Chief Masanja
Member
- Feb 6, 2007
- 31
- 1
habari za leo wajukuu zangu?
ni kwa kipindi kirefu kweli nimeshuhudia huu mjadala juu ya huyu kijana mwenzenu! kama ilivyo ada yangu, leo nimeamua nijitokeze tena; pamoja na mambo mengine mengi ambayo yametokea hapa karibuni na mwaka huu mpya leo nataka nieleze kwa ufupi juu ya huyu kijana na jinsi ninavyo mjua mimi.........
RIDHIWANI KIKWETE,kama wengin wanavyomjua alizaliwa katika hospital ya wilaya ya bagamoyo tarehe 16 mwezi wa NNE mwaka 1979. kijana huyu alizaliwa toka kwa mama AZIZA bint SABURI na baba JAKAYA MRISHO KIKWETE.
RIDHIWANI ni kijana wa kwanza kwa wazazi hawa na alifuatiwa na mdogo wake anayejulikana kwa jina la SALAMA ambaye kwa sasa ni daktari na mwalimu pale MUHIMBILI chuoni.
kijana huyu alianza shule ya msingi mwaka 1987 pale shule ya msingi MATANGINI,nachingwea mkoa wa LINDI.sababu kubwa za yeye kuanza shule huko ni kazi aliyokuwa akifanya baba yake kipindi hicho. ikumbukwe kuwa bwana Kikwete alikuwa katibu wa CCM ,wilayani hapo. mwaka mmoja baadae, bwana ridhiwani na baba yake waliamia MASASI,mkoa wa MTWARA.akiwa huko alijiunga na shule ya MKOMAINDO kwa masomo yake ya darasa la pili kabla hawajarudi DAR ES SAALAAM, mwaka1989 ambapo alijiunga na shule ya FORODHANI iliyopo maeneo ya posta ya zamani hadi alipomaliza darasa la saba.
masomo ya sekondari aliyapata katika shule ya SHAABAN ROBERT na baadae MKWAWA mkoani IRINGA kabla ya kurudi DAR ES SALAAAM kwa ajili ya elimu ya juu katika CHUO KIKUUU CHA DAR ES SALAAM, sehemu ya mlimani na baadae ENGLAND,kwa masomo ya cheti cha elimu ya juu.
KISIASA
kisiasa kijana huyu alianza akiwa mdogo sana.historia inaanza akiwa nyumbani kwao na babu yake pale bagamoyo, ambapo alishiriki katika shughuli za kucheza gwaride kama chipukizi wa chama na hata alipokwenda huko NCHINGWEA NA MASASI aliendelea na shughuli za kucheza gwaride la chipukizi wa chama cha mapinduzi.
mwaka 1992, alikuwa ni mmoja kati ya vijana walioshiriki kama wajumbe kwenye mkutano mkuu wa chipukizi wa ccm taifa uliofanyika mbeya ambao ulimchagua bwana RAYMOND MANGWALE kuwa mwenyekiti wa jumuiya hiyo taifa. ( ikumbukwe bwana RAYMOND ni katibu wa UV-CCM, mkoa wa DODOMA ,kwa sasa). hata hivyo pia, wakati wa enzi hizo za masomo ya shule ya msingi, ridhiwani atakumbukwa kama kijana aliyechangia hela nyingi kwenye mradi wa mabasi ya UV-CCM na hata kupeWa nishani na RAISI mstaafu wa AWAMU YA PILI, ALHAJI ALLY HASSAN MWINYI katika viwanja vya KARIMJEE sherehe ambazo zilihudhuriwa na wageni mbalimbali wakiwemo mabalozi wa nchi mbalimbali na viopngozi wa serikali.
wakati yupo sekondari aliendelea kuwa mwana harakati wa kawaida pale shuleni DAR ES SALAAM na hata baadae IRINGA.Waliosoma naye iringa wanakumbuka pilika zake na wenzake katika siasa za wanafunzi ,na michezoni.alikuwa mcheza mpira mzur sana enzi hizo.sijui siku hizi kama anacheza au bado.kumbukumbu zinaonyesha ushiriki wake katika kampeni za kufanikisha wenzake kupata nafasi za uongozi.
wakati akiwa chuoni, alikuwa mstari wa mbele katika siasa za DARUSO. RIDHIWANI amewahi kuwa katibu wa serikali ya wanafunzi, WIZARA YA MAMBO YA NJE NA WANAFUNZI WANAOTOKA NCHI ZA NJE, na baadae alikuwa MBUNGE MWAKILISHI TOKA KITIVO CHA WANAFUNZI WA SHERIA, kabla hajawa MWENYEKITI WA DARUSO-KITIVO CHA SHERIA.
katika kipindi hiki tumeona alivyokuwa akishiriki katia siasa za wanafunzi na hata kushirikiana na wenzake kuhakikisha kuwa yale mambo wanayoyataka katika mazingira ya chuoni hapo yanakuwa vizuri.
