GENTAMYCINE
JF-Expert Member
- Jul 13, 2013
- 56,694
- 109,128
Tena kwa taarifa yenu sasa ni kwamba kama kuna mechi ngumu kwa Taifa Stars na ambayo tukijiandaa nayo sana tutafungwa Goli chache sana 3 ila tukifanya maandalizi ya zima moto kuna hatari ya Kubugizwa / Kufungwa kati ya Goli 7 au 9 Uwanja wa Taifa mwakani mwezi Machi.
Yaani kabisa Uganda Cranes wachafue rekodi yao ya kutokufungwa eti waiachie au wafungwe na Taifa Stars yetu tena hii hii ya Mabeki ' wabovu ' na ' washamba ' akina Ally Sonso na Abdallah Kheri? Labda siyo Uganda Cranes ninayoijua Mimi.
Na hapa wala tusidanganyane na najua ukweli huu utakuwa ni mchungu Kwenu ila kwa wenye akili sawasawa na wanaoujua mpira vyema ni kwamba Safari yetu ya kwenda AFCON nchini Cameroon mwakani imehitimishwa / imezikwa rasmi leo pale Jijini Maseru nchini Lesotho.
Nimewasikia Watangazaji ' Wanafiki ' wa Redio za Tanzania wakijifanya kuwapa moyo Watanzania kuwa eti bado tuna nafasi ila GENTAMYCINE a.k.a Mzee wa Kunyoosha na Kunyooka daima nasema hapa hapa na leo hii hii kuwa tujipange kwa Michuano ya AFCON na mwaka 2021 na tuwekeze nguvu sasa kwa Timu ya Vijana labda huko tunaweza tukabahatisha kwa michuano ya karibuni japo na kwenyewe pia nimeshaanza kuona tatizo hasa kwa upande wa Wachezaji wake ambao kwa sasa na Wao wameshaanza kuwa na Majipu / Maringo na kujiona kuwa tayari nao wamefanikiwa Kimpira wakati ukweli ni kwamba bado hawajui lolote na wanatakiwa kuendelea Kujifunza na Kukomaa zaidi.
Ushindi wa Taifa Stars kwa Uganda Cranes mwezi Machi mwakani ni sare ( draw ) pekee ila siyo kuwafunga na hapa naweza hata kusema bila Kupepesa macho, Kumung'unya maneno wala Kutikisa masikio kwa baada ya matokeo ya Kufungwa na Lesotho kwa Taifa Stars nawaona kabisa Cape Verde ambao hapo awali tulikuwa tunawacheka kuwa wanaenda Kupindua Meza na Wao sasa ndiyo wataungana na Uganda katika Kundi letu na Kufuzu kwenda AFCON mwakani huko Cameroon.
Taifa Stars ikitoka Sare na Uganda Cranes halafu Cape Verde akamfunga Lesotho Kwake Jijini Praia atakuwa na alama Saba ( 7 ) huku Sisi tukiwa na alama zetu Sita ( 6 ) hivyo tutabaki Kuendelea na Ligi yetu hii mbovu ya Mafarasi wakubwa Watatu tu huku wengine wakilia njaa tu na hata Timu zao Kukosa nauli.
Kocha mwenye akili timamu kabisa hawezi kumuacha nje Tanzania Midfield Maestro kwa sasa Jonas Gerald Mkude na kumpanga Himid Mao Mkami ambaye sijawahi Kumkubali na sitokuja Kumkubali kwani hajui mpira bali anabahatisha tu. Utamwekaje nje Faisal Toto halafu kuwaingiza Watu kama akina John Boko na Shiza Kichuya dakika za mwisho kabisa? Hivi huyu Kocha wenu / wetu Amunike anavuta Bange / Bangi au?
