Naomba tupeane ushauri wa jumla kilimo vs ufugaji

Naomba tupeane ushauri wa jumla kilimo vs ufugaji

Mrejesho: Baada ya kuwasiliana naye,kasema kabla hajaomba msaada kwangu,alikuwa tayari kaonyeshwa eneo la ekari 8 alinunue. Amesita kulinunua kwa vile hajajishauri vya kutosha alime au afuge! Aliambiwa bei ni 5 M. Na ameona bora apate ushauri wa kutosha kabla. Hii ina maana yuko tayari kupokea ushauri wako!

Hilo shamba lipo wapi? Linafaa kulimwa mazao gani? Kuwa ekari 8 na kuuzwa mil 5 sio tatizo

Maana kwenye kilimo tunazingatia shamba lipo wapi mfano mkoa gani, hapo tutajua hali ya hewa ya mkoa husika na ili kujua linafaa kwa zao gani

pia tunazingatia unataka kulima nini, hapo tutaangalia zao unalotaka kulima na udongo uliopo shambani kwako vinaendana?

Tutaangalia upatikanaji wa maji nk
Bei pekee isiwe kigezo cha kununua au kutonunua shamba kwa uchache mwambie azingatie hayo niliyomwambia
 
Hilo shamba lipo wapi? Linafaa kulimwa mazao gani? Kuwa ekari 8 na kuuzwa mil 5 sio tatizo
Maana kwenye kilimo tunazingatia shamba lipo wapi mfano mkoa gani, hapo tutajua hali ya hewa ya mkoa husika na ili kujua linafaa kwa zao gani
pia tunazingatia unataka kulima nini, hapo tutaangalia zao unalotaka kulima na udongo uliopo shambani kwako vinaendana?
Tutaangalia upatikanaji wa maji nk
Bei pekee isiwe kigezo cha kununua au kutonunua shamba kwa uchache mwambie azingatie hayo niliyomwambia

Liko kama Km 10 hivi kutoka Morogoro mjini. Maji yapo kwa kuchimba kisima au kutegemea mvua.

Juu ya alime nini,kasema hajapanga,alihitaji ushauri zaidi. Angepata mchanganuo mzuri wa afanye nini na kwa gharama gani,na matarajio yake ingemsaidia.
 
Liko kama Km 10 hivi kutoka Morogoro mjini. Maji yapo kwa kuchimba kisima au kutegemea mvua.
Juu ya alime nini,kasema hajapanga,alihitaji ushauri zaidi. Angepata mchanganuo mzuri wa afanye nini na kwa gharama gani,na matarajio yake ingemsaidia.
Mkuu mm ni mkulima na nipo moro, kwa mkoa wa moro tunalima sn nyanya,mpunga na mahindi
Akishajua zao gani anataka kulima ningeweza kumpa mchanganuo mzuri maana hayo ndio mazao niliyo na uzoefu nayo
 
Mkuu kumshauri mstaafu yataka moyo.
Kama ana mtaji mkubwa ni aheri angejenga nyumba ya gharama nafuu aweke wapangaji.

Au lah, afanye ufugaji wa mbuzi. Mpaka mwezi huu bei ya mbuzi makamo ya kuzaa ipo chini sana karibu minada yote wilayani Mvomero. Kwa sh 3000000 anaweza kununua mbuzi hadi80+ make jike linasimamia 30000 na beberu kubwa50000.

Atajenga banda lenye ulinzi madhubuti na atamuajiri kijana mchungaji.

Kuondoa vurugu na usumbufu machungani, anunue na lau ng'ombe3 kutuliza ukimbiaji wa mbuzi wawapo machungani.

Ng'ombe kwa msimu wanauzwa hadi 200000 mkubwa.
Ni hayo tu mkuu mwambie atulize akili ktk mipangilio ya pesa.
 
Wastaafu ni wa kushauri na kuhakikisha kwamba hawatapeliwi. Ni vizuri kulima kuliko kufuga. Umesema ana milioni 20? Ni kidogo ila M8 anunue shamba, alisafishe na aanze na kilimo cha mvua wakati huo akitumia kiasi kilichobaki kuchimba maji na baada ya kuzoea mazingira afanye kilimo cha umwagiliaji wa mbogamboga.
 
