Chizi Fureshi
JF-Expert Member
- Oct 26, 2010
- 1,718
- 462
Kanisa gani jamaa yangu!
Kanisa gani jamaa yangu!
tendo la ndoa navyojua ni kukutana kimwili kwa watu walio oana.
Ninavyojua Biblia inasema kijana atawaacha wazazi wake na ataambatana na mkewe nao watakua mwili mmoja,je ni wapi Biblia inasema lazma ukafunge ndoa kanisani?je km mm nimependana na bint,tumekubaliana na tunaishi pamoja kwa upendo na amani bila kufunga ndoa kuna dhambi yoyote hapo?mi naomba kujua ni wap biblia inataka tukafunge ndoa kanisani?msing wa hyo dhana unatoka wap?naomba nielimishwe.
Wewe ni mkristu kweli maana sikutegemea ungeuliza swali kama hilo. Hata kama kwenye biblia haijaandikwa lakini ndoa ni sakramenti kama ilivyo ubatizo, upadri, ekaristi n.k na hivyo kuna utaratibu wa utoaji wa sakramenti yoyote ile. Kuchukuana na kuanza kuishi siyo ndoa bali unataka kuhalalisha uasherati na kwa amri za Mungu unavunja amri ya sita.
Mkuu naona watu wanakurushia tuhuma na mameno mengi lakini swali lako ni la msingi na nna amini hata baadhi ya wakristo wengi hawana jibu licha ya kutaka lipuuzwe.
Sina mstari wa moja kwa moja unaohusu sherehe ya harusi au jinsi gani ifanyike licha ya ukweli kwamba Biblia imejaa mistari inayoelezea umuhimu wa ndoa tangu mwanzo.
Inategemea unaongelea dhehebu gani, kwa sababu licha ya kwamba ndoa inafungwa kanisani lakini kile cheti kinatoka serikalini.
Na kuna taratibu zake kama vile tangazo litoke siku ngapi kabla ya siku ya harusi.
Kwa ufupi niseme, kila dhehebu wamekuja na utaratibu wao (Mapokeo) ya jinsi wanavyotaka waumini wao waishi kutokana na misingi ya hilo dhehebu. Ndio maana kuna wengine wanabatiza kwa maji mengi, wengine wanabatiza watoto, wengine wanaabudu siku ya Jumapili na wengine siku ya Jumamosi n.k
Kama wewe ni mkristo na uko kwenye mojawapo ya makanisa ya kikristo, ni lazima ukubaliane na utaratibu waliojiwekea.