binywa
Member
- May 31, 2012
- 18
- 2
Habari zenu ndugu zangu popote mlipo.
Mimi ni mgeni ktk forum hii na nimekuwa nikivutiwa sana na hoja mbalimbali hapa jamvini.
Kuna jambo nahitaji ushauri wenu. Mimi ni kijana (male)wa miaka 28 nina mchumba ambae ana miaka 22, na tumekubaliana kufunga ndoa kwani tayari nimekwisha jitambulisha kwao. Wiki iliyopita nimesikia kuwa mchumba wangu anasema (kwa watu wengine) kuwa alinikubali kwa sababu tu mimi ninafanya kazi na ninajimudu maisha yangu lakini kutoka moyoni hanipendi bali anampenda kijana mwingine ambae aliwahi kumchumbia ila binti alimkataa eti kwa sababu anafanya kazi ya ulinzi na hali yake ni duni kifedha, na ana wasiwasi na uaminifu wangu kwake kwa sababu anahisi bado nina mahusiano na girlfriend wangu wa zamani so haamini kama kweli yule nimemwacha yeye anaona bado tunaendelea na mahusiano. Anasema hivo kwa sababu kuna harusi fulani nilialikwa na nilitakiwa kwenda na mchumba wangu ila mchumba wangu alichelewa kufika na bila kupanga au kujua huyo girl friend wangu wa zamani nae alikuwa amealikwa kwenye harusi hiyo na alikuja na boyfriend wake mpya so tukakaa meza moja. Mchumba wangu alivyoingia ukumbini aliona nimekaa meza moja na huyo Ex girlfriend wangu na mimi sikujua kama mchumba wangu amefika kwani nilikua napiga simu na haikupokelewa kwa zaidi ya saa nzima na alivyokuja alikaa meza nyingine, so wakati wa chakula ulipofika tulinyanyuka mimi, my ex girlfriend, na boyfriend wa my ex girl friend. kumbe mchumba wangu alikuwa anatuona lakini ilipofika zamu ya mchumba wangu kuchukua chakula ndipo nikamwona na nikamfuata tukakaa meza moja. baada ya harusi mchumba wangu aliniuliza eti kwa nini nilimuumiza roho kwa kuingia na my ex girlfriend na alidai kuwa mimi ndiye nilimwambia huyo msichana aje baada ya kuona yeye amechelewa, nilimwelewesha na akaonekana kuelewa lakini cha ajabu mchumba wangu alienda kuongea habari kwa watu wengine kama watatu na kusema kua hajui afanye nini kwa kua mimi si mwaminifu kwake.
Mimi kwa upande wangu sina mahusiano tena na huyo ex girl friend wangu japo mchumba wangu haamini ninapomwambia hivo.
Naombeni mnipe ushauri nifanye nini kwani suala la mchumba wangu kuniuliza habari za ex girlfriend wangu huwa inajirudia mara kwa mara na anaonesha dalili zote kuwa yeye haniamini sana. Lakini pia ni jambo hili lililozuka kuhusu huyu kijana mwingine kua yeye anampenda japo sijasikia direct toka kwa mchumba wangu ila nimesikia toka kwa mtu mwingine ambae aliombwa ushauri na mchumba wangu. Nafikiria nimuulize mchumba wangu kuhusu jambo hili kwani naona ni jambo ambalo ni serious.
Tafadhali nisaidieni nifanye nini na ni nifanyeje
Nimefuatilia kwa muda nimepata yafuatayo....... Nisaidieni jamani
Nimejaribu kufuatilia kwa muda mfupi huu ninahisi kuna kitu kinaendelea kati ya huyu mchumba wangu na huyo jamaa mlinzi kwani kuna siku moja (msichana) alikuja nyumbani kwangu tukiwa tunaongea simu ikaita kumbe ni ya yule jamaa mlinzi nilipomwambia apokee alisema kuwa haina haja kwani jamaa hana jipya nilimlazimisha sana lakini bado hakukubali, mimi nikaamua kuacha lakini huyu msichana alipoondoka wakati wa usiku nilimpigia simu msichana kanimtega tu kama jamaa alimpigia akakubali hapo pia wasiwasi ukaongezeka
Na siku nyingine tukiwa tumetulia nilikuwa nachezea simu yangu kumbe msichana alikuwa ananiangalia kwa jicho la kuibia ktk inbox yangu kulikua n sms toka kwa huyo kijana mlinzi alipoona jina la yule jamaa aliongea kwa mshituko akitaka kusoma sms ya huyo kijana huku mapigo ya moyo wake yakienda kasi zaidi na aliposoma alikua km mtu aleetua mzigo mzito uliomlemea......
Kwa taarifa nilizozipata toka kwa rafiki wa karibu wa mlinzi ni kuwa huyu binti ndo alionesha dalili za kumpenda huyu kijana lakini nilipomuuliza binti alisema kua yule kijana alitaka kumwoa ila yeye akakataa...... utata unaendelea kuongezeka
Ndugu zangu kwa kweli kazi bado ni kubwa ila bado naendelea namini nitaupata ukweli ulipo ila naomba ndugu zangu msinichoke kwa kuwaomba ushauri katika hili naamini ushauri wenu ni wa muhimu katika jambo hili
Asanteni
Mimi ni mgeni ktk forum hii na nimekuwa nikivutiwa sana na hoja mbalimbali hapa jamvini.