Wastaafu ni wa kushauri na kuhakikisha kwamba hawatapeliwi. Ni vizuri kulima kuliko kufuga. Umesema ana milioni 20? Ni kidogo ila M8 anunue shamba, alisafishe na aanze na kilimo cha mvua wakati huo akitumia kiasi kilichobaki kuchimba maji na baada ya kuzoea mazingira afanye kilimo cha umwagiliaji wa mbogamboga.
Mkuu kwa hali ya hewa ya miaka leo nachelea kumshauri mstaafu kuingia moja kwa moja na kilimo hasa kwa yule hakuwa akijihusisha nacho.
Binafsi nimemshauri ajihusishe na ufugaji wa mbuzi make ni mifugo inayo vumilia ukame na haishambuliwi na magonjwa kadharika mbuzi wanakuwa na kuzaliana haraka. Ni mradi ambao hauna stress kulinganisha na mingine.
Pia ujenzi wa nyumba nao ni stress free mpangaji akizingua mnaachana bila chuki wala uharibifu na hakuibii.
 
Mkuu kwa hali ya hewa ya miaka leo nachelea kumshauri mstaafu kuingia moja kwa moja na kilimo hasa kwa yule hakuwa akijihusisha nacho.
Binafsi nimemshauri ajihusishe na ufugaji wa mbuzi make ni mifugo inayo vumilia ukame na haishambuliwi na magonjwa kadharika mbuzi wanakuwa na kuzaliana haraka. Ni mradi ambao hauna stress kulinganisha na mingine.
Pia ujenzi wa nyumba nao ni stress free mpangaji akizingua mnaachana bila chuki wala uharibifu na hakuibii.
Asante kwa ushauri. Mbegu nzuri ya mbuzi anaweza pata wapi?
 
Dah! Kumshauli mstaaf inaitaji hekima sana maana iyo ela ndo finally inabidi mtu unayemshauli umshauli step by step lasivyo atakulilia kichwan aki fell
Asante,ndiyo maana nikaomba ikibidi tumshauri hadi kwenye mchanganuo wa mradi ili ajipange vizuri.
 
Asante,ndiyo maana nikaomba ikibidi tumshauri hadi kwenye mchanganuo wa mradi ili ajipange vizuri.
Cha muhimu kwanza kabla ya yote apate shamba nzuri sana angalau ekari 5 zilizogawanyika kati ya bonde na juu alaf ndo mwiingie step two kama ya kulima au kufuga maana atakua teyari anakianzio
 
Mkuu kumshauri mstaafu yataka moyo.
Kama ana mtaji mkubwa ni aheri angejenga nyumba ya gharama nafuu aweke wapangaji.

Au lah, afanye ufugaji wa mbuzi. Mpaka mwezi huu bei ya mbuzi makamo ya kuzaa ipo chini sana karibu minada yote wilayani Mvomero. Kwa sh 3000000 anaweza kununua mbuzi hadi80+ make jike linasimamia 30000 na beberu kubwa50000.

Atajenga banda lenye ulinzi madhubuti na atamuajiri kijana mchungaji.

Kuondoa vurugu na usumbufu machungani, anunue na lau ng'ombe3 kutuliza ukimbiaji wa mbuzi wawapo machungani.

Ng'ombe kwa msimu wanauzwa hadi 200000 mkubwa.
Ni hayo tu mkuu mwambie atulize akili ktk mipangilio ya pesa.
ushauri murua huu jana nimeenda mvomero nimerud na mbuz kwa bei ya kutupa
 
mwabie aende pale kilolo iringa pale msimu mzima wanalima,,alime ngegele na mahindi alafu hayo mahindi anakuja kuyauza kama mabichi,,muhind moja kwa shamba wananua sh300,,hakika hela yake hatakua ameiwekeza mahala sahihi
 
  • Thanks
Reactions: MC7
Asante kwa ushauri. Mbegu nzuri ya mbuzi anaweza pata wapi?
Mwambie aende mnada wa Mkongeni huko atapata mbegu nzuri za kimasai. Ila ni vizuri pia akachanganya na mbegu za wafugaji wengine kama 'Wamang'ati'na 'Wambulu' ni wavumilivu na huzaliana.
Akiwa na mwenyeji mzuri atamsaidia kupata mbegu ya mbuzi wenye kuzaa mapacha.
Huu ni mradi mzuri sana hakika hatajuta.
 
Mkuu kumshauri mstaafu yataka moyo.
Kama ana mtaji mkubwa ni aheri angejenga nyumba ya gharama nafuu aweke wapangaji.

Au lah, afanye ufugaji wa mbuzi. Mpaka mwezi huu bei ya mbuzi makamo ya kuzaa ipo chini sana karibu minada yote wilayani Mvomero. Kwa sh 3000000 anaweza kununua mbuzi hadi80+ make jike linasimamia 30000 na beberu kubwa50000.

Atajenga banda lenye ulinzi madhubuti na atamuajiri kijana mchungaji.

Kuondoa vurugu na usumbufu machungani, anunue na lau ng'ombe3 kutuliza ukimbiaji wa mbuzi wawapo machungani.

Ng'ombe kwa msimu wanauzwa hadi 200000 mkubwa.
Ni hayo tu mkuu mwambie atulize akili ktk mipangilio ya pesa.
Mkuu hao ng'ombe wa 200,000 wanapatikana wapi??
 
Uamuzi: Mstaafu mzee wetu amezingatia ushauri wenu. Amenunua eneo la ekari 7. Kati ya kilimo na ufugaji,kachagua ufugaji.
Baada ya kununua eneo,kabakiza 15.2 M. Zote hizi anataka kuweka katika ufugaji.
Ombi: Anaomba ushauri wa afuge nini na mchanganuo wa mradi. Asanteni.
 
Km amestaafu kazi maana yake and miaka 55 au zaidi, Anataka alime... Ataweza kusimamia vizuri hao wafanyakazi? Au anataka stress za uzeeni tu? Ushauri wangu afungue duka la nafaka akae mwenyewe kupokea pesa akishirikiana na kijana mmoja wa kazi kwa ajili ya upimaji na mizungiko ya hapa na pale.... Asimamie duka Lake mpaka Mungu atakapomuchukua.vingenevyo watoto akiwakabidhi Mradi wowote kusimamia km hawajielewi watazila pesa zote... Au ajenge nyumba za kupangisha karibu na maeneo ya chuo, umesema yuko morogoro ajenge maeneo km darkcity, barakuda, mzumbe n. K
 
Km amestaafu kazi maana yake and miaka 55 au zaidi, Anataka alime... Ataweza kusimamia vizuri hao wafanyakazi? Au anataka stress za uzeeni tu? Ushauri wangu afungue duka la nafaka akae mwenyewe kupokea pesa akishirikiana na kijana mmoja wa kazi kwa ajili ya upimaji na mizungiko ya hapa na pale.... Asimamie duka Lake mpaka Mungu atakapomuchukua.vingenevyo watoto akiwakabidhi Mradi wowote kusimamia km hawajielewi watazila pesa zote... Au ajenge nyumba za kupangisha karibu na maeneo ya chuo, umesema yuko morogoro ajenge maeneo km darkcity, barakuda, mzumbe n. K
Amestaafu at 55 mwaka jana.
 
Basi afanye biashara atakayoisimamia mwenyewe kwa msaada wa kijana mmoja wa kazi au mtoto wake... Lakini akithubutu kujiweka pembeni kwa 70% atapoteza pesa na zitaisha kabla hata ya miaka sitini.
 
Nina rafiki yangu amestaafu utumishi wa Umma. Anataka afanye investment katika kilimo au ufugaji. Ameniomba ushauri kumchagulia awekeze wapi?
Kwa vile jukwaa hili ni la ushauri,naye siyo mwanachama,naombeni ushauri kulingana na hali halisi iliyopo sasa.
Shikamoo babu.
 
Back
Top Bottom