Heshima kwenu wote!!
Nimeamua kuomba msaada humu jamvini baada ya kuota ndoto za ajabu kwa siku mbili mfululizo (juzi na jana) zote zikiwa zinahusu wanyama wa porini. Ndoto ya kwanza ilikuwa hivi: Nilijikuta niko juu ya mlima mrefu sana(ndivyo ndoto ilivyoanza hivyo) na ghafla nikawa na shauku ya kushuka mlima ule maana mazingira yale yalinitisha sana. Nilipoanza safari ya kushuka mlima ghafla nikakutana na wanyama wawili ambao ni Dubu na mwingine kama Mbwa mwitu wote wawili wakanivamia na nikaanza kupambana nao. Ghafla nikaanza kupaa kama ndege (huku mbawa zikiwa ni mikono yangu mwenyewe). Wale wanyama wiwili wakawa wanatafuta namna ya kunishusha chini huku wakitoa sauti za ukali sana. Kwa jinsi walivyokuwa wanapigana vikumbo wao kwa wao, Dubu akakasirika na akamgh'ata Mbwa mwitu miguu ya nyuma na ndipo Mbwa mwitu akaishiwa nguvu na Dubu akapambana peke yake. Nikajikuta napaa kwa nguvu hadi kumwacha yule Dubu akiwa na hasira sana. Nikaendelea kushuka mlima na ghafla nikakutana na kundi la Tembo. Mtoto wa tembo akanifuata kwa shari nikamshika mkonga wake kumzuia asinizuru na ghafla akadondoka chini. Mama wa tembo akanifuata kwa hasira kali ajabu na ghafla nikaanza kupaa tena(mbawa zikiwa ni mikono yangu mwenyewe). Yule tembo akanyanyua mkonga wake juu kabisa hadi akanigusa nikiwa angani ingawa alishindwa kunishusha chini!!! Ugomvi ulikuwa wa kutisha sana na niliogopa sana. Baadaye nikajikuta napaa kwa kasi na kumwaccha Tembo yule na ule uwezo wa kupaa ukaniishia nikawa natembea kwa kwaida. Nikaendelea na safari hadi nikafika chini ya mlima bila ya kukutana na kizuizi kingine. Ndoto ikaishia hapo.
Jana usiku nikaota ndoto nyingine: Nipo katikati ya pori nene lililojaa wanyama wakali. Ghaafla nikakutana na Simba na akanivamia nikaokota fimbo pembeni nikaanza kupambana nae hadi nikamuua!!! Ghafla nikaona kundi la Simba wanakuja kwa mbali na njia wanayoijia ndio hiyo hiyo ninayoiendea, nikjawa na woga sana lakini ghafla nikamuona mtu ninayemfahamu yupo pembeni ya njia ileile huku naye akiwatazama Simba wale wakija kwa mbali. Akanipa ushauri kwamba tujifiche nyuma ya kichaka kilicho karibu huenda tukapona. Sikuwa na shaka naye maana namfahamu vizuri nikakubali tukajificha nyuma ya kichaka kile. Wale simba walipita huku wakitoa mingurumo ya hasira kali sana. Baada ya muda kidogo nikiwa nimeshaachana na yule mtu nikaendelea na safari yangu ghafla nikaona kundi la tembo wengi sana wakija kwa njia ileile ninayoiendea!!! Nikaona mtu anapita na gari lenye sura ya nyumba, nikamwambia wewe huogopi kundi lile la tembo wanaokuja mbele yako? Akatazama mbele akawaona wale tembo naye akaogopa sana. Akasimamisha gari lake pembeni lakini akagoma kunipa hifadhi ili tembo wale wapite kwanza!!! Ndipo nikajificha chini ya gari yake pasipo yeye kujua hadi wale tembo walipopita....walikuwa tembo wengi sana sana!!! Ndipo nikaendelea na safari yangu nikafika kwenye kidaraja fulani ambacho ndicho kinachotenga pori hilo na kijiji fulani. Nikaingia ndani ya kijiji hicho na watu wa sehemu ile ni watu watulivu sana na wala sikuona shari yoyote baada ya hapo. Ndoto ya pili ikaishia hapo.
My concern
Kiimani (Be it Islam or Christian) ndoto yoyote ile ina maana yake. Kwahiyo jambo hili nimeliieta jamvini ili kuomba msaada wa possible interpretation ya ndoto hizo. Ningependa mtu akitafsiri ndoto hizo atoe clear framework kulingana na muongozo ya dini yake juu ya masuala ya ndoto(atoe reference ya kifungu husika kutoka kwenye maandiko matakatifu ya dini yake). Please wanajamvi nawasilisha for solution.
