Yericko Nyerere
JF-Expert Member
- Dec 22, 2010
- 16,987
- 20,271
CCM yote ni wachafu, lakini hakuna upuuzi ulio upuuzi mtu. Leo wanaCCM wamekomaza shingo wanasema wanatafuta mtu aliye msafi ili aliokoe taifa, hii ina maana kuwa rais aliyepo sio mwadilifu wala msafi na kaliharibu taifa (kwa tafsiri ya WanaCCM hasa watia nia).
WanaCCM wanaujua moyo wa Kikwete unawaza nini? Wanafahamu kuwa rais ni mzoefu wa kutenda asichoongea na kuongea asichokitenda? (kumbukeni Katiba Mpya, Richmond n.k.)
Nimemsikia rais pale Dodoma, nae akitangaza wazi kuwa anamtaka mgombea wa CCM aliye msafi kuanzia utosi mpaka unyayo. Najiuliza sana, hivi rais anafahamu vema kuwa maslahi yake yapo hatarini ikiwa atapatikana mtu aliye tofauti na yeye kihulka na kimaadili?
Katiba ya nchi inayompa kinga rais ambayo ndio kichaka cha viongozi wetu, rais Kikwete anafahamu kuwa inaweza kubadilishwa ndani masaa 48 tu baada ya kuapishwa rais huyu msafi na mwadilifu ili JK awajibishwe?
Nani atalinda heshima na maslahi ya rais Jakaya Kikwete kati ya waliotangaza kuwania urais na wale wanaotajwatajwa?
WanaCCM wanaujua moyo wa Kikwete unawaza nini? Wanafahamu kuwa rais ni mzoefu wa kutenda asichoongea na kuongea asichokitenda? (kumbukeni Katiba Mpya, Richmond n.k.)
Nimemsikia rais pale Dodoma, nae akitangaza wazi kuwa anamtaka mgombea wa CCM aliye msafi kuanzia utosi mpaka unyayo. Najiuliza sana, hivi rais anafahamu vema kuwa maslahi yake yapo hatarini ikiwa atapatikana mtu aliye tofauti na yeye kihulka na kimaadili?
Katiba ya nchi inayompa kinga rais ambayo ndio kichaka cha viongozi wetu, rais Kikwete anafahamu kuwa inaweza kubadilishwa ndani masaa 48 tu baada ya kuapishwa rais huyu msafi na mwadilifu ili JK awajibishwe?
Nani atalinda heshima na maslahi ya rais Jakaya Kikwete kati ya waliotangaza kuwania urais na wale wanaotajwatajwa?