Naomba Ushauri, Mpangaji wangu 'kaniblock'

Naomba Ushauri, Mpangaji wangu 'kaniblock'

Pole sana mkuu. Mimi wapangaji wangu wakizingua tu kulipa kodi nampa notice ya siku saba awe tayari amenikabidhi funguo za nyumba, na pia nyumba aiache ikiwa na hali ya usafi kama siku anaingia.

Pili bill ya maji ni shared kwa kila apartment block, hivyo ikitokea mpangaji anazingua tu kulipa bill ya maji na yeye notice inamhusu kwa sababu siwezi sababisha usumbufu kwa wapangaji wengine kwa ajili ya mzembe mmoja.

Kwa wapangaji huwa sitaki mzahaa na FEDHA yangu
Kuna mpangaji wangu mmoja nadeal nae sahivi anazingua sanaa, sahivi hapokei simu na anadai yuko kenya, kodi imeisha mwezi sasa, chumba kafunga halafu ni sehem wapangaji kupatikana ni siku 1 tu!! Daah inataka umakini sana (sio mihemko) kudeal na hawa wajinga hasa mjini, ndo nimeanza kwa mjumbe twende serikali za mtaa kupata notisi formal.
Unaushauri gani mkuu?
 
Notice ya pango ni miezi mitatu (3) tu yaani mpangaji kukaa bure akijiandaa kuhama, kwa hiyo huyo tayari keshajipa notice.

Akirudi mburuze kwa mwenyekiti S/M kudai haki yako aliyokaa ziada ya miezi mitatu ya notice na kumtaka ahame bila wewe kutoa visingizio.

Hapo kubali hasara ndogo kuliko kuendelea kufuga hicho kirusi.

Mpangaji yeyote mwenye mkwamo, hufunguka mwenyewe mapema kwa mwenye nyumba akiwa tayari kapiga hesabu zake ni mwezi gani atakuwa tayari kulipa na ukifika mwezi huo lazima alipe na siyo kusongesha blah blah zake tena.

Wapangaji aina hiyo siyo wazuri, umesoma kwenye mitandao issue ya Kawe, hadi Mbunge Gwajima kulivalia njuga?

Nyumba ya mamillioni imeuzwa na mpangaji, kisa kilo 38 za nyama na mwenye nyumba kubaki analalamika asijue aanzie wapi.

Baadaye akiisha kukuzoea sawasawa, mtaingia naye kwenye migogoro ya kupotezeana muda mahakamani na ukimhurumia lazima itakula kwako tu, mimi nina uzoefu sana na mambo hayo, kubali hasara hiyo ya kodi ya miezi mitatu kisha fukuza.
Kuna mpangaji wangu m1 naona analeta mambo sielewi nae naanza kudeal nae taratibu bila mihemko! Kuna watu hawajielewi kabisa. Na ukiangalia kiuhalisia ni bora hasara ndogo kuliko kumfanyia fujo ikawa majuto baadae.
 
Kuna mpangaji wangu m1 naona analeta mambo sielewi nae naanza kudeal nae taratibu bila mihemko! Kuna watu hawajielewi kabisa. Na ukiangalia kiuhalisia ni bora hasara ndogo kuliko kumfanyia fujo ikawa majuto baadae.
Ukiona mpangaji analeta mazoea, piga notice ya kisiasa...'wanangu wa mkoani wanakuja, tafuta chumba bwashee'... huku tabasamu limekujaa usoni kwa kuua nyani!
Mtu asikuletee ujinga ujinga kwenye maisha yako.
 
Ukiona mpangaji analeta mazoea, piga notice ya kisiasa...'wanangu wa mkoani wanakuja, tafuta chumba bwashee'... huku tabasamu limekujaa usoni kwa kuua nyani!
Mtu asikuletee ujinga ujinga kwenye maisha yako.
Huyu wangu kodi imeisha mwezi sasa, anadai yupo kenya, kulipa anapiga uongo mwingi, namwambia niachie chumba hajibu na ubaya kafunga na haonekani na sasa hivi hapokei na simu. Ubaya zaidi sina siku mingi natoka nchini na anajua huwa sipo muda mwingi babeki. Daaah ananiumiza kichwa ndo nimeanza process ya notisi serikali za mtaa. Lakin naona kabisa dalili za mtu kukaa bure halafu ni sinza nyumba mpya, wahitaji ni wengi saaana
 
Back
Top Bottom