katika kuandaa na kutekeleza shughuli mbalimbali
Anzisha jukwaa lenye kujikita katika maswala yatakayokupa fursa ya kuwasilisha mawazo yako. Mfano, labda klabu ya kusoma vitabu chuoni kisha mnakuwa na siku moja katika mwezi mnakutana na kuwasilisha muhtasari wa vitabu mlivyosima.
Andika makala na share kwa wadau kwa njia mbalimbali. Hii haitakupa "platform" ya kuzungumza ila itakusaidia katika kufikiri kwa haraka, kupanga hoja na kuweza kujibu hoja. Hivi vitakusaidia kwenye "public speaking" unayoitarajia.
Share na jamii juu ya maswala mabalimbali ambayo unayafahamu kutokana na elimu na uziefu wako. Mathalani kama unasoma saikoloji angalia mada gani nzuri inayohusu labda namna bora ya kusoma na kukumbuka mambo. Kisha unawatafuta wenzako kadhaa mnajiandaa na kuomba nafasi katika shule mbalimbali ili kuwasaidia vijana kwenye kipengele hicho na vingine vingi.
Tuishie hapo kwa sasa
Naomba kuwasilisha