Naomba ushauri juu ya mimba isiyo na baba

Naomba ushauri juu ya mimba isiyo na baba

Inaonekana mlikuwa na matatizo na mumeo tangu kipindi cha uchumba wenu, lakini ukachukulia poa tu. Now ndo unaanza kujuta anyway hayo yalishapita.

Hakuna mtoto asiye na baba, na mumeo ana haki ya kujua kuhusu ujauzito wako kwa kuwa yeye ndo mhusika. Na mwisho wa siku anatakiwa amlee na kumtunza mwanae kwa hiyo wewe mwambie tu, ila usirudi kwake kwanza. Hakawii kukupiga hadi mimba itoke. Ingawa natamani nijue nini kimempata hadi anaanza kukupiga tu hovyo. Muweke kwenye maombi, ndoa nayo ni vita my dear
 
Naboti

Naweza kusema pole sana kwa kipigo..ila nachoamini hujasema vzr chanzo cha huyo bwana mpaka afikie kukupiga,inamaana atakua mwehu sasa,mtu hawezi toka huko atokako akafika na kuanza kukupiga tu bila sababu,hajanywa pombe,hajavuta bangi,hamjakwaluzana,hajachanganyikiwa na anafika na kushusha kipigo hapana hapana! Kama kuna jambo sema ili tujue tunakushauli nini.hata kama kuna mahala ulikosea wewe b4 sema bila kuficha ili tukufundishe namna ya kutengeneza upate amani
 
Last edited by a moderator:
Hilo janaume lako litakua ni fuasi la UKAWA tu.
 
Yaani upigwe tuu bila sababu? Hujasema kama ni mlevi au laa wewe rudi tuu bado unampenda kuna jambo unaficha hapo bado hujaeleza vizuri.
 
Wamekupa ushauri nami acha nitoe wangu kidogo. Kwa kweli, mara nyingi saana, wanawake wengi hupigwa na waume wao pale kwenye mwanzo wa mimba changa. Sitaki ubishi wa hao waliosoma shule za kata, nataka ubishi wa wazee waliokaa na ndoa muda mrefu. Wewe muhusika, jaribu kufikiri, ni tangu lini alianza kukupiga?? Utakuta ni wakati huo huo mimba ilipo tunga.

Sasa, ka ni hivyo, mtoto wako atakuwa tofauti na huyu aliyeko sasa. Yaani kama huyu ni ke ajaye atakuwa ni me. Au huenda mimba hii ikawa mapacha.
Hakuna sababu ya kumficha ujauzito huu.

Mtoto akija kuwa mkubwa, atamjua babake tu na utashangaa umekula naye shida halafu mtoto analilia kwenda kwa babake. Utamzuia? Mwarifu ujauzito huu tena kupitia kwa wazazi wako na wake.

Ajue kuwa anamzigo mahali wa kutunza asikuachie kazi hii. Nakuhakikishia, yeye kujua ujauzito wako hakumaanishi ni warrant wa kukurudisha nyumbani. Ningetamani mrudiane kwa ajili ya malezi ya watoto hawa, kufungana jela sijui faida yake kwako, ila fikiri zaidi ukiona yafaa, mfunge
 
Pole dada hawa wanaume wanatupa wkt mgumu bure,km unakipato chako cha uhakika na unaona unaweza kuendesha maisha yk vzr basi zaa huyu mtoto umlee mwenyewe kumbuka atakuja kukusaidia ww mwenyewe hapo baadae,huyo shetani mpotezee,maisha gan ya kupigana bl sbb asije akakutia kilema cha maisha bure.

