KiuyaJibu
JF-Expert Member
- Aug 29, 2007
- 841
- 175
Nimekuwa na pata wakati mgumu kukubali au kukataa katika utumiaji wa maneno/sentensi ifuatayo, "Naomba unipatie dawa ya mbu."Hii inatumika sana pale mtu anapofika dukani/supermarket kununua hii bidhaa.
Kwasababu ninavyojua mimi dawa ni kwaajili ya tiba/matibabu kutokana na maradhi yaliyokupata;sumu,ni kwaajili ya kuangamiza/kuua kiumbe asiyestahili/kisichostahili kuishi hapa duniani.
Sasa ukisema upatiwe dawa ya mbu ni kweli inakuwa ni kauli sahihi?Cha ajabu watengenezaji na wauzaji wanatumia kauli hiyo bila hata aibu!Wakati ningetegemea wao ndiyo wangekuwa mstari wa mbele kutuweka sawa.Inashangaza kuona kama kuna mtu anadiriki kufuga mbu wakati tunajua madhara yake.
Anyway,ningependa kufahamu ipi ni kauli sahihi.
Kwasababu ninavyojua mimi dawa ni kwaajili ya tiba/matibabu kutokana na maradhi yaliyokupata;sumu,ni kwaajili ya kuangamiza/kuua kiumbe asiyestahili/kisichostahili kuishi hapa duniani.
Sasa ukisema upatiwe dawa ya mbu ni kweli inakuwa ni kauli sahihi?Cha ajabu watengenezaji na wauzaji wanatumia kauli hiyo bila hata aibu!Wakati ningetegemea wao ndiyo wangekuwa mstari wa mbele kutuweka sawa.Inashangaza kuona kama kuna mtu anadiriki kufuga mbu wakati tunajua madhara yake.
Anyway,ningependa kufahamu ipi ni kauli sahihi.