Naomba ushauri kuhusu mpenzi niliye naye

Da tall gal

Member
Oct 29, 2016
11
9
Mimi ni msichana wa miaka 20 nipo Chuo Kikuu mwaka wa kwanza lakini nilitokea kuanzisha mhusiano na Mwanaume nikiwa form three. Nampenda na nimekuwa mwaminifu kwake toka nilivyoanzisha mahusiano naye.

Lakini yeye alikuwa mbele yangu kimasomo na alivyomaliza kidato cha nne hakufanikiwa kujiunga na kidato cha tano hivyo akaamua kurudia mtihani mara ya pili. Mimi nilivyomaliza kidato cha nne nilifanikiwa kujiunga na kidato cha tano hivyo nikawa nimemwacha hatua kadhaa nyuma.

Matokeo yake yalivyotoka akawa amefeli tena kwa mara ya pili lakinihakukata tamaa akarudia mtihani kwa mara ya tatu. Sasa mimi nipo Mwaka wa kwanza na yeye anasubiri matokeo ya kidato cha nne.

TATIZO NI KWAMBA NIKIMUULIZA MAISHA YETU YA MBELENI HATAKI TUZUNGUMZIE HILO na ninaona kuwa tayari kila mtu anahitji kutimiza malengo yake na mimi nataka nikimaliza chuo niolewe ila atakuwa bado anasoma.

NAOMBENI USHAURI WENU NIFANYEJE?
 
Sema ukweli kwamba ushampata mwingine huko chuo yaan hapa hata bado test hazijachanganya vizur ushaanza kuwaza ndoa,wewe binti kuwa makini utachezewa sana na kuachwa maana unaweka wazi unataka ndoa.

Soma, ndoa itakuja tu either kwa huyo jamaa au kwa mwingine. Supplementary na carry sio za mchezo mchezo hasa ukiziletea stress za mapenzi
 
Kama kweli unampenda kwa dhati nakuomba kwanza umshauri ili apunguze mawazo, pia kufeli mtihani siyo ndio kufeli maisha.
Ipo mifano mingi hapa Tanzania, kuna watu hawana kitabu kichwani ila kimaisha wako vizuri sana. Kaa pamoja ili myajenge, fikiri kitabu maana chuoni kuna kitu tunaita discontinues maana unaweza pata mpenzi mpya akakuharibia future yako ya maisha kabisa.
 
Kila Kitu mungu alisha qadiria ,liwe jema au baya ,Na pia unapoomba basi inawezekana kukuepushia kama ni baya na kama ni zuri pia akakuletea,.
Mume/mke wa kuishi naye mungu ndo anajua ,Kubwa kukaa chini na kuomba sana mungu akupe kilicho bora maana mimi na ww hakuna anayejuwa ya kesho,
m'bora wa leo kesho anaweza kuwa si bora tena
 
Wapo wengi,kuna mmoja wenzake aliomaliza nao form four wakafeli na kwenda certificate yeye akaamua kurisit,wamemaliza diploma bado anarisit,wanapata ajira ndio akashtuka,too late.
Tangia we ulikua chini mpaka umemkuta mpaka upo chuo yeye bado anasubiri matokeo ya o level, dah inauma sana ingekua Mimi nisingepoteza muda tena kwa sasa ningejikita ktk ujasiriaMali tu.kusoma badae.
 
Hataki kuzungumzia Future yenu kwa sababu hata future yake yeye bado anashindwa kuitathmini..

Halafu suala la wewe kutaka kuolewa baada ya chuo sio wewe unaeamua, fanya kwanza linalo kukabiri..
Marriage is not something you can wear on your finger, You can buy your ring but you can buy your husband
 
Tatizo huyo mwanaume anapenda shule wakati shule haimtaki

Mshauri afanye mambo mengine aachane na mambo ya shule manake umri unaenda na ye anazidi kupambana na form four tu

Kuhusu mapenzi nahisi huyo mwanaume amekata tamaa ya maisha kiujumla ndio maana anashindwa kukupa jibu la moja kwa moja kuhusu future yenu

Kama unampenda kiasi hiko mshawishi aanzishe hata biashara
Kuna maisha bila shule
 
Kama unampenda "achana nae kabisaa"
Kwa sababu mtu kuresit mara zote hizoo Kutakuwa na sababu, wewe labda ndo utakuwa unamtoa katika full concentration katika masomo yake .
 
Back
Top Bottom