EasyFit
JF-Expert Member
- Jul 4, 2011
- 1,269
- 1,082
Nakubaliana na wewe kabisa lakini matumizi ya neno pambana na hamasisha/elimisha hutegemea sehemu na aina ya kazi husika. Mazingira ya wakati huo yanaweza kabisa kubadili maana na matumizi ya maneno hayo.Mimi nafikiri tungebadilisha lugha, badala ya kusema mapambano. Tusema uhamasishaji na uelimishaji wa wananchi. Mapambano limekaa kimgomomgo/kunji/maandamano. We should find a good name on this.. Ningeshauri tupunguze kutumia nguvu kupita kiasi, jazba na hasira badala yake tuelimishe umma kujua haki zake and maove yanayoendelea ili kufanya uamuzi mzuri wa kuwapata viongozi waadilifu wa nchi hii iliyobarikiwa.
Ukikutana na Simba polini huwezi kusema unaelimisha ni lazima upambane, rushwa imefikia stage ya ufisadi ni sawa na mnyama ni kupambana nayo kwanza baadae tutawaelimisha wananchi, CCM ilipofikia si ya kuelimisha eti kuachana na ufisadi au kuelimishwa kuachia madaraka ni kupambana nayo vinginevyo utakesha na hawatakuelewa.
Mimi nashauri twende navyo vyote pamoja wakati tunaelimisha tunapambana vile vile.