Tumevuna tulichopanda na namuomba Rais Mstaafu wa Awamu ya Pili Mzee Ally Hassan Mwinyi atuongezee neno lingine baada ya lile la ' laana ' alilotuachia kuwa Sisi daima tutaendelea tu kuwa Kichwa cha Mwendawazimu kwani kwa Upomboyo / Upuuzi uliopo tunastahili kupewa kila aina ya majina na laana.
Nawasilisha.
Yaani kabisa Uganda Cranes wachafue rekodi yao ya kutokufungwa eti waiachie au wafungwe na Taifa Stars yetu tena hii hii ya Mabeki ' wabovu ' na ' washamba ' akina Ally Sonso na Abdallah Kheri? Labda siyo Uganda Cranes ninayoijua Mimi.
Na hapa wala tusidanganyane na najua ukweli huu utakuwa ni mchungu Kwenu ila kwa wenye akili sawasawa na wanaoujua mpira vyema ni kwamba Safari yetu ya kwenda AFCON nchini Cameroon mwakani imehitimishwa / imezikwa rasmi leo pale Jijini Maseru nchini Lesotho.
Nimewasikia Watangazaji ' Wanafiki ' wa Redio za Tanzania wakijifanya kuwapa moyo Watanzania kuwa eti bado tuna nafasi ila GENTAMYCINE a.k.a Mzee wa Kunyoosha na Kunyooka daima nasema hapa hapa na leo hii hii kuwa tujipange kwa Michuano ya AFCON na mwaka 2021 na tuwekeze nguvu sasa kwa Timu ya Vijana labda huko tunaweza tukabahatisha kwa michuano ya karibuni japo na kwenyewe pia nimeshaanza kuona tatizo hasa kwa upande wa Wachezaji wake ambao kwa sasa na Wao wameshaanza kuwa na Majipu / Maringo na kujiona kuwa tayari nao wamefanikiwa Kimpira wakati ukweli ni kwamba bado hawajui lolote na wanatakiwa kuendelea Kujifunza na Kukomaa zaidi.
Ushindi wa Taifa Stars kwa Uganda Cranes mwezi Machi mwakani ni sare ( draw ) pekee ila siyo kuwafunga na hapa naweza hata kusema bila Kupepesa macho, Kumung'unya maneno wala Kutikisa masikio kwa baada ya matokeo ya Kufungwa na Lesotho kwa Taifa Stars nawaona kabisa Cape Verde ambao hapo awali tulikuwa tunawacheka kuwa wanaenda Kupindua Meza na Wao sasa ndiyo wataungana na Uganda katika Kundi letu na Kufuzu kwenda AFCON mwakani huko Cameroon.
Taifa Stars ikitoka Sare na Uganda Cranes halafu Cape Verde akamfunga Lesotho Kwake Jijini Praia atakuwa na alama Saba ( 7 ) huku Sisi tukiwa na alama zetu Sita ( 6 ) hivyo tutabaki Kuendelea na Ligi yetu hii mbovu ya Mafarasi wakubwa Watatu tu huku wengine wakilia njaa tu na hata Timu zao Kukosa nauli.
Kocha mwenye akili timamu kabisa hawezi kumuacha nje Tanzania Midfield Maestro kwa sasa Jonas Gerald Mkude na kumpanga Himid Mao Mkami ambaye sijawahi Kumkubali na sitokuja Kumkubali kwani hajui mpira bali anabahatisha tu. Utamwekaje nje Faisal Toto halafu kuwaingiza Watu kama akina John Boko na Shiza Kichuya dakika za mwisho kabisa? Hivi huyu Kocha wenu / wetu Amunike anavuta Bange / Bangi au?
Tumevuna tulichopanda na namuomba Rais Mstaafu wa Awamu ya Pili Mzee Ally Hassan Mwinyi atuongezee neno lingine baada ya lile la ' laana ' alilotuachia kuwa Sisi daima tutaendelea tu kuwa Kichwa cha Mwendawazimu kwani kwa Upomboyo / Upuuzi uliopo tunastahili kupewa kila aina ya majina na laana.
Nawasilisha.