Naomba Ushauri Jinsi ya Kuendelea na Masomo ya Juu

Easymutant

R I P
Jun 3, 2010
2,564
1,129
Bila kusahau kuzingatia umri wake 43yrs now so wana JF naomba ushauri uzingatie na umri wa jamaa.

Nafahamu kabisa hapa nitapata msaada we ukweli ninaoamini utanisaidia,
Nina mpango wa kuendelea na masomo ya juu at least the minimum to be 1st degree
lakini background yangu ni form four leaver nilijiendeleza ma course za IT kwa sasa nina MCSE na CCNA mwakani by January or Feb ninampango wa kufanya mtihani wa CCNP je kuna uwezekano nikawa nakubalika kujiunga na chuo chochote kikuu ambayo kiko recognizable nikaweza kufanya degree? na kama sikubaliki nifanyeje/niongeze kitu gani ili niweze kuwa eligible to join the chuo wakuu?

NB:Nimefanya kazi za IT kama System administrator kwa miaka mitatu sasa naomba kuwakilisha na ninaamini kwamba greet thinkers will help me out,



Asanteni
 
kwanza nikupe pongezi kwa kuwa na moyo wa kujiendeleza. Pili kuwa form four leaver isikupe tabu kwani sio wote wanaosoma degree ya kwanza wamemaliza form six. Kikubwa tu uangalie je hizo kozi ulizosoma zinatambulika kama kigezo cha kujiunga na degree? huwa kuna sifa ambazo zinaweza kumuingiza mtu chuo kama equivalent qualification. Mfano kwenye degree nyingi ukiwa na diploma unaweza kupata admission. sasa sijui hizo kozi zako kama ni diploma manake mie si mtaalam wa ICT. pili waweza kufatilia sifa za kujiunga na vyuo vikuu kwenye hiyo kozi unayoitaka.
 
i think unaweza kuingia as matured student,sehemu kama IFM,ila utahitajika kufanya entry exam...am not soo sure though!
 
unaweza kwenda au kucheki kwenye website ya UDSM computing centre ukaona wao wanahitaji mtu mwenye vigezo gani kujiunga na kozi zao. La sivyo ukajiendeleza kupitia vituo vyao mpaka ufikie vigezo wanavyohitaji ili kujiunga na chuo.Hongera sana na usijali umri kwani elimu haina mwisho!
 
Back
Top Bottom