Robot la Matope
JF-Expert Member
- Apr 10, 2015
- 7,091
- 13,790
Hili ni swali ambalo nimeulizwa na watu wengi sana huku wakitaka kujua, ni sababu zipi zinazomfanya Padre ashindwe kutoa sadaka Kanisani kama wanavyofanya Waamini wengine?
Maana wakati wa adhimisho la Misa Takatifu, mara nyingi tunamsikia Padre akisema: "๐๐๐ฅ๐ข๐ง๐ข ๐ง๐๐ฎ๐ ๐ฎ ๐ข๐ฅ๐ข ๐ฌ๐๐๐๐ค๐ ๐ฒ๐๐ง๐ ๐ฎ ๐ง๐ ๐ฒ๐๐ง๐ฎ ๐ข๐ค๐ฎ๐๐๐ฅ๐ข๐ฐ๐ ๐ง๐ ๐๐ฎ๐ง๐ ๐ฎ ๐ฆ๐ฐ๐๐ง๐ฒ๐๐ณ๐ข".
๐๐๐๐๐: Sasa sadaka anayoitoa Padre hapo ni ipi wakati hatuioni?
๐๐๐๐: Ni kweli kabisa kwa macho ya kawaida, ni vigumu kuiona sadaka anayoitoa Padre altareni kama vile wanavyofanya Waamini wengine, lakini nikuambie kwamba, sadaka ya Padre ni kubwa zaidi kuliko ya mtu yoyote yule.
Ngoja nikuulize swali: Hivi ushawahi kujiuliza kwanini wakati wa utoaji wa sakramenti ya daraja takatifu, Mapadre huwa wanalala chini kifudifudi huku akisaliwa sala maalumu pamoja na litania ya Watakatifu kabla hajawekwa wakfu na Askofu kwa kupakwa mafuta kwenye viganja vyake mikono na kuvalishwa rasmi mavazi ya kikuhani?
Hakika wengi wanadhani kitendo hicho cha kulala kifudifudi kwa Padre, basi anaweka nadhiri za utii kwa Askofu na kumuahidia kuishi maisha ya usafi wa moyo bila kufunga ndoa, ili aweze kumtumikia Mungu kwa uhuru zaidi.
Niseme tu kwamba, hayo yote yanaweza kuwa majibu ila sio kwa mantiki hiyo ya kulala kifudifudi. Kwani kitendo cha Padre kulala kifudifudi, inaashiria kujitoa sadaka kwa ajili ya kuutangaza Ufalme wa Mungu na kuufia ulimwengu kama Yesu alivyofanya.
Kwa sababu hiyo katika hatari yoyote ile ya kifo, ni rahisi sana kumuona Padre akiwa yuko radhi kutoa maisha yake kwa ajili ya Mungu na Kanisa ili kutetea imani iliyoachwa tangu zamani na Mitume wa Yesu.
Kadhalika ukiachana na sababu hiyo, pia hata maisha yake kwa ujumla ni sadaka tosha. Maana wakati wewe unalala usiku, Padre hutumia muda huo kuwaombea watu, yuko tayari kuacha chakula chake ili kumuwahi mgonjwa anayekaribia kufa na kumpa Sakramenti ya Upako. Wakati wote anashinda Kanisani ili kusikiliza shida za watu na kuwasaidia, daima aachi kutoa Sakramenti ya Kitubio hata kama afya yake haiko vizuri siku hiyo.
Maisha ya Padre kwa nje unaweza kuona ni mepesi, ila ukweli ni magumu sana, bila sala na moyo wa majitoleo huwezi. Kwa sababu kokote pale Padre akihitajika huwa anafika kwa wakati licha ya kuwa na kazi nyingi. Tena muda mwingine kwenye msiba utamkuta Padre anahuzunika na wale waliofiwa hata kama msiba huo haumuhusu, na wakati wa harusi hufurahi pamoja na wale waliofunga ndoa. Kwangu hiyo ni sadaka, sasa sijui muuliza swali alikuwa anataka sadaka ipi?
