Naomba Serikali iweke usimamizi wa karibu kwa watu wanaoanzisha biashara ya kuchanganya chakula cha Mifugo

MSIMISEKI SENIOR

JF-Expert Member
Nov 1, 2014
459
287
Mimi ni mfugaji wa kuku, nguruwe na ng'ombe

Miaka ya hivi karibuni kumekuwa na utitiri wa maduka ya kutengeneza vyakula vya Mifugo ambayo havina ubora. Bahati mbaya watengenezaji hao hawana utaalam wowote juu ya mahitaji halisi ya wanyama hasa kuku.

Mara kadhaa nimenunua vyakula vinavyotengenezwa na watu waliopo mitaani kusema kweli havileti matokeo chanya mfano utagaji wa kuku au ukuaji wa kuku wa mayai ni mbaya na ukuaji wa kuku wa nyama ni mdogo sana

Binafsi imefika wakati ikabidi nitafute mtaalam wa Mifugo nimlipe anitengenezee fomula ambazo nikizitumia angalau ninapata matokeo kwa kiasi changamoto niliyonayo ni upatikanaji wa baadhi ya malighafi

OMBI
Naomba Serikali iweke usimamizi wa karibu kwa watu wanaoanzisha biashara ya kuchanganya chakula cha Mifugo kwani anayeumia ni Mfugaji kwa kupata tija ndogo

Ikiwezekana itoe elimu ya utengenezaji wa vyakula vya Mifugo na kuwapa vyeti wale wote wanaojihusisha na kuchanganya vyakula vya Mifugo au basi iwe inafanya ukaguzi ili kudhibiti ubora maana kuna wakati mtu unaenda kutengeneza chakula halafu unakutana na Dagaa zimeoza, Pumba hazieleweki, nk

Mnaohusika tafadhali fikisheni salaam hizi kwa WAZIRI WA MIFUGO
 
Tembelea mkuu kunakituo cha utafiti mifugo TARILI huko mpwapwa unapata kila kitu,hats ukiwa na pumba,dagaaa,majani n.k wanachambua kila kitu kilichomo na wanakwambia chakula au malisho yako yanaupungufu was madini gani au yana cruide proteins (CP) kiasi gani.In short pale kunavitu vingi sana kama ww ni mfugaji ambaye uko serous unatoka na vitu vya kutosha kabisa
 
Nitafute nikupe formular zenye matokeo chanya kwa broiler mkuu....

Epuka kupewa formular za kutengenezea chakula kutoka kwa watu ambao hawana utaalamu wa mifugo na lishe za mifugo (VISHOKA) nitafute nitakusaidia mkuu....
 
usiende mtaani nenda interchick na makampuni makubwa,siku hizi soko huria,ukinunua cha mtaani umependa
 
Mimi ni mfugaji wa kuku, nguruwe na ng'ombe

Miaka ya hivi karibuni kumekuwa na utitiri wa maduka ya kutengeneza vyakula vya Mifugo ambayo havina ubora. Bahati mbaya watengenezaji hao hawana utaalam wowote juu ya mahitaji halisi ya wanyama hasa kuku.

Mara kadhaa nimenunua vyakula vinavyotengenezwa na watu waliopo mitaani kusema kweli havileti matokeo chanya mfano utagaji wa kuku au ukuaji wa kuku wa mayai ni mbaya na ukuaji wa kuku wa nyama ni mdogo sana

Binafsi imefika wakati ikabidi nitafute mtaalam wa Mifugo nimlipe anitengenezee fomula ambazo nikizitumia angalau ninapata matokeo kwa kiasi changamoto niliyonayo ni upatikanaji wa baadhi ya malighafi

OMBI
Naomba Serikali iweke usimamizi wa karibu kwa watu wanaoanzisha biashara ya kuchanganya chakula cha Mifugo kwani anayeumia ni Mfugaji kwa kupata tija ndogo

Ikiwezekana itoe elimu ya utengenezaji wa vyakula vya Mifugo na kuwapa vyeti wale wote wanaojihusisha na kuchanganya vyakula vya Mifugo au basi iwe inafanya ukaguzi ili kudhibiti ubora maana kuna wakati mtu unaenda kutengeneza chakula halafu unakutana na Dagaa zimeoza, Pumba hazieleweki, nk

Mnaohusika tafadhali fikisheni salaam hizi kwa WAZIRI WA MIFUGO
Mimi pia nahitaji kujua fomula ya kutengeneza chakula cha kuku hebu na mimi nipe mawasiliano ya huyo mtaalamu aliyekupa huo utaalamu wa kutengeneza chakula cha kuku
 
Nitafute nikupe formular zenye matokeo chanya kwa broiler mkuu....

Epuka kupewa formular za kutengenezea chakula kutoka kwa watu ambao hawana utaalamu wa mifugo na lishe za mifugo (VISHOKA) nitafute nitakusaidia mkuu....
Nana kakuambia shida ni Formula?

Unajua makamouni ya kutengeneza vyakula yana Formula nyingi na zinabadilika badilika?

Batch ya January inaweza kuwa na Formula tofauti na Batch ya Feb na ubora ukabakia pale pale.

Shida sio Formula na hilo ndo watu hadi leo hawajui wakiamini tatizo ni Formla.

Hata ukipewa Formula ya Interchick baso tatizo litabakia pale pale
 
Nana kakuambia shida ni Formula?

Unajua makamouni ya kutengeneza vyakula yana Formula nyingi na zinabadilika badilika?

Batch ya January inaweza kuwa na Formula tofauti na Batch ya Feb na ubora ukabakia pale pale.

Shida sio Formula na hilo ndo watu hadi leo hawajui wakiamini tatizo ni Formla.

Hata ukipewa Formula ya Interchick baso tatizo litabakia pale pale
Tatizo ni ubora wa malighafi ya kutengeza chakula.
 
Kweli kabisa mkuu, hili ni bomu linalokaribia kulipuka wakati wowote.
 
Ni vyema kujitengenezea mwenyewe kuliko hivyo vya madukani. Watengenezaji wengi wanakosa uaminifu hivyo huvichakachua sana ili kuongeza faida.
 
Back
Top Bottom