Naomba ifanywe kwa dharura: Napendekeza kuanzia Jumamosi iwe ni marufuku mtu kutoka nje ya nyumba yake bila kufunika uso kwa kitambaa/ barakoa/ scarf

Napendekeza katika hali ya dharura sana, serikali itangaze kuanzia jumamosi hii iwe ni marufuku kwa mtu yeyote kutoka nje ya nyumba yake bila kufunika uso kwa kitambaa au scarf, na kama ana uwezo wa kununua barakoa basi avae barakoa.

Japo barakoa/ scarf haikukingi moja kwa moja na maambukizi kwa sababu bado macho yapo wazi, lakini inasaidia kuwalinda wanaokuzunguka pale unapokohoa au kupiga chafya, shida inayokuja sasa hivi ni kwamba mtu kwa nia njema kabisa unapotaka kuvaa barakoa watu wanakushangaa na kukugeuza kituko.

Its very unnerving, ndio maana wengi tumeacha kuvaa hizo barakoa, ila Serikali ikitangaza kwamba ni lazima basi kila mtu atavaa na hakutakuwa na wa kumshangaa au kumgeuza mwenzie kituko /kivutio cha utalii na kumshangaa shangaa anapopita.

Natoa masaa 12 tu hili lifanyike. NB: Sitaongeza muda.
Utawanunulia?
 
Chupi mimi ndio niliwanunulia?
Vijana wengi ambao mnaishi kwa mashemeji zenu mnatengenezewa juice kula bure mnajifanya kuona maisha maraisi sana, hujui kuwa watu wanashindwa hata kulipa nauli ya daladala wanatembea kwa miguu, ukiwaongezea gharama za hizo barakoa maana yake wafie ndani siyo, hata huko kwa wataalam USA walilipiga suala la kulazimsha watu kuvaa, suala ni kuchukua tahadhari,
 
Vijana wengi ambao mnaishi kwa mashemeji zenu mnatengenezewa juice kula bure mnajifanya kuona maisha maraisi sana, hujui kuwa watu wanashindwa hata kulipa nauli ya daladala wanatembea kwa miguu, ukiwaongezea gharama za hizo barakoa maana yake wafie ndani siyo, hata huko kwa wataalam USA walilipiga suala la kulazimsha watu kuvaa, suala ni kuchukua tahadhari,
Acha kukariri takataka wewe, shemeji shemeji, shemeji ndio upuuzi gani, umeambiwa vaa barakoa unaanza kuleta ngonjera ndeeefu.., hopeless..! Na barakoa hata ya kitambaa inasaidia sana
 
Acha kukariri takataka wewe, shemeji shemeji, shemeji ndio upuuzi gani, umeambiwa vaa barakoa unaanza kuleta ngonjera ndeeefu.., hopeless..!
Kula kulala unanyamba kwenye sofa za shemeji yako unajitia mjuaji huna jipya, tafuta pesa uone isivyopatikana hovyo
 
Kula kulala unanyamba kwenye sofa za shemeji yako unajitia mjuaji huna jipya, tafuta pesa uone isivyopatikana hovyo
Unaongea upuuuzi, shemeji ndio nini wewe.., hatuko hapa kutambiana nani anaingiza kiasi gani, hata nikikuambia haikusaidii kujua mimi au wewe unajamba kwa shemeji yako au la, point is vaa kitambaa, scarf, au kama shemeji yako yupo vizuri, akupe pesa ukanunue barakoa speacial, thats the point
 
Hii serikali inaleta ubishi usio na tija, subiri sasa, mtake msitake lazima mtatangaza hii amri, sirudi nyuma.
 
Nakuunga mkono.
Serikali imechelewa na inachelewa sana kutoa tamko la kujikinga zaidi ya kunawa mikono.

Watu wote tungeanza mapema kukinga midomo na pua ingesaidia kupunguza maambukizi kwa njia ya chafya na kukohoa.

Unakuta basi zima hakuna hata MTU mmoja aliyefunika USO. Watu wanaingia msikitini na kusujudi bila kuvaa maski wakati anapogusa ardhini ndipo mwngine alipogusa dk chache zilizopita.

Pia watu wanunue gloves wavae kwani zinafaa kuosha kwa sabuni na kuvaliwa tena na tena. Mana sio kwamba zinatumika hospitalini Bali ni kugusa vitu na kisha zinaoshwa na sabuni kisha MTU asiye na uwezo anavaa tena kuliko kuuza vitu sokono mikono mitupu na mdomo na pua wazi.

Watoa huduma wote wavae maski kwa kweli mana huenda bidhaa wanazouzia watu wanazipigia Chafya au kukoholea halafu wateja wananunua.

Wauza vyakula na vinywaji nao wavae maski na mikononi wavae gloves.

Sent using Jamii Forums mobile app
Ushauri mzr

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Vijana wengi ambao mnaishi kwa mashemeji zenu mnatengenezewa juice kula bure mnajifanya kuona maisha maraisi sana, hujui kuwa watu wanashindwa hata kulipa nauli ya daladala wanatembea kwa miguu, ukiwaongezea gharama za hizo barakoa maana yake wafie ndani siyo, hata huko kwa wataalam USA walilipiga suala la kulazimsha watu kuvaa, suala ni kuchukua tahadhari,
Hopeless!
 
Asitoke wala asiingie mtu ndani ya jiji hili kwa muda wa siku 15, kwa kufanya hivi tutajiepusha na madhara makubwa sana yanayoweza kuwakumba mababu na mabibi zetu huko mikoani.
Magari ya mizigo tu ndio yaruhusiwe kupita, tudeal na huu ugonjwa humu humu mpaka tuukomeshe kabisa, ni rahisi zaidi kuliko ukisambaa huko mikoani, tutakuja kulaumiana sana hapo baadae, ni ngumu kuamini, ila RC ndio kashikilia uhai wa WaTanzania milioni 60 kwa sasa, yeye ndiye ataamua tufe au tuishi.
Na hapa ndio tunaona umuhimu wa kushiriki katika siasa, tusikubali watu wachache wakahodhi madaraka yote, ni hatari sana!
 
Back
Top Bottom