Wakati yupo chuoni, akiwa mwaka wa tatu, 2002 aliteuliwa kuwa MUHAMASISHAJI WA UVCCM-wilaya ya BAGAMOYO.ikumbukwe kipindi hiki ni kipindi bwana SAIDI MTANDA ambaye kwa sasa ni MBUNGE WA JIMBO LA MCHINGA,LINDI alikuwa ndiyo MWENYEKITI WA UVCCM wilaya ya bagamoyo.ufanisi wa bwana RIDHIWANI katika mambo ya shughuli za vijana ikiwemo kushirikiana na wenzake kufanya makambi ya kuwaandaa vijana kwa shughuli za jumuiya na mchango wake ulimpelekea kuchaguliwa 2004 kuwa MJUMBE WA BARAZA LA UVCCM-PWANI.ikumbukwe kuwa kipindi hiki mwenyekiti wa vijana mki=oa wa pwani alikuwa BW.KULWA SAID.
katika uchaguzi wa ndani wa CCM , mwaka 2007 bwana RIDHIWANI lichaguliwa kwa kura nyingi , tena kwa kuongoza kwa wingi wa kura kuwa MJUMBE WA MKUTANO MKUU WA CCM TAIFA (nafasi abayo anayo hadi sasa).Pamoja na hillo pia RIDHIWANI katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2008 lichaguliwa na vijana wenzake wa wilaya ya BAGAMOYO kuwa MJUMBE WA MKUTANO MKUU WA UVCCM-TAIFA na pia MJUMBE WA HALMASHAURI KUU YA CCM YA WILAYA -BAGAMOYO.
nafasi ya ujumbe wa halmashauri ya ccm ya wilaya , inampa nafasi ya kuwawakilisha vijana wenzake ndani ya vijao vya chama ngaz ya wilaya. mwaka 2008 alichaguliwa kuwa MJUMBE WA BARAZA KUU LA VIJANA TAIFA kuwakilisha UVCCM-PWANI na kabla kikao cha baraza kuu akijamchagua yeye kuwa MJUMBE WA KAMATI YA UTEKELEZAJI YA UVCCM-TAIFA.
RIDHIWANI amekuwa akishiriki katika shughuli za vijana kila siku. kama walivyovijana wengine amekuwa mstari wa mbele kukitetea chama chake cha CCM na pia sera zake. ameshiriki katika mambo yanayohusu vijana wenzake katika makundi mbalimbali hasa yale ya wanafunzi,wanamuziki,wanamitindo,walemavu na mengoineyo mengi.
Kichama ameshiriki kwenye mambo mengi hasa ili la kampeni za chama safari hii. yeye na wenzake akiwemo MAKAMU MWENYEKITI, KATIBU MKUU,NAIBU KATIBU MKUU na wengineo ambao waligawanyika katika makundi mbalimbali wakikinadi chama chao.kubwa zaidi ni jinsi walivyojipanga vijana hasa kukisaidia chama chao kirudi lakini Ukiacha yote ni jinsi kijana alivyokuwa mstari wa mbele kuhahakikisha mambo yanakuwa mazuri.
RIDHIWANI amewahi wakilisha nchi yetu katika mikutano mbalimbali toka akiwa mtoto. mtakumbuka mkutano wa watoto ,ROME 1992, YES-SUMMIT MEXICO 2001,PANEL ON ENVIRONMENTAL SINGAPORE 2005,COMMONWEALTH YOUTH ORGANISATION MALTA 2007- YES-AFRICAN CAUCAS LESOTHO 2006, DEVELOPMENT AND CHALLENGE FACING RULLING PARTIES-SOUTH AFRICA 2008 na mengineyo mengi
RIDHIWANI ameoa na mungu amemjalia mtoto mmoja wa kike anaitwa AZIZA.
ni imani wajukuu zangu sasa mnamuelewa kidogo RIDHIWANI.tunapojadili ndani ya kitivo hiki cha waelewa nafikiri ni vyema tukaanzia hapa.kwamba ridhiwani tunayemjua anafanana hivi. na ni imani yangu kuwa kidogo kama sio kwa msaada swali '' HUYU RIDHIWANI NI NANI, ANAZUNGUMZA KAMA NANI NA ANAFANYA HIVI KAMA NANI LINAWEZA KUWA LIMEPATIWA JIBU''
MNYONGE MNYONGENI, LAKINI HAKI YAKE..................................
ni kwa kipindi kirefu kweli nimeshuhudia huu mjadala juu ya huyu kijana mwenzenu! kama ilivyo ada yangu, leo nimeamua nijitokeze tena; pamoja na mambo mengine mengi ambayo yametokea hapa karibuni na mwaka huu mpya leo nataka nieleze kwa ufupi juu ya huyu kijana na jinsi ninavyo mjua mimi.........