Always Uwa Nashaur Wanawake Kabla Ya Kuingia Kwenye Ndoa, Hakikisha Angalau Unao Uwezo Binafs W Kuendesha Maisha Pasipo Mtegmea Mwanaume Moja Kwa Moja, Matokeo Yake Uwa Kma Haya Mwanamke Ujikuta Mtumwa Ndan Ya Nyumba Mojawapo Ya Sabbu Ni Kutokua Na Uwezo Binafsi. Fanyeni Hayo Ya Msingi Hili Mwisho Wa Siku Msije Kuahibika Kma Hivi,

Unadhan Kma Mwanamke Anakua Na Uwezo Wake Binafsi Angewaza Hayo?? Nan Anaependa Mateso?? Hata Kma Ni Upendo Sio Uwe Mtumwa Na Mateso Juu...Hapo Unakusnya Vyako Unachomoka Kimpango Wako Sema Inakuaga Ngumu Coz Unakuta Mwanamke Anamtegmea Mwanaume Kwa Kila Kitu.
 
Kichapo bila sababu yoyote?
Story ya upande mmoja
 
Kichapo bila sababu yoyote?
Story ya upande mmoja

Hata ikiwa ni stori ya upande mmoja kipigo hakikubaliki kwenye familia.

Kama hataki kuachana naye basi atafute kaka zake naye wamdunde vizuri aone raha ya kupigwa.

Huruma hailei mwana akishamtoa meno atakwenda kutafuta mwengine.
 
Always Uwa Nashaur Wanawake Kabla Ya Kuingia Kwenye Ndoa, Hakikisha Angalau Unao Uwezo Binafs W Kuendesha Maisha Pasipo Mtegmea Mwanaume Moja Kwa Moja, Matokeo Yake Uwa Kma Haya Mwanamke Ujikuta Mtumwa Ndan Ya Nyumba Mojawapo Ya Sabbu Ni Kutokua Na Uwezo Binafsi. Fanyeni Hayo Ya Msingi Hili Mwisho Wa Siku Msije Kuahibika Kma Hivi, Unadhan Kma Mwanamke Anakua Na Uwezo Wake Binafsi Angewaza Hayo?? Nan Anaependa Mateso?? Hata Kma Ni Upendo Sio Uwe Mtumwa Na Mateso Juu...Hapo Unakusnya Vyako Unachomoka Kimpango Wako Sema Inakuaga Ngumu Coz Unakuta Mwanamke Anamtegmea Mwanaume Kwa Kila Kitu.

Halafu uzuri simtegemei kwa lolote yeye anauza sokoni ni muajiriwa wa serikali nimesoma mwaka huu ndo nagraduate degree ya pili so simtegemei labda ndo maana anakazana kunipiga.
 
Halafu uzuri simtegemei kwa lolote yeye anauza sokoni ni muajiriwa wa serikali nimesoma mwaka huu ndo nagraduate degree ya pili so simtegemei labda ndo maana anakazana kunipiga.

That could be the reason ana some inferiority complex issues...yaani ww uqe na Mastaz afu yeye anauza sokoni tu?
 
Halafu uzuri simtegemei kwa lolote yeye anauza sokoni ni muajiriwa wa serikali nimesoma mwaka huu ndo nagraduate degree ya pili so simtegemei labda ndo maana anakazana kunipiga.

Basi, Fanya Fanya Tuu Kuachana Nae, Aina Manaa Uhusiano Wa Mateso Namna Hiyo.
 
Kwa Mjibu Wa Mada Yako Huyo Jaa Hakuwa Hivyo Toka Mwanzo Kabadilika Tu Hivi Kalibuni, Mimi Naami Kuna Kitu Umekifanya Kinachompa Hasira Kila Anapokuona Kama Sivyo Basi Amelogwa Nakushauli Hiyo Mimba Usitoe Kwanza Futa Kabisa Hayo Mawazo Mjulishe Mwenzio Muendelee Kulea Mimba Huku Ukiwa Kwenu Na Ninaamini Mtarudiana Tu Hata Ungeapa Kwa Miungu Wote Unaowajua Ipo Siku Mtaludiana
 
Kwa Mjibu Wa Mada Yako Huyo Jaa Hakuwa Hivyo Toka Mwanzo Kabadilika Tu Hivi Kalibuni, Mimi Naami Kuna Kitu Umekifanya Kinachompa Hasira Kila Anapokuona Kama Sivyo Basi Amelogwa Nakushauli Hiyo Mimba Usitoe Kwanza Futa Kabisa Hayo Mawazo Mjulishe Mwenzio Muendelee Kulea Mimba Huku Ukiwa Kwenu Na Ninaamini Mtarudiana Tu Hata Ungeapa Kwa Miungu Wote Unaowajua Ipo Siku Mtaludiana

Hata Kma Kuna Kitu Amekifanya Kinampa Hasira, Kumpiga Daily Ndio Soln?? Mambo Mengine Ni Ya Kiwendawazimu Kma Haya, Afanye Afanye Jamaa Ajirekebish Akizingua, Afanye Fanye Tuu Kuchukua Ustaarabu Wake.
 
