Naomba kuuliza kuhusu kuthibitisha vyeti

Naomba kuuliza kuhusu kuthibitisha vyeti

svoca

JF-Expert Member
Joined
Jun 6, 2014
Posts
373
Reaction score
70
Habarini wapendwa!

Mimi naomba kuuliza katika mambo ya certify vyeti, ni kwamba unathibitisha zile copy ambazo unatuma ktk application , au inakuwaje?
 
Ndio. Unatoa copy vyeti vyako. Halafu wakili anagonga muhuri kuthibitisha kwamba ulimuonyesha originals. Certify copy nyingi ukae nazo, hizo ndio utakazotuma.
 
utatumia pesa nying manake zinahitajikaga sana...gonga muhuri kwenye original afu utakua unatoa kopi tu utakapohitaji..haina madhara na ni best way ya kutunza hivyo vijisenti
 
Last edited by a moderator:
Mkuu kuhusu hilo kupiga mhuri vyeti original sijawah sikia jaribu kuthibitisha kwa watu wengine
 
utatumia pesa nying manake zinahitajikaga sana...gonga muhuri kwenye original afu utakua unatoa kopi tu utakapohitaji..haina madhara na ni best way ya kutunza hivyo vijisenti


Ilo si kweli huruhusiwi cheti original kuongezea kitu chochote maana ya certify vyeti kutoa copy na kwenda navyo either kwa hakimu or wakili kuwa wakati anasaini na kugonga muhuri ina maana anathibitisha kuwa alikiona kile cha original ina maana ile copy imetokana na original.
 
Ndio. Unatoa copy vyeti vyako. Halafu wakili anagonga muhuri kuthibitisha kwamba ulimuonyesha originals. Certify copy nyingi ukae nazo, hizo ndio utakazotuma.
Nashukuru mkuu nimekuelewa vilivyo ntafanya hivyo.
 
aisee mimi vyeti vyangu vyote vimegongwa muhuri tangu mwaka 2006 na sijawahi pata navyo shida kabisa...sijui tafuta mwanasheria muulize na aliyenishauri nifanye hivyo ni mwanasheria alienigongea. hebu ulizeni na wengine tuone
 
au njia rahis toa copy then certify halafu utoage kopi ile kopi ya mwanzo manake haya mambo yanamalizaga senti mia mia zetu sana.......na utakapoenda kugonga si ni kwa mwanasheria hebu muulize kesi yangu..mimi niligonga mahaka ya mwanzo pale temeke 2oo6
 
aisee mimi vyeti vyangu vyote vimegongwa muhuri tangu mwaka 2006 na sijawahi pata navyo shida kabisa...sijui tafuta mwanasheria muulize na aliyenishauri nifanye hivyo ni mwanasheria alienigongea. hebu ulizeni na wengine tuone

Tuelewane kitu kimoja hapa ni kwamba unatoa copy unaenda certify alafu unapika copy Kutoka kwenye ile copy uliyo certify then unatumia sehemu yoyote tu na haina tatizo
 
Huwezi kutumia copy ya ile certified copy. Njia rahisi ni kutoa copy nyingi (kama 20 hivi) na kuzigongesha kwa wakili. Zikiisha unatoa tena copy upya
inaruhusiwa tena kutoa copy ile ambayo iko certified mkuu?
 
huko mahakama ya mwanzo pia kuna mawakili. Wakili anakuwa na mhuri maalum anaopewa na mwanasheria mkuu
au njia rahis toa copy then certify halafu utoage kopi ile kopi ya mwanzo manake haya mambo yanamalizaga senti mia mia zetu sana.......na utakapoenda kugonga si ni kwa mwanasheria hebu muulize kesi yangu..mimi niligonga mahaka ya mwanzo pale temeke 2oo6

hapana kaka. Maana ya ule muhuri ni kuthibitisha kuwa wakili ameona nakala halisi. Sasa ukipeleka copy ina maanisha ule muhuri hauna maana tena, haina tofauti na kutogongewa kabisa
Tuelewane kitu kimoja hapa ni kwamba unatoa copy unaenda certify alafu unapika copy Kutoka kwenye ile copy uliyo certify then unatumia sehemu yoyote tu na haina tatizo
 
aisee mimi vyeti vyangu vyote vimegongwa muhuri tangu mwaka 2006 na sijawahi pata navyo shida kabisa...sijui tafuta mwanasheria muulize na aliyenishauri nifanye hivyo ni mwanasheria alienigongea. hebu ulizeni na wengine tuone

vi upload hapa tuone
 
Nakala iliyothibitishwa haiwezi na hairuhusiwi kutolewa nakala. Ikitolewa,nayo itapaswa kuthibitishwa.

Muhimu: Mthibitishaji ni Wakili au Hakimu. Gharama ni maelewano kutokana na mazingira. Mimi pia ni mmoja wa wathibitishaji
 
Hawa utumishi matangazo yao ya kazi sahivi ni lazima kucertify vyeti itakua ni usumbufu tu ila ndio hivyooo no way
 
salam wanajamii. nlikuwa naomba msaada kwa yoyote anayejua sehem gani wanaweza kinisaidia ku certify vyeti vyangu na ni bei gani
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom