Perry
JF-Expert Member
- Feb 24, 2011
- 10,043
- 2,000
Nimechaguliwa udsm,cheti changu original cha form 4 ninacho,ila kwa bahati mbaya jana nikiwa natoka kuchukua original yangu ya form 6 nikawa nimeiweka pamoja na cheti cha kuzaliwa,nikavisahau kwenye daladala<kwa kifupi vimepotea> bahati nzuri nilikua na photocopy ya cheti cha kuzaliwa iliyokua certified na mahakama to be a true copy of original na ina muhuri wa mahakama,vile vile nimebaki na result slip yangu ya form 6 ingawa imetolewa miaka 3 iliyopita.sasa,nauliza nikienda chuo watakubali kweli kunisajili au watanisumbua maana nimeenda kuriport police wao wameniandkia notice report pekee wakanipa na risiti flani hv baada ya kulipia shiling 500?