Naomba kuuliza kwa wanawake tu

Naomba kuuliza kwa wanawake tu

Mkimuyangu

JF-Expert Member
Joined
Oct 5, 2022
Posts
1,054
Reaction score
1,947
Naomba kuwauliza kina dada humu ndani, kuna binti mmoja nilitaka kumuoa lakini akanikatalia kwa kigezo hawezi kuolewa na mimi kwa sababu ni bosi wake.

Kiukweli huyu binti nilitafutiwa na mtu kwa ajili ya kuja kunisaidia kuuza duka langu, lakini siku zilivyokuwa zinakwenda kutokana na kuikubali tabia yake nikaanza kupanga kumuoa.

Lakini alinikatalia na kuniambia hawezi kuolewa na mimi kwani ni bosi wake, baadaye akaja kuolewa na mtu mwingine na akaacha kazi. Sasa kinachonifanya kuja kuuliza, muda mwingi amekuwa akiniambia vitu vyake vya siri, anaishia kuniambia, unayejua wewe na mume wangu tu, usimwambie mtu.

Mfano alikuwa anaumwa akanipigia simu ameenda hospital kakutwa mja mzito lakini nisimwambie mtu, najua mimi tu na mme wake, kama wanawake hii inaleta picha gani? Na bado muda mwingi ananipiga mizinga, akija dukani lazima aombe vitu, ingawa huwa nampa kila anachotaka, lakini nimeanza kujistukia labda ananichukulia bwege?
 
Unaonekana wewe ni mtoto na yeye ni mtoto.

Pili unaonekana wewe bado unampenda.

Kukukataa kwa kigezo cha kua wewe ni boss wake haikua sababu, binti hakua amekukubali hivyo akaona asingizie hiyo sababu.

Sasa cha kukushauri, usiendeleze mawasiliano nae ya karibu. Kaa nae mbali.

Mwambie ajali familia yake na mume wake. Wewe kua bize na mambo yako. Tafta mwanamke mwingine uoe.
 
Unaonekana wewe ni mtoto na yeye ni mtoto.

Pili unaonekana wewe bado unampenda.

Kukukataa kwa kigezo cha kua wewe ni boss wake haikua sababu, binti hakua amekukubali hivyo akaona asingizie hiyo sababu.

Sasa cha kukushauri, usiendeleze mawasiliano nae ya karibu. Kaa nae mbali.

Mwambie ajali familia yake na mume wake. Wewe kua bize na mambo yako. Tafta mwanamke mwingine uoe.
Ahsante
 
Wewe ni wa akiba...in case akikosa kwa kwenda...!!so anafanya hayo yote ili usipotee kwenye ramani...mambo yakiharibika kule anajua ana msaada....yan wew ni km upatu...kikoba....au kama ushawah kubet wew ni "Both Team Will Score"
Ushauli mzuri
 
Unaonekana wewe ni mtoto na yeye ni mtoto.

Pili unaonekana wewe bado unampenda.

Kukukataa kwa kigezo cha kua wewe ni boss wake haikua sababu, binti hakua amekukubali hivyo akaona asingizie hiyo sababu.

Sasa cha kukushauri, usiendeleze mawasiliano nae ya karibu. Kaa nae mbali.

Mwambie ajali familia yake na mume wake. Wewe kua bize na mambo yako. Tafta mwanamke mwingine uoe.
Nina miaka 40 anamika 27, wote ni watu wazima
 
Mabosi hapo ndipo mnapokoseaga, hivi unaanzaje kumtongoza mfanyakazi wako?
yaani nimuache waje watongoze wengine wakati mda wote wakati yuko na mimi nilikuwa namsoma tabia yake nikalizika naye
 
Naomba kuwauliza kina dada humu ndani, kuna binti mmoja nilitaka kumuoa lakini akanikatalia kwa kigezo hawezi kuolewa na mimi kwa sababu ni bosi wake.

Kiukweli huyu binti nilitafutiwa na mtu kwa ajili ya kuja kunisaidia kuuza duka langu, lakini siku zilivyokuwa zinakwenda kutokana na kuikubali tabia yake nikaanza kupanga kumuoa.

Lakini alinikatalia na kuniambia hawezi kuolewa na mimi kwani ni bosi wake, baadaye akaja kuolewa na mtu mwingine na akaacha kazi. Sasa kinachonifanya kuja kuuliza, muda mwingi amekuwa akiniambia vitu vyake vya siri, anaishia kuniambia, unayejua wewe na mume wangu tu, usimwambie mtu.

Mfano alikuwa anaumwa akanipigia simu ameenda hospital kakutwa mja mzito lakini nisimwambie mtu, najua mimi tu na mme wake, kama wanawake hii inaleta picha gani? Na bado muda mwingi ananipiga mizinga, akija dukani lazima aombe vitu, ingawa huwa nampa kila anachotaka, lakini nimeanza kujistukia labda ananichukulia bwege?
Unafaa kuwa mchepuko wake
 
32535692-B34E-4609-8370-ACEFBA947CD2.jpeg

Kuwa makini inayopendwa hapo ni Pochi.. nimeshindwa kuvumilia 🤣🤣🤣🤣🤣🤣
 
Hakuna urafiki usio na faida, kama yeye anaweza kukuomba...hata wewe unaweza kumuomba...utofauti utakuja kwenye vitu mnavyoombana
 
Hakuna urafiki usio na faida, kama yeye anaweza kukuomba...hata wewe unaweza kumuomba...utofauti utakuja kwenye vitu mnavyoombana
Nimempa vitu vingi sana, kabla ya kumtamkia kama ninataka kumuowa maana maisha yake yalikuwa kidogo changamoto,lakini namuona bado anataka niendelee kumsaidia wakati ana mume wake
 
Nimempa vitu vingi sana, kabla ya kumtamkia kama ninataka kumuowa maana maisha yake yalikuwa kidogo changamoto,lakini namuona bado anataka niendelee kumsaidia wakati ana mume wake
Emu peleka msaada wako kwenye watu wa mahitaji. Hapo unapoteza muda na pesa.
 
Back
Top Bottom