Naomba ushahuri wenu tafadhali

Naomba ushahuri wenu tafadhali

Habari za wakati huu wakuu. Nawasilimu sana.
Moja kwa moja kwenye hoja ya msingi "Naomba Ushauri Wenu Tafadhali".

Nina mchumba ambaye nimekwisha posa na kujitambulisha nyumbani kwao. Tumepanga kuoana mwezi wa saba.

Kwa bahati mbaya kwa sasa ninapitia kipindi kigumu kifedha, kiasi cha kushindwa kutimiza maandalizi ya ndoa na harusi.

Bado sijalipa mahari ( nimetozwa ndefu kidogo 6Millioni), na kiukweli kwa sasa hata kodi ya nyumba inanikimbiza. Mbaya zaidi binti ameshawatangazia watu wake wa karibu na kuwapa kadi za harusi.

Wazee nao wanasema walau nilipe milioni 3 kwanza ndo mambo yaendelee.

Nimejaribu kumwabia tufunge ndoa ya kawaidi (bila harusi) lakini binti, wazazi (wangu na wake) hawako tayari.

Ninaotamani kuomba kuahirisha lakini roho inakataa. Nifanyeje?

Asanteni
Six millions
Mshahara wa boss wangu...

Huyo mwanamke ni mzungu?
Je ulitafutiwa au ulimtafuta?

Nahisi umefumaniwa naye au umempa mimba na ndo maana umeitika kila kitu

Wapare, Upareni!
 
Kwenye mambo ya kuoa usipokuwa makini unaweza kujikuta uko dilema!

Mm kipindi nataka kuoa mwaka juzi nikamwambia mwanamke tarehe flani tunaenda kwenu kutoa mahali, lkn nikamwambia najua ninyi wachaga mnaoenda sana hela mm mahali nitakayotoa haitazidi laki 8, kwa hiyo naomba uwambie kabisa ndugu zako kwamba mchumba wangu hana so mahali mtakayopnga isizidi milion 1
Na kama hutaki kuolewa basi wewe usifanye nlichokwambia alafu wapange mamilion huko uone kitakachotokea.

Akatafuta namba ya babaake mdogo akampigia huku analia kwamba mchumba wangu hana kitu kwahiyo naomba msimpangie hela nyingi.

Basi siku ikafika wakafulukuta wewee, wakanipangia mlion 1 na laki 8 mm nikamwambia mshenga wangu waambie hiyo hela sina kama vipi tuondoke tumeshindwa, tukaanza kunanyua kweli, eee wakasema basi leteni hiyo iliyopo kwanza, nikatoa laki 5 kabla ya harusi nikaongezea lk 3 ikawa laki 8 basi mchezo umeisha.

Nikwambie tu ukweli, katika suala la mahali mabint wenyewe kama anajitambua ataplay part kubwa sana kukutetea, kwasababu Maisha ni yako wewe na yeye sasa akiacha wazazi wake wakunyonge alafu sijui mnaenda kuishije alafu?

Alafu unakuta demu mwenyewe kashafikisha miaka 28+ alafu bado ana act kama bint wa miaka 20! Komaa na wazazi mpaka kielewke uoelwe hata kama ni kwa laki 2 ili mradi mtu wako kaja kuweka heshima kwenu na wewe umeolewa kwa heshima kabisa.

Lkn mkiendelea kuachia wazazi waoange mahali wanavyo taka mataemdelea kumegwa huku ndoa mkiendelea kuzishuhudia kwenye kumbi tu.
 
Six millions
Mshahara wa boss wangu...

Huyo mwanamke ni mzungu?
Je ulitafutiwa au ulimtafuta?

Nahisi umefumaniwa naye au umempa mimba na ndo maana umeitika kila kitu

Wapare, Upareni!
Mkuu sijafumaniwa wala kumpa mimba. Nimetumia utaratibu wa mila na desturi wa kuposa kabisa
 
Habari za wakati huu wakuu. Nawasalimu sana.
Moja kwa moja kwenye hoja ya msingi "Naomba Ushauri Wenu Tafadhali".

Nina mchumba ambaye nimekwisha posa na kujitambulisha nyumbani kwao. Tumepanga kuoana mwezi wa saba.

Kwa bahati mbaya kwa sasa ninapitia kipindi kigumu kifedha, kiasi cha kushindwa kutimiza maandalizi ya ndoa na harusi.

Bado sijalipa mahari ( nimetozwa ndefu kidogo 6Millioni), na kiukweli kwa sasa hata kodi ya nyumba inanikimbiza. Mbaya zaidi binti ameshawatangazia watu wake wa karibu na kuwapa kadi za harusi.

Wazee nao wanasema walau nilipe milioni 3 kwanza ndo mambo yaendelee.

Nimejaribu kumwabia tufunge ndoa ya kawaidi (bila harusi) lakini binti, wazazi (wangu na wake) hawako tayari.

Ninaotamani kuomba kuahirisha lakini roho inakataa. Nifanyeje?

Asanteni
Kwanza mwambie mchumba wako na familia yako ukweli halafu kuna kamati ya harusi.
 
Kwenye mambo ya kuoa usipokuwa makini unaweza kujikuta uko dilema!

Mm kipindi nataka kuoa mwaka juzi nikamwambia mwanamke tarehe flani tunaenda kwenu kutoa mahali, lkn nikamwambia najua ninyi wachaga mnaoenda sana hela mm mahali nitakayotoa haitazidi laki 8, kwa hiyo naomba uwambie kabisa ndugu zako kwamba mchumba wangu hana so mahali mtakayopnga isizidi milion 1
Na kama hutaki kuolewa basi wewe usifanye nlichokwambia alafu wapange mamilion huko uone kitakachotokea.

Akatafuta namba ya babaake mdogo akampigia huku analia kwamba mchumba wangu hana kitu kwahiyo naomba msimpangie hela nyingi.

Basi siku ikafika wakafulukuta wewee, wakanipangia mlion 1 na laki 8 mm nikamwambia mshenga wangu waambie hiyo hela sina kama vipi tuondoke tumeshindwa, tukaanza kunanyua kweli, eee wakasema basi leteni hiyo iliyopo kwanza, nikatoa laki 5 kabla ya harusi nikaongezea lk 3 ikawa laki 8 basi mchezo umeisha.

Nikwambie tu ukweli, katika suala la mahali mabint wenyewe kama anajitambua ataplay part kubwa sana kukutetea, kwasababu Maisha ni yako wewe na yeye sasa akiacha wazazi wake wakunyonge alafu sijui mnaenda kuishije alafu?

Alafu unakuta demu mwenyewe kashafikisha miaka 28+ alafu bado ana act kama bint wa miaka 20! Komaa na wazazi mpaka kielewke uoelwe hata kama ni kwa laki 2 ili mradi mtu wako kaja kuweka heshima kwenu na wewe umeolewa kwa heshima kabisa.

Lkn mkiendelea kuachia wazazi waoange mahali wanavyo taka mataemdelea kumegwa huku ndoa mkiendelea kuzishuhudia kwenye kumbi tu.
Nashukuru kaka kwa ushahuri wako mwema. Ninaomba kulichukua hili, na mrejesho nitakupa. Asante
 
Nashukuru kaka kwa ushahuri wako mwema. Ninaomba kulichukua hili, na mrejesho nitakupa. Asante
Poa mkuu, komaa na bint mpige hata bit kidogo, weka msimamo mwambie awaeleze ukweli wazazi wake kwamba huna kitu na yeye anaoneshe ushirikiano kukutetea, kama anataka kweli kuolewa.
 
Samahani kwa kuchangia nje na ulichotaka kushauriwa.
Ninachokijua mimi wewe na mchumba wako mkikubaliana kuoana ishu ya mahali huwa ni bargainable mpk kiasi ambacho wewe unaweza kulipia sio wakuforce nje ya uwezo wako.
Sasa ilikuaje wewe ukakubali kulipa mahali kubwa kiasi hicho?.
Swali la msingi:
Huyo mwanamke ni BIKRA?
 
Samahani kwa kuchangia nje na ulichotaka kushauriwa.
Ninachokijua mimi wewe na mchumba wako mkikubaliana kuoana ishu ya mahali huwa ni bargainable mpk kiasi ambacho wewe unaweza kulipia sio wakuforce nje ya uwezo wako.
Sasa ilikuaje wewe ukakubali kulipa mahali kubwa kiasi hicho?.
Swali la msingi:
Huyo mwanamke ni BIKRA?
Si bikira
 
Milion 6 halafu mkioana mkale nini nyie wote na huyo mchumba wako mna matatizo sana , unakomaa mpaka kodi yenyewe inakushinda? Kwaninj usiwe mkweli wambie hauna hizo tatizo mnadanganya wasichana wewe mboga 7 ona sasa unavyo adhirika, na magu kabana kila kona fungu la mchicha tu mia 5, huyo mchumba kuwa naye makini atakuendesha huyo mtajikuta baada ya ndoa mnahamia ukweni maisha yamewashinda
 
Kodi ya nyumba inamshinda halafu anakubali kulipa mahari ya millioni 6!!!

Waambie mahari millioni tu au unaingia mitini wasikufanye mgongo wao wao kutafuta utajiri kwa nguvu.
Ndiyo chakujiuliza hicho mnafunga ndoa leo kesho mnafukuzwa kwenye nyumba kodi imeisha
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Tuachane na ndoa embu tujadili hiyo mahali kwanza.
 
Habari za wakati huu wakuu. Nawasalimu sana.
Moja kwa moja kwenye hoja ya msingi "Naomba Ushauri Wenu Tafadhali".

Nina mchumba ambaye nimekwisha posa na kujitambulisha nyumbani kwao. Tumepanga kuoana mwezi wa saba.

Kwa bahati mbaya kwa sasa ninapitia kipindi kigumu kifedha, kiasi cha kushindwa kutimiza maandalizi ya ndoa na harusi.

Bado sijalipa mahari ( nimetozwa ndefu kidogo 6Millioni), na kiukweli kwa sasa hata kodi ya nyumba inanikimbiza. Mbaya zaidi binti ameshawatangazia watu wake wa karibu na kuwapa kadi za harusi.

Wazee nao wanasema walau nilipe milioni 3 kwanza ndo mambo yaendelee.

Nimejaribu kumwabia tufunge ndoa ya kawaidi (bila harusi) lakini binti, wazazi (wangu na wake) hawako tayari.

Ninaotamani kuomba kuahirisha lakini roho inakataa. Nifanyeje?

Asanteni
Fata mfuko wako unavyosema hao wazaz wanaotaka harusi iwe kubwa waambie watoe pesa zao mfukoni shubaaaaah miti
 
Hjitambui hyo mwanamke anayo ya dhahabu ,,simama kama una ndevu ,, tena mwambie umeahirisha mpaka mwakani !!akah acha umandazi jomba
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom