Habari zenu wakuu,
Leo nimepokea simu ya mdogo wangu akinipa taarifa ya kuachana rasmi na aliyekuwa mkewe madai kuwa mkewe alikuwa akimfanyia vitendo vya ushirikina (limbwata) na mambo yanayo husiana na urozi kiasi cha mdogo wangu kukabidhi mshahara wote kwa mkewe kila apatapo, kumuogopa amuonapo na kushindwa kujiamini.
Mimi binafsi sikuweza kumshauri aachane nae ila nikamwambia awaeleze wazazi maana huenda wao wakawa na jibu zuri au ushauri sahihi zaidi kilichonifanya niandike uzi huu ni kuwa, baada ya kulifikiria sana suala hili nikaona bora nimshirikishe mke wangu kwa kumueleza kisa kizima cha shemeji yake na mkewe.
Jibu alilonipa mke wangu limenishangaza jamani nanukuu ''HAKUNA TATIZO HAPO MUME WANGU, KAMA MKEWE KAMROGA ILI AMPENDE MBONA NI VIZURI KWANI HUENDA MDOGO WAKO ALIKUWA NA MICHEPUKO. MWAMBIE AMRUDISHE TU WALA ASIMUACHE KWANI ALIKUWA AKIMSAIDIA ILI AMPENDE YEYE TU'' Mwisho wa kunukuu.
Jamani mimi nimebaki nimeduwaa maana sijui niseme nini kwa huyu mke wangu, yeye anaona yuko sawa na wala hana wasiwasi na kauli hiyo.Kama ndo ungekuwa wewe ndugu yangu ungefanyeje?