Maana Padre hawezi kutoa sadaka ya pesa, mazao au mnyama wa aina yoyote yule kama Wakristo wengine wanavyotoa. Ukweli nikuambie tu kuwa, muda mrefu Padre kashajisadaka tayari mwili na roho yake kwa lengo la kumtumikia Mungu na Kanisa. Na ndio sababu nasema, sadaka ya Padre ni kubwa zaidi kuliko zile tunazozitoa sisi kila siku.
Pia hata tukisema leo hii sheria ipitishwe rasmi, eti Padre naye atoe sadaka sawa na Waamini wengine. Je unafikiri sadaka hiyo Padre ataitoa wapi, wakati hana kazi wala kitega uchumi chochote kitachomuwezesha kufanya hayo yote?
Nadhani hapo ndio mwanzo wa Kanisa kuingia katika migogoro, kisa tu Padre ameanza tabia ya kuiba sadaka za watu ili apate pesa za kutoa Kanisani. Suala hili sio nzuri na halifai kabisa.
Kwani ukisoma vema Biblia, utakutana na kisa cha makabila 12 ya Waisraeli, ambayo makabila hayo yote yalipewa urithi katika sehemu yake ila kasoro kabila moja tu la Walawi, maana urithi wao ulikuwa kwa Bwana pekee na walipewa kibali cha kutumia sadaka zote zilizotolewa na Waisraeli wa wakati ule Hekaluni. (๐๐ฐ๐๐ง๐ณ๐จ 14:17-20).
Biblia inatuambia kabila hilo la Walawi ndilo lililowekwa wakfu kwa lengo la kutoa Makuhani kwa kazi ya Mungu tu, utaratibu ambao unatumika hadi sasa kwa Mapadre wetu. (๐๐๐ฅ๐๐ฐ๐ข 22:1-33).
Kwahiyo nihitimishe kwa kusema kwamba, sote kama wanadamu tuna wajibu wa kutoa sadaka ingawa sadaka zetu zinatofautiana kidogo. Maana Padre hutoa sadaka yake ya mwili na roho kwa ajili ya Kanisa, na sisi basi tutoe sadaka za pesa na mali tulizonazo kwa ajili ya kujiombea wenyewe baraka na wale wote wanaotuzunguka.
๐๐๐๐๐๐ ๐ ๐๐๐๐ ๐๐๐๐๐๐
Maana wakati wa adhimisho la Misa Takatifu, mara nyingi tunamsikia Padre akisema: "๐๐๐ฅ๐ข๐ง๐ข ๐ง๐๐ฎ๐ ๐ฎ ๐ข๐ฅ๐ข ๐ฌ๐๐๐๐ค๐ ๐ฒ๐๐ง๐ ๐ฎ ๐ง๐ ๐ฒ๐๐ง๐ฎ ๐ข๐ค๐ฎ๐๐๐ฅ๐ข๐ฐ๐ ๐ง๐ ๐๐ฎ๐ง๐ ๐ฎ ๐ฆ๐ฐ๐๐ง๐ฒ๐๐ณ๐ข".
๐๐๐๐๐: Sasa sadaka anayoitoa Padre hapo ni ipi wakati hatuioni?
๐๐๐๐: Ni kweli kabisa kwa macho ya kawaida, ni vigumu kuiona sadaka anayoitoa Padre altareni kama vile wanavyofanya Waamini wengine, lakini nikuambie kwamba, sadaka ya Padre ni kubwa zaidi kuliko ya mtu yoyote yule.
Ngoja nikuulize swali: Hivi ushawahi kujiuliza kwanini wakati wa utoaji wa sakramenti ya daraja takatifu, Mapadre huwa wanalala chini kifudifudi huku akisaliwa sala maalumu pamoja na litania ya Watakatifu kabla hajawekwa wakfu na Askofu kwa kupakwa mafuta kwenye viganja vyake mikono na kuvalishwa rasmi mavazi ya kikuhani?
Hakika wengi wanadhani kitendo hicho cha kulala kifudifudi kwa Padre, basi anaweka nadhiri za utii kwa Askofu na kumuahidia kuishi maisha ya usafi wa moyo bila kufunga ndoa, ili aweze kumtumikia Mungu kwa uhuru zaidi.