Kuna jambo nahitaji ushauri wenu. Mimi ni kijana (male)wa miaka 28 nina mchumba ambae ana miaka 22, na tumekubaliana kufunga ndoa kwani tayari nimekwisha jitambulisha kwao. Wiki iliyopita nimesikia kuwa mchumba wangu anasema (kwa watu wengine) kuwa alinikubali kwa sababu tu mimi ninafanya kazi na ninajimudu maisha yangu lakini kutoka moyoni hanipendi bali anampenda kijana mwingine ambae aliwahi kumchumbia ila binti alimkataa eti kwa sababu anafanya kazi ya ulinzi na hali yake ni duni kifedha, na ana wasiwasi na uaminifu wangu kwake kwa sababu anahisi bado nina mahusiano na girlfriend wangu wa zamani so haamini kama kweli yule nimemwacha yeye anaona bado tunaendelea na mahusiano. Anasema hivo kwa sababu kuna harusi fulani nilialikwa na nilitakiwa kwenda na mchumba wangu ila mchumba wangu alichelewa kufika na bila kupanga au kujua huyo girl friend wangu wa zamani nae alikuwa amealikwa kwenye harusi hiyo na alikuja na boyfriend wake mpya so tukakaa meza moja. Mchumba wangu alivyoingia ukumbini aliona nimekaa meza moja na huyo Ex girlfriend wangu na mimi sikujua kama mchumba wangu amefika kwani nilikua napiga simu na haikupokelewa kwa zaidi ya saa nzima na alivyokuja alikaa meza nyingine, so wakati wa chakula ulipofika tulinyanyuka mimi, my ex girlfriend, na boyfriend wa my ex girl friend. kumbe mchumba wangu alikuwa anatuona lakini ilipofika zamu ya mchumba wangu kuchukua chakula ndipo nikamwona na nikamfuata tukakaa meza moja. baada ya harusi mchumba wangu aliniuliza eti kwa nini nilimuumiza roho kwa kuingia na my ex girlfriend na alidai kuwa mimi ndiye nilimwambia huyo msichana aje baada ya kuona yeye amechelewa, nilimwelewesha na akaonekana kuelewa lakini cha ajabu mchumba wangu alienda kuongea habari kwa watu wengine kama watatu na kusema kua hajui afanye nini kwa kua mimi si mwaminifu kwake.
Mimi kwa upande wangu sina mahusiano tena na huyo ex girl friend wangu japo mchumba wangu haamini ninapomwambia hivo.
Naombeni mnipe ushauri nifanye nini kwani suala la mchumba wangu kuniuliza habari za ex girlfriend wangu huwa inajirudia mara kwa mara na anaonesha dalili zote kuwa yeye haniamini sana. Lakini pia ni jambo hili lililozuka kuhusu huyu kijana mwingine kua yeye anampenda japo sijasikia direct toka kwa mchumba wangu ila nimesikia toka kwa mtu mwingine ambae aliombwa ushauri na mchumba wangu. Nafikiria nimuulize mchumba wangu kuhusu jambo hili kwani naona ni jambo ambalo ni serious.
Tafadhali nisaidieni nifanye nini na ni nifanyeje
Nimefuatilia kwa muda nimepata yafuatayo....... Nisaidieni jamani
Nimejaribu kufuatilia kwa muda mfupi huu ninahisi kuna kitu kinaendelea kati ya huyu mchumba wangu na huyo jamaa mlinzi kwani kuna siku moja (msichana) alikuja nyumbani kwangu tukiwa tunaongea simu ikaita kumbe ni ya yule jamaa mlinzi nilipomwambia apokee alisema kuwa haina haja kwani jamaa hana jipya nilimlazimisha sana lakini bado hakukubali, mimi nikaamua kuacha lakini huyu msichana alipoondoka wakati wa usiku nilimpigia simu msichana kanimtega tu kama jamaa alimpigia akakubali hapo pia wasiwasi ukaongezeka
Na siku nyingine tukiwa tumetulia nilikuwa nachezea simu yangu kumbe msichana alikuwa ananiangalia kwa jicho la kuibia ktk inbox yangu kulikua n sms toka kwa huyo kijana mlinzi alipoona jina la yule jamaa aliongea kwa mshituko akitaka kusoma sms ya huyo kijana huku mapigo ya moyo wake yakienda kasi zaidi na aliposoma alikua km mtu aleetua mzigo mzito uliomlemea......
Kwa taarifa nilizozipata toka kwa rafiki wa karibu wa mlinzi ni kuwa huyu binti ndo alionesha dalili za kumpenda huyu kijana lakini nilipomuuliza binti alisema kua yule kijana alitaka kumwoa ila yeye akakataa...... utata unaendelea kuongezeka
Ndugu zangu kwa kweli kazi bado ni kubwa ila bado naendelea namini nitaupata ukweli ulipo ila naomba ndugu zangu msinichoke kwa kuwaomba ushauri katika hili naamini ushauri wenu ni wa muhimu katika jambo hili
Asanteni