GoldDhahabu
JF-Expert Member
- Apr 29, 2023
- 4,695
- 6,398
Wiki ijayo ninatarajia kwenda Mombasa nchini Kenya. Nipo Mwanza, na nitavukia mpaka wa Sirari. Naombeni mwongozo kwa wenyeji na wazoefu:
1. Ni muda gani mzur kusafiri kutoka Sirari kwenda Mombasa? Najua Kenya kuna usafiri masaa 24 kwa siku.
2. Kuna gari la moja kwa moja kutoka Sirari hadi Mombasa?
3. Nauli ni shilingi ngapi Sirari hadi Mombasa?
4. Lodge gani nzuri lakini ya bei nafuu Mombasa? Kipaumbele cha kwanza ni usalama.
Bei ya lodge/gesti ni shilingi ngapi?
5. Shughuli inayonipeleka Mombasa inaweza ikanichukua siku mbili kuikamikisha. Baada ya hapo, nitarejea Tz.
Ninafikiria kurudi kwa kuzungukia Kampala, kama gharama haitakuwa kubwa sana. Inaweza ikanigharimu shilingi ngapi kutoka Mombasa hadi Mutukula kwa kupitia Kampala? Kuna changamoto yoyote kwenye mpaka wa Kenya kwenda Uganda (sijawahi kuingia Uganda kupitia Kenya).
Ni magari gani yanayoenda Kampala/ Mutukula kutokea Mombasa Kenya?
Naomba kuwasilisha🙏
1. Ni muda gani mzur kusafiri kutoka Sirari kwenda Mombasa? Najua Kenya kuna usafiri masaa 24 kwa siku.
2. Kuna gari la moja kwa moja kutoka Sirari hadi Mombasa?
3. Nauli ni shilingi ngapi Sirari hadi Mombasa?
4. Lodge gani nzuri lakini ya bei nafuu Mombasa? Kipaumbele cha kwanza ni usalama.
Bei ya lodge/gesti ni shilingi ngapi?
5. Shughuli inayonipeleka Mombasa inaweza ikanichukua siku mbili kuikamikisha. Baada ya hapo, nitarejea Tz.
Ninafikiria kurudi kwa kuzungukia Kampala, kama gharama haitakuwa kubwa sana. Inaweza ikanigharimu shilingi ngapi kutoka Mombasa hadi Mutukula kwa kupitia Kampala? Kuna changamoto yoyote kwenye mpaka wa Kenya kwenda Uganda (sijawahi kuingia Uganda kupitia Kenya).
Ni magari gani yanayoenda Kampala/ Mutukula kutokea Mombasa Kenya?
Naomba kuwasilisha🙏