Naomba kujuzwa kuhusu maisha ya Same mjini

Naomba kujuzwa kuhusu maisha ya Same mjini

Same pazuri sana mradi mkubwa wa maji umefika hakutakuwa na shida ya maji kama awali. Utafanya mengi nenda ujionee ila fanya kilichokupeleka achana na vidosho utapata shida kubwa sana..
Fafanua,mi najua maeneo ya masandare kuna walozi wengi sana,pia wanawake wengi wa same hawajui kusema no, ni enzi hizo za 1999 nilikuwa pande hizo lakini sijui sasa hali ikoje
 
Ule mradi niliacha umefika pale Mgagau-Mnadani,hivi unategemewa kumalizika lini?Shida ya huo mji ni maji,tabu sana ya maji hapo...Yanapatikana ya chumvi ambayo yanaharibu sana nguo.

Nilikaa Same miezi minne kikazi.Nilifikia sehemu moja inaitwa Elephant Motel.Ipo pembeni ya mji.Chakula hasa matunda na mengineyo,yanapatikana kwenye gulio la Kwasakwasa,gulio lipo kila J'pili,watu wanashuka na vyakula toka milimani,hapo maji ndio tatizo.

Jumamosi maduka mengi yanafungwa sbb wenyeji wengi ni Wasabato.Ila watoto wa Kipare ukimuonja tu,lazima akupandie milimani akutulize.Bar kubwa ni PADEKO na Kimweri karibu na kituo cha Mafuta cha Panone.

Wilaya ina ukame sana,jua kali sana lakini usiku kuna baridi ya upepo(kipupwe),na vumbi kubwa sana ndio maana wadada wengi wanavaa open shoes na soksi.Nyumba za kupanga si gharama sana.

Wewe mkuu unaenda kuwa mtumishi wa Serikali au shirika binafsi?
Daah umeidadavua vizuri sana ,wanawake wa same ni kama warangi wanaitwa gusa unate ,ukionja tu mara moja ubanduki kuna vibabu vina dawa hatari tena vibabu vya huko siyo vitapeli ni vya uhakika kama vya kwa msisi
 
Habari za Leo wanajukwaa, kama heading inavyosema, natamani kupata highlights za maisha katika mji wa Same mkoani Kilimanjaro. Nimepata uhamisho kwenda Same, so naomba kujuzwa hali ya maisha hapo Same, fursa zilizopo na information yoyote kuhusu Same unayoona ni muhimu. Ahsanteni sana

Fursa kubwa za huko Same ni kujitahidi tu kuepuka UKIMWI Mkuu.
 
Fuata kilichokupeleka, waheshimu wenyeji nao watakuheshimu ukilete mikwara watakunyoosha. Ningekupa mifano lakini itaathiri wahusika maana bado wapo.
Sema tu ukweli kwamba ukiingia kwenye 18 za watu hawakuachi,kuoteshwa kitu mgongoni ni ishu ndogo
 
Unachotakiwa kujua ni kuwa Same km ilivyo kwa wilaya nyingi za Mikoani fursa zake ziko vijijini, kinachotakiwa ni wewe kufanya survey ukifika huko. Hiyo nchi ina madini mengi sana ukijichanganya na wadau unatoka vizuri. Pia kuna fursa za utalii wana mbuga ya Mkomaz National Park, pia culture tourism iko sana hapo. Kuna ufugaji na kilimo cha mpunga,tangawizi na mazao mengine. Mambo ya wanawake au wanaume hayo kila mahali yapo hivyo ni discipline yako uliyolelewa nayo huko utokako.
 
Hata ukitaka kufanya kilimo utafanikiwa sana,watu wengi hawajui kuwa same ni moja ya wilaya za tanzania zenye maji mengi sana.lazima itakuwepo kwnye tano bora.kalime kitunguu,mpunga ama tangawizi.kazi ni kwako.ukiwa unapenda vimwana kama mimi hapo ndo umefika
 
Fafanua,mi najua maeneo ya masandare kuna walozi wengi sana,pia wanawake wengi wa same hawajui kusema no, ni enzi hizo za 1999 nilikuwa pande hizo lakini sijui sasa hali ikoje
Masandare tumepigga miti wake za watu mitaa hiyo...Pia maeneo ya Stesheni kama unaelekea mjini kuna mother alikuwa mjane basi nikawa nampa TULIZO kiaina. LODGE ilikwa GHETTO kwake. Mimi MSINGI KIUNO tu
 
dah mimi nilipitiliza tu mpaka kule kisiwani...
 
Pakame sana pale. Nilikaa miezi miwili lkn hali ya hewa ni nzuri japo kuna vumbi sana. Usiku ni baridi ya upepo, vyakula sio shida sana ila maji ilikuwa ishu wakati huo. Sijui sasa hivi.
 
Back
Top Bottom