Niseme tu kwamba, hayo yote yanaweza kuwa majibu ila sio kwa mantiki hiyo ya kulala kifudifudi. Kwani kitendo cha Padre kulala kifudifudi, inaashiria kujitoa sadaka kwa ajili ya kuutangaza Ufalme wa Mungu na kuufia ulimwengu kama Yesu alivyofanya.
Kwa sababu hiyo katika hatari yoyote ile ya kifo, ni rahisi sana kumuona Padre akiwa yuko radhi kutoa maisha yake kwa ajili ya Mungu na Kanisa ili kutetea imani iliyoachwa tangu zamani na Mitume wa Yesu.
Kadhalika ukiachana na sababu hiyo, pia hata maisha yake kwa ujumla ni sadaka tosha. Maana wakati wewe unalala usiku, Padre hutumia muda huo kuwaombea watu, yuko tayari kuacha chakula chake ili kumuwahi mgonjwa anayekaribia kufa na kumpa Sakramenti ya Upako. Wakati wote anashinda Kanisani ili kusikiliza shida za watu na kuwasaidia, daima aachi kutoa Sakramenti ya Kitubio hata kama afya yake haiko vizuri siku hiyo.
Maisha ya Padre kwa nje unaweza kuona ni mepesi, ila ukweli ni magumu sana, bila sala na moyo wa majitoleo huwezi. Kwa sababu kokote pale Padre akihitajika huwa anafika kwa wakati licha ya kuwa na kazi nyingi. Tena muda mwingine kwenye msiba utamkuta Padre anahuzunika na wale waliofiwa hata kama msiba huo haumuhusu, na wakati wa harusi hufurahi pamoja na wale waliofunga ndoa. Kwangu hiyo ni sadaka, sasa sijui muuliza swali alikuwa anataka sadaka ipi?
Maana Padre hawezi kutoa sadaka ya pesa, mazao au mnyama wa aina yoyote yule kama Wakristo wengine wanavyotoa. Ukweli nikuambie tu kuwa, muda mrefu Padre kashajisadaka tayari mwili na roho yake kwa lengo la kumtumikia Mungu na Kanisa. Na ndio sababu nasema, sadaka ya Padre ni kubwa zaidi kuliko zile tunazozitoa sisi kila siku.
Pia hata tukisema leo hii sheria ipitishwe rasmi, eti Padre naye atoe sadaka sawa na Waamini wengine. Je unafikiri sadaka hiyo Padre ataitoa wapi, wakati hana kazi wala kitega uchumi chochote kitachomuwezesha kufanya hayo yote?
Nadhani hapo ndio mwanzo wa Kanisa kuingia katika migogoro, kisa tu Padre ameanza tabia ya kuiba sadaka za watu ili apate pesa za kutoa Kanisani. Suala hili sio nzuri na halifai kabisa.
Kwani ukisoma vema Biblia, utakutana na kisa cha makabila 12 ya Waisraeli, ambayo makabila hayo yote yalipewa urithi katika sehemu yake ila kasoro kabila moja tu la Walawi, maana urithi wao ulikuwa kwa Bwana pekee na walipewa kibali cha kutumia sadaka zote zilizotolewa na Waisraeli wa wakati ule Hekaluni. (๐๐ฐ๐๐ง๐ณ๐จ 14:17-20).
Biblia inatuambia kabila hilo la Walawi ndilo lililowekwa wakfu kwa lengo la kutoa Makuhani kwa kazi ya Mungu tu, utaratibu ambao unatumika hadi sasa kwa Mapadre wetu. (๐๐๐ฅ๐๐ฐ๐ข 22:1-33).
Kwahiyo nihitimishe kwa kusema kwamba, sote kama wanadamu tuna wajibu wa kutoa sadaka ingawa sadaka zetu zinatofautiana kidogo. Maana Padre hutoa sadaka yake ya mwili na roho kwa ajili ya Kanisa, na sisi basi tutoe sadaka za pesa na mali tulizonazo kwa ajili ya kujiombea wenyewe baraka na wale wote wanaotuzunguka.
๐๐๐๐๐๐ ๐ ๐๐๐๐ ๐๐๐๐๐๐