Halafu uzuri simtegemei kwa lolote yeye anauza sokoni ni muajiriwa wa serikali nimesoma mwaka huu ndo nagraduate degree ya pili so simtegemei labda ndo maana anakazana kunipiga.
Sema ukweli, nadhani wakati ukisoma ulichepuka akakunasa au kauli zako kwake ni hatari. Kila wakati najaribu kuwahusia akinadada kabla ya kuolewa waangalia status za wanaume hao. Kama unamzidi kisomo, inferiority complex itawafanya ndoa iwe ngumu na mwisho wake ni kuachana. Ukimzidi mwanaume umri, hii nayo shida hasa ikifika saa 9 hata kabla ya saa 12 jioni.
 
Nyie hawa watu wenye ndoa baadhi huwa na matatzo. Pia siku zote mtu humsemea mwenzake ndo chanzo! Kwa nini unasema akijua ninamimba yake atakurudia?? Huoni kama mwenzio anakuhitaji?? Mwanamke siku zote ni mwombelezaji mumy hujasimama katika nafasi yako. Polee
 
Kwanza kabisa let me start by my apologies on what I am going to comment on your post.

in my view naona kama wewe mwenyewe hujitambui, hujielewi.

Unawezaje kushirikisha jukwaa dhambi zako eti nitoe au nilee mimba. Kama unataka kutoa katoe mwenyewe usije shirikisha jukwaa.

Pili nashindwa kuelewa kama akisikia una mimba yake atakungangania kivipi while unasema hakupendi anakupiga.

hiki kizazi mnatakiwa maombi sana. as a woman you have to stand firm na ujue unafanya nini in your life.

Be real be a woman.

Period.

again very sorry.
 
Naboti

Sio kweli mwanamme atoke atokako akupige tu lazima kuna sababu ingawa hata kama kuna sababu hapaswi kukupigia kibinadamu.

Lakini kama mwaname mumeachana kurudina ni lazima kuwe na ridhaa ya nyote wawili hata kama una ujauzito wake.(Nakusudia nyinyi ikies ni waislamu na ndoa mlifunga hivyo kwa taratibu za kiislamu)

Kwa ufupi lea mimba yako mazae mtoto wako salama ata akija akijuwa akisikia kwamba una mtoto wake utakachokubali wewe ni aje na huduma za mtoto tu. na hata kama akimuhitaji mtoto wake mpe achukue lakini sio kurudiana naye wewe na kulala naye kitanda kimoja.

ukishazaa tafuta anayekupenda kwa mapenzi ya heshima na ya dhati muoane muanze maisha mapya huyo ulokuwa naye si mume ni gumegume tu.
 
Last edited by a moderator:
Nenda kwenye maombi huko kuna mabingwa wa ushauri fasaha kuifanya ndoa yako iwe ya furaha hata ikiwa ni mashetani yameingilia kati yataombewa na kufukuzwa kabisa na utaishi kwa amani na starehe katika ndoa yako na kusahau kabisa kuwa ulishapata masaibu kama hayo tena hawachagui mtu wa kumhudumia awe mwislamu mkristo au asiye na dini wote wanapewa huduma za maombezi sawa na kwa kiwango kilekile. tahadhari usijiabishe bure kwa kukitoa hicho kiumbe cha mungu hauwezi kujua kama ndiyo angekuwa Nyerere wa kizazi chake yote mwachie mwenyezi mungu ndiye mwamuzi kwa usadizi wa maombi.
 
Back
Top Bottom