RIDHIWANI KIKWETE,kama wengin wanavyomjua alizaliwa katika hospital ya wilaya ya bagamoyo tarehe 16 mwezi wa NNE mwaka 1979. kijana huyu alizaliwa toka kwa mama AZIZA bint SABURI na baba JAKAYA MRISHO KIKWETE.
RIDHIWANI ni kijana wa kwanza kwa wazazi hawa na alifuatiwa na mdogo wake anayejulikana kwa jina la SALAMA ambaye kwa sasa ni daktari na mwalimu pale MUHIMBILI chuoni.
kijana huyu alianza shule ya msingi mwaka 1987 pale shule ya msingi MATANGINI,nachingwea mkoa wa LINDI.sababu kubwa za yeye kuanza shule huko ni kazi aliyokuwa akifanya baba yake kipindi hicho. ikumbukwe kuwa bwana Kikwete alikuwa katibu wa CCM ,wilayani hapo. mwaka mmoja baadae, bwana ridhiwani na baba yake waliamia MASASI,mkoa wa MTWARA.akiwa huko alijiunga na shule ya MKOMAINDO kwa masomo yake ya darasa la pili kabla hawajarudi DAR ES SAALAAM, mwaka1989 ambapo alijiunga na shule ya FORODHANI iliyopo maeneo ya posta ya zamani hadi alipomaliza darasa la saba.
masomo ya sekondari aliyapata katika shule ya SHAABAN ROBERT na baadae MKWAWA mkoani IRINGA kabla ya kurudi DAR ES SALAAAM kwa ajili ya elimu ya juu katika CHUO KIKUUU CHA DAR ES SALAAM, sehemu ya mlimani na baadae ENGLAND,kwa masomo ya cheti cha elimu ya juu.
KISIASA
kisiasa kijana huyu alianza akiwa mdogo sana.historia inaanza akiwa nyumbani kwao na babu yake pale bagamoyo, ambapo alishiriki katika shughuli za kucheza gwaride kama chipukizi wa chama na hata alipokwenda huko NCHINGWEA NA MASASI aliendelea na shughuli za kucheza gwaride la chipukizi wa chama cha mapinduzi.
mwaka 1992, alikuwa ni mmoja kati ya vijana walioshiriki kama wajumbe kwenye mkutano mkuu wa chipukizi wa ccm taifa uliofanyika mbeya ambao ulimchagua bwana RAYMOND MANGWALE kuwa mwenyekiti wa jumuiya hiyo taifa. ( ikumbukwe bwana RAYMOND ni katibu wa UV-CCM, mkoa wa DODOMA ,kwa sasa). hata hivyo pia, wakati wa enzi hizo za masomo ya shule ya msingi, ridhiwani atakumbukwa kama kijana aliyechangia hela nyingi kwenye mradi wa mabasi ya UV-CCM na hata kupeWa nishani na RAISI mstaafu wa AWAMU YA PILI, ALHAJI ALLY HASSAN MWINYI katika viwanja vya KARIMJEE sherehe ambazo zilihudhuriwa na wageni mbalimbali wakiwemo mabalozi wa nchi mbalimbali na viopngozi wa serikali.
wakati yupo sekondari aliendelea kuwa mwana harakati wa kawaida pale shuleni DAR ES SALAAM na hata baadae IRINGA.Waliosoma naye iringa wanakumbuka pilika zake na wenzake katika siasa za wanafunzi ,na michezoni.alikuwa mcheza mpira mzur sana enzi hizo.sijui siku hizi kama anacheza au bado.kumbukumbu zinaonyesha ushiriki wake katika kampeni za kufanikisha wenzake kupata nafasi za uongozi.
wakati akiwa chuoni, alikuwa mstari wa mbele katika siasa za DARUSO. RIDHIWANI amewahi kuwa katibu wa serikali ya wanafunzi, WIZARA YA MAMBO YA NJE NA WANAFUNZI WANAOTOKA NCHI ZA NJE, na baadae alikuwa MBUNGE MWAKILISHI TOKA KITIVO CHA WANAFUNZI WA SHERIA, kabla hajawa MWENYEKITI WA DARUSO-KITIVO CHA SHERIA.
katika kipindi hiki tumeona alivyokuwa akishiriki katia siasa za wanafunzi na hata kushirikiana na wenzake kuhakikisha kuwa yale mambo wanayoyataka katika mazingira ya chuoni hapo yanakuwa vizuri.
Wakati yupo chuoni, akiwa mwaka wa tatu, 2002 aliteuliwa kuwa MUHAMASISHAJI WA UVCCM-wilaya ya BAGAMOYO.ikumbukwe kipindi hiki ni kipindi bwana SAIDI MTANDA ambaye kwa sasa ni MBUNGE WA JIMBO LA MCHINGA,LINDI alikuwa ndiyo MWENYEKITI WA UVCCM wilaya ya bagamoyo.ufanisi wa bwana RIDHIWANI katika mambo ya shughuli za vijana ikiwemo kushirikiana na wenzake kufanya makambi ya kuwaandaa vijana kwa shughuli za jumuiya na mchango wake ulimpelekea kuchaguliwa 2004 kuwa MJUMBE WA BARAZA LA UVCCM-PWANI.ikumbukwe kuwa kipindi hiki mwenyekiti wa vijana mki=oa wa pwani alikuwa BW.KULWA SAID.
katika uchaguzi wa ndani wa CCM , mwaka 2007 bwana RIDHIWANI lichaguliwa kwa kura nyingi , tena kwa kuongoza kwa wingi wa kura kuwa MJUMBE WA MKUTANO MKUU WA CCM TAIFA (nafasi abayo anayo hadi sasa).Pamoja na hillo pia RIDHIWANI katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2008 lichaguliwa na vijana wenzake wa wilaya ya BAGAMOYO kuwa MJUMBE WA MKUTANO MKUU WA UVCCM-TAIFA na pia MJUMBE WA HALMASHAURI KUU YA CCM YA WILAYA -BAGAMOYO.
nafasi ya ujumbe wa halmashauri ya ccm ya wilaya , inampa nafasi ya kuwawakilisha vijana wenzake ndani ya vijao vya chama ngaz ya wilaya. mwaka 2008 alichaguliwa kuwa MJUMBE WA BARAZA KUU LA VIJANA TAIFA kuwakilisha UVCCM-PWANI na kabla kikao cha baraza kuu akijamchagua yeye kuwa MJUMBE WA KAMATI YA UTEKELEZAJI YA UVCCM-TAIFA.
RIDHIWANI amekuwa akishiriki katika shughuli za vijana kila siku. kama walivyovijana wengine amekuwa mstari wa mbele kukitetea chama chake cha CCM na pia sera zake. ameshiriki katika mambo yanayohusu vijana wenzake katika makundi mbalimbali hasa yale ya wanafunzi,wanamuziki,wanamitindo,walemavu na mengoineyo mengi.
Kichama ameshiriki kwenye mambo mengi hasa ili la kampeni za chama safari hii. yeye na wenzake akiwemo MAKAMU MWENYEKITI, KATIBU MKUU,NAIBU KATIBU MKUU na wengineo ambao waligawanyika katika makundi mbalimbali wakikinadi chama chao.kubwa zaidi ni jinsi walivyojipanga vijana hasa kukisaidia chama chao kirudi lakini Ukiacha yote ni jinsi kijana alivyokuwa mstari wa mbele kuhahakikisha mambo yanakuwa mazuri.
RIDHIWANI amewahi wakilisha nchi yetu katika mikutano mbalimbali toka akiwa mtoto. mtakumbuka mkutano wa watoto ,ROME 1992, YES-SUMMIT MEXICO 2001,PANEL ON ENVIRONMENTAL SINGAPORE 2005,COMMONWEALTH YOUTH ORGANISATION MALTA 2007- YES-AFRICAN CAUCAS LESOTHO 2006, DEVELOPMENT AND CHALLENGE FACING RULLING PARTIES-SOUTH AFRICA 2008 na mengineyo mengi
RIDHIWANI ameoa na mungu amemjalia mtoto mmoja wa kike anaitwa AZIZA.
ni imani wajukuu zangu sasa mnamuelewa kidogo RIDHIWANI.tunapojadili ndani ya kitivo hiki cha waelewa nafikiri ni vyema tukaanzia hapa.kwamba ridhiwani tunayemjua anafanana hivi. na ni imani yangu kuwa kidogo kama sio kwa msaada swali '' HUYU RIDHIWANI NI NANI, ANAZUNGUMZA KAMA NANI NA ANAFANYA HIVI KAMA NANI LINAWEZA KUWA LIMEPATIWA JIBU''
MNYONGE MNYONGENI, LAKINI HAKI YAKE..................................