Nani anasimama nyuma ya Mwekezaji wa Soko la CCM Katoro Geita?

Mkurya mweupe

JF-Expert Member
Aug 10, 2023
227
742
Kwanza nipende kutoa shukrani kutokana na maboresho yaliyofanywa na mwekezaji katika kuboresha soko la CCM, Katoro Geita, Changamoto kubwa iliyoibuka baada ya Mwekezaji kushika hili soko ni unyanyasi mkubwa unaofanyika kwa wafanyabiashara wadogo wadogo, ikiwemo;

1. Mkuu wa mkoa wa Geita, ndugu Martin Shigela alikuja na kuhutubia mbele ya soko akiwaambia wafanyabiashara wadogo walioko kwenye road reserves hawahusiki na mwekezaji inabidi watozwe tu hela ya ushuru ,mfano wa usafi, lakini mwekezaji alikiuka agizo la mkuu wa mkoa akidai kuwa yeye labda atafute soko lake na watu wakatozwa kodi kubwa, kulipia meza hyo, pia mkuu wa Mkoa aliomba wamama wauza mboga wanaotandika chini mfano wauza mchicha, wasitozwe Kodi kubwa ambapo mwekezaji anawatoza elfu 20,000, lakini agizo hilo la mkuu wa mkoa lilikiukwa? Nani yupo nyuma ya Mwekezaji huyu hadi kudharau amri ya mkuu wa mkoa?

2. Kuna machinga waliokuwa wamewekwa na mwekezaji mwenyewe wakimlipa kodi kwa mwaka kwa