gadrock
Senior Member
- Oct 7, 2016
- 151
- 103
Habari wadau,
Ni wiki ya tatu tu tangu nipate kazi katika moja ya mashirika binafsi hapa nchini. Ni jambo la heri ukizingatia ndio kwanza nimemaliza chuo mwaka jana novemba.
Nilikuwa mwenye furaha sana kama mnavyo jua ( nilikuwa kama ndama aliyetoka zizini kwa mara ya kwanza). Ghafla faraja na furaha niliyokuwa nayo inapotea baada ya afisa muajiri (human resource) kuanza kunisumbua ananitaka kimapenzi (si vibaya), tatizo ni mtu mzima anayekaribia kustaafu (50+) yrs, ameolewa na mume wake ni boss mkubwa tu. Ni kama bibi yangu vile!
Hivi sasa amefikia pabaya, analeta figisu figisu hata kazi zangu haziendi. Ananiambia atahakikisha naiaga ofisi. Kazi naipenda haswa ila afya yangu naipenda zaidi . Nashindwa nifanye nini kwa sasa? Ushauri wenu ni wa msingi sana.
Hali hii inanifanya nashindwa kufikiri sawa sawa.
Ni wiki ya tatu tu tangu nipate kazi katika moja ya mashirika binafsi hapa nchini. Ni jambo la heri ukizingatia ndio kwanza nimemaliza chuo mwaka jana novemba.
Nilikuwa mwenye furaha sana kama mnavyo jua ( nilikuwa kama ndama aliyetoka zizini kwa mara ya kwanza). Ghafla faraja na furaha niliyokuwa nayo inapotea baada ya afisa muajiri (human resource) kuanza kunisumbua ananitaka kimapenzi (si vibaya), tatizo ni mtu mzima anayekaribia kustaafu (50+) yrs, ameolewa na mume wake ni boss mkubwa tu. Ni kama bibi yangu vile!
Hivi sasa amefikia pabaya, analeta figisu figisu hata kazi zangu haziendi. Ananiambia atahakikisha naiaga ofisi. Kazi naipenda haswa ila afya yangu naipenda zaidi . Nashindwa nifanye nini kwa sasa? Ushauri wenu ni wa msingi sana.
Hali hii inanifanya nashindwa kufikiri sawa sawa.