Naomba niwaage

Naomba niwaage

Kwa heshima na taadhima, sio mbaya nikiwaaga members wenzangu ambao nimefahamiana nao hapa JF. Pia, kwa dhati kabisa naomba wote wenye niliwakwaza kwa makusudi ama kwa bahati mbaya wanisamehe.

Siamini kama kuna yeyote anaeye tamani kuhitimisha safari yake hapa duniani akiwa mwenye dhambi, kwasababu Mungu wetu mwenye upendo ametupa nafasi ya kutubu dhambi zetu siku zote.

Baada ya kazi sasa nimeona nijitenge kwa muda wa siku kadhaa ili niitazame afya yangu. Kama Mungu akipenda basi tutaendelea kujiona tena, lakini akinipenda zaidi basi yote kheri.

Hakika ninaogopa, nimekuwa na hofu kuu, moyo wangu unahuzunika.

Ngoja nipambanie hii pumzi.

Sent using Jamii Forums mobile app
Update uzi wako mkuu!
 
Mwanangu Ushimen Mungu atukuzwe kwa kukuruzuku maisha tena maana ulikuwa umeshakata tamaa kabisa! Sasa mwanangu usije ukamwacha hata siku moja, kama ukikuwa humjui sasa ni fursa yako kumjua na kumtumikia! Yunafundishwa kwenye Katekismu kwamba Mungu ametuumba ili tumjue, tumpende, tumtumikie na mwisho twende kwake mbinguni. Sasa kama haya ulikuwa umeyasahau ni wakati muafaka kuyakumbuka na kuyatenda! Kila wakati Mungu anapotupa fursa ya pili huwa ana makusudi yake! Mimi nilikoswakoswa kufa kwenye ajali ya gari landcrusier mkonga ikawa nyang'anyang'a lakini nikatoka bila mchubuko, kila nilipogonga humo kwenye gari penyewe ndipo palibondeka siyo mimi! Huwa nikifika hapo nachoka mwenyewe na haya makusudi ya Mungu! Sasa mkuu hiyo dawa iliyokutibu iweke hapa kwa ufasaha kabisa ili wote tujue! Pia toa ushuhuda kabisa!
Mbona hujaweka namba akutumie sadaka kwa Mpesa?
 
Umejuaje kuwa ni mungu na wala sio corona imeghairi kwa hiyari yake yenyewe na kuachana na windo lake?
Siyo kazi yangu kujua hayo mengine, mimi ninachojua Mungu kwamruzuku maisha tena bwana Ushimen basi!!
 
Ebana huu ugonjwa hata mimi nadhan ninao japo sijapima coz kupumua imekua ishu sana at least sa iv pumzi imeachia ila siku mbili tatu nyuma apa nilikua napata tabu sana hasa ikifika usiku sometime naamka saa tisa usiku pumzi zimebana nafanya mazoezi kidogo zinaachia narud tena kulala.Natumia malimao,nakula machungwa na asali kwa sana sa iv naweza vuta pumzi kidogo afadhali sio kama hapa katikati Siku nne zilizopita.
Yan kiukweli huu ugonjwa umeshatapakaa sana dar hapa na mimi ukuniuliza nimeutoa wapi hata sijui kwa sababu nilijitahidi sana kujizuia nisitoke toke lakini wapi ngoma nimekutana nayo nacheza nayo sa ivi.. Tena mimi sijasikia dalili nyingine zaidi ya kushindwa kupumua na sijamwambia yoyote ukiniona wala huwezi jua kama hata ninazo ila nimeacha kutoka kabisa zaidi ya kununua vitu vya msingi tena kwa tahadhari kubwa sana..
 
Acha basi!!! Mbona mm nimekunywa hii na ndio imenisaidia na watu waliniambia ndio yenyew na ukiifananisha na ile ya Madagascar mbona zinafanana jamani!!!

Sent using Jamii Forums mobile app
Siyo yenyewe niskize mimi mrombo
Ijapokua ni dawa pia. Na waweza pia kujifukiza.. iyaka is different. Hili ni iyombo.
Tizama iyaka. Nimelipiga picha hapa shambani kwetu kimara. Karibu upate mbegu
Hii hata mkichinja mbuzi ni kiboko ya shombo unachemshia kwenye supu
20200430_131943.jpg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nakwambiaje hilo ndio nawekaga kwenye subu ya mbuzi unabisha nini kiongozi

CCM DAMUDAMU!!!,CHAMA CHA MAMA &BABA
Achaga ubishi basi mkuu. Silo. Angalia yofauti ya majani yake. Hayo uloweka ni manene. Ya iyaka ni tofauti. Unaweka haya hapa sema umeshindwa tofautisha. Angalia kwa umakini sana majani yalivyo ujur tofauti yake. Fananisha majani na picha uloweka kama vyafanana mkuu
20200430_131943.jpg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ebana huu ugonjwa hata mimi nadhan ninao japo sijapima coz kupumua imekua ishu sana at least sa iv pumzi imeachia ila siku mbili tatu nyuma apa nilikua napata tabu sana hasa ikifika usiku sometime naamka saa tisa usiku pumzi zimebana nafanya mazoezi kidogo zinaachia narud tena kulala.Natumia malimao,nakula machungwa na asali kwa sana sa iv naweza vuta pumzi kidogo afadhali sio kama hapa katikati Siku nne zilizopita.
Yan kiukweli huu ugonjwa umeshatapakaa sana dar hapa na mimi ukuniuliza nimeutoa wapi hata sijui kwa sababu nilijitahidi sana kujizuia nisitoke toke lakini wapi ngoma nimekutana nayo nacheza nayo sa ivi.. Tena mimi sijasikia dalili nyingine zaidi ya kushindwa kupumua na sijamwambia yoyote ukiniona wala huwezi jua kama hata ninazo ila nimeacha kutoka kabisa zaidi ya kununua vitu vya msingi tena kwa tahadhari kubwa sana..
Ninadalili kama zako siumwi chochote zaidi ya pumzi, sema kuanzia jana ninapata nafuu baada ya kuanza kutumia Azithromycin, Predinisorone, aspirin pamoja na matunda yenye vitamin C kwa wingi .Na mida hiyoyo ndio mida ya kubana ila nakupiga pushup napo inanisaidia kupumua vizuri.Nina jifungi siku nzima nikitoka nje natumia mask na sanitizer kila muda ili kulinda wengine.
 
Achaga ubishi basi mkuu. Silo. Angalia yofauti ya majani yake. Hayo uloweka ni manene. Ya iyaka ni tofauti. Unaweka haya hapa sema umeshindwa tofautisha. Angalia kwa umakini sana majani yalivyo ujur tofauti yake. Fananisha majani na picha uloweka kama vyafanana mkuuView attachment 1444777

Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu haya nimeweka kwenye supu ya mbuzi mbona huniamini?

CCM DAMUDAMU!!!,CHAMA CHA MAMA &BABA
 
Huyu mdau amegoma hata kuleta feedback ya matumizi ya dawa anazotajiwa humu jukwaani?

Sent using iphone pro max
 
Huyu mdau amegoma hata kuleta feedback ya matumizi ya dawa anazotajiwa humu jukwaani?

Sent using iphone pro max
Tayari nikiweka feedback mkuu, nime eleza kwa uwazi bila tashwishwi dawa nilizo tumia na mitishamba pamoja na majini niliyo jifukizia nyungu.
Sasa nipo ngangari na nimekuwa mpya kabisa mkuu.
Ebu jaribu kurudi nyuma kidogo utayapata niliyo yaelezea kwenye mrejesho.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Tayari nikiweka feedback mkuu, nime eleza kwa uwazi bila tashwishwi dawa nilizo tumia na mitishamba pamoja na majini niliyo jifukizia nyungu.
Sasa nipo ngangari na nimekuwa mpya kabisa mkuu.
Ebu jaribu kurudi nyuma kidogo utayapata niliyo yaelezea kwenye mrejesho.

Sent using Jamii Forums mobile app
Ni post namba ngapi mkuu hayo majibu yako? Nimeyatafuta sana mpaka nimechoka!
 
Tayari nikiweka feedback mkuu, nime eleza kwa uwazi bila tashwishwi dawa nilizo tumia na mitishamba pamoja na majini niliyo jifukizia nyungu.
Sasa nipo ngangari na nimekuwa mpya kabisa mkuu.
Ebu jaribu kurudi nyuma kidogo utayapata niliyo yaelezea kwenye mrejesho.

Sent using Jamii Forums mobile app


Kwanza kabisa pole na tunafurahi kuwa nawe tena jukwaani mkuu.

Pili, ungefanya update kwenye uzi huu post ya mwanzo kabisa ingefaa zaidi.

Kila la kheri
 
Back
Top Bottom