Nimeamua kuomba msaada humu jamvini baada ya kuota ndoto za ajabu kwa siku mbili mfululizo (juzi na jana) zote zikiwa zinahusu wanyama wa porini. Ndoto ya kwanza ilikuwa hivi: Nilijikuta niko juu ya mlima mrefu sana(ndivyo ndoto ilivyoanza hivyo) na ghafla nikawa na shauku ya kushuka mlima ule maana mazingira yale yalinitisha sana. Nilipoanza safari ya kushuka mlima ghafla nikakutana na wanyama wawili ambao ni Dubu na mwingine kama Mbwa mwitu wote wawili wakanivamia na nikaanza kupambana nao. Ghafla nikaanza kupaa kama ndege (huku mbawa zikiwa ni mikono yangu mwenyewe). Wale wanyama wiwili wakawa wanatafuta namna ya kunishusha chini huku wakitoa sauti za ukali sana. Kwa jinsi walivyokuwa wanapigana vikumbo wao kwa wao, Dubu akakasirika na akamgh'ata Mbwa mwitu miguu ya nyuma na ndipo Mbwa mwitu akaishiwa nguvu na Dubu akapambana peke yake. Nikajikuta napaa kwa nguvu hadi kumwacha yule Dubu akiwa na hasira sana. Nikaendelea kushuka mlima na ghafla nikakutana na kundi la Tembo. Mtoto wa tembo akanifuata kwa shari nikamshika mkonga wake kumzuia asinizuru na ghafla akadondoka chini. Mama wa tembo akanifuata kwa hasira kali ajabu na ghafla nikaanza kupaa tena(mbawa zikiwa ni mikono yangu mwenyewe). Yule tembo akanyanyua mkonga wake juu kabisa hadi akanigusa nikiwa angani ingawa alishindwa kunishusha chini!!! Ugomvi ulikuwa wa kutisha sana na niliogopa sana. Baadaye nikajikuta napaa kwa kasi na kumwaccha Tembo yule na ule uwezo wa kupaa ukaniishia nikawa natembea kwa kwaida. Nikaendelea na safari hadi nikafika chini ya mlima bila ya kukutana na kizuizi kingine. Ndoto ikaishia hapo.
Jana usiku nikaota ndoto nyingine: Nipo katikati ya pori nene lililojaa wanyama wakali. Ghaafla nikakutana na Simba na akanivamia nikaokota fimbo pembeni nikaanza kupambana nae hadi nikamuua!!! Ghafla nikaona kundi la Simba wanakuja kwa mbali na njia wanayoijia ndio hiyo hiyo ninayoiendea, nikjawa na woga sana lakini ghafla nikamuona mtu ninayemfahamu yupo pembeni ya njia ileile huku naye akiwatazama Simba wale wakija kwa mbali. Akanipa ushauri kwamba tujifiche nyuma ya kichaka kilicho karibu huenda tukapona. Sikuwa na shaka naye maana namfahamu vizuri nikakubali tukajificha nyuma ya kichaka kile. Wale simba walipita huku wakitoa mingurumo ya hasira kali sana. Baada ya muda kidogo nikiwa nimeshaachana na yule mtu nikaendelea na safari yangu ghafla nikaona kundi la tembo wengi sana wakija kwa njia ileile ninayoiendea!!! Nikaona mtu anapita na gari lenye sura ya nyumba, nikamwambia wewe huogopi kundi lile la tembo wanaokuja mbele yako? Akatazama mbele akawaona wale tembo naye akaogopa sana. Akasimamisha gari lake pembeni lakini akagoma kunipa hifadhi ili tembo wale wapite kwanza!!! Ndipo nikajificha chini ya gari yake pasipo yeye kujua hadi wale tembo walipopita....walikuwa tembo wengi sana sana!!! Ndipo nikaendelea na safari yangu nikafika kwenye kidaraja fulani ambacho ndicho kinachotenga pori hilo na kijiji fulani. Nikaingia ndani ya kijiji hicho na watu wa sehemu ile ni watu watulivu sana na wala sikuona shari yoyote baada ya hapo. Ndoto ya pili ikaishia hapo.
My concern
Kiimani (Be it Islam or Christian) ndoto yoyote ile ina maana yake. Kwahiyo jambo hili nimeliieta jamvini ili kuomba msaada wa possible interpretation ya ndoto hizo. Ningependa mtu akitafsiri ndoto hizo atoe clear framework kulingana na muongozo ya dini yake juu ya masuala ya ndoto(atoe reference ya kifungu husika kutoka kwenye maandiko matakatifu ya dini yake). Please wanajamvi nawasilisha for solution.