Empress_sheila
JF-Expert Member
- Apr 16, 2022
- 293
- 339
Mimi ni Muislam kwa baba na mama na hatuna historia ya dini nyingine labda huko nyuma kabisa ambapo hata bibi zangu hawakuwepo au hawajui, imetokea mimi tu kuupenda ukiristo kiasi ambacho tangu niko form one miaka zaidi ya ishirini kubadili majina yangu na kuwa ya Kikiristo na nilikua nikisema baba yangu mkristo mama yangu ndiyo Muislam.
Bahati mbaya nikiwa form two nilikaa hostel ya waroma kwahivyo nilikuwa napenda wakati mwingine kwenda kanisani japo nilikua sielewi kitu, kuna wakati napotezea naanza kusali kiislam kwasababu dini ya Kiislam naijua nimesoma madrasa nikiwa mdogo na hakuna kitabu cha dini kina kina kinanishinda kusoma na hapo zamani nilikua nikisia mtu anasoma kuruan nalia bila kujua nalilia nini nikawa namwambia mama mbona nie nalia nikiona au kusikia kuruan inasomwa? Mama ananiambia tu inaitwa midadi hiyo.
Nimejikuta tu wanangu sijawapeleka madrasa na shule nimewapeleka shule za kikiristo na sipendi kabisa za kiislam wala madrasa na huwa nawaambia wanangu nendeni kanisani, na utu uzima huu kuna wakati nilipata majanga makubwa nikaona njia sahihi ni kuombewa kanisani nikaenda roma kuombewa ndani ya siku tatu pepo likatoka na nimeendelea kusali kiroma nikiwa nyumbani na natumia maji ya baraka wakati mwingi nahisi kabisa yananisaidia, halafu nikiwa kanisani nina amani zote nachokisema nakielewa nachokisali nakielewa! Naona mahubiri ya father nayaelewa vizuri na hapa nyumbani redio nasikiliza redio Maria tu na naifurahia.
Sasa wakuu nisaidieni hili ni pepo au nini? Je nibadili dini na utu uzima huu? Au nifanyaje nifute historia hii? Yaan sasa hivi ndiyo nazidi kuzama kwenye ukristo kiasi ambacho hata wanangu natamani waanze mafundisho, au kuna sehemu sijielewi?
Bahati mbaya nikiwa form two nilikaa hostel ya waroma kwahivyo nilikuwa napenda wakati mwingine kwenda kanisani japo nilikua sielewi kitu, kuna wakati napotezea naanza kusali kiislam kwasababu dini ya Kiislam naijua nimesoma madrasa nikiwa mdogo na hakuna kitabu cha dini kina kina kinanishinda kusoma na hapo zamani nilikua nikisia mtu anasoma kuruan nalia bila kujua nalilia nini nikawa namwambia mama mbona nie nalia nikiona au kusikia kuruan inasomwa? Mama ananiambia tu inaitwa midadi hiyo.
Nimejikuta tu wanangu sijawapeleka madrasa na shule nimewapeleka shule za kikiristo na sipendi kabisa za kiislam wala madrasa na huwa nawaambia wanangu nendeni kanisani, na utu uzima huu kuna wakati nilipata majanga makubwa nikaona njia sahihi ni kuombewa kanisani nikaenda roma kuombewa ndani ya siku tatu pepo likatoka na nimeendelea kusali kiroma nikiwa nyumbani na natumia maji ya baraka wakati mwingi nahisi kabisa yananisaidia, halafu nikiwa kanisani nina amani zote nachokisema nakielewa nachokisali nakielewa! Naona mahubiri ya father nayaelewa vizuri na hapa nyumbani redio nasikiliza redio Maria tu na naifurahia.
Sasa wakuu nisaidieni hili ni pepo au nini? Je nibadili dini na utu uzima huu? Au nifanyaje nifute historia hii? Yaan sasa hivi ndiyo nazidi kuzama kwenye ukristo kiasi ambacho hata wanangu natamani waanze mafundisho, au kuna sehemu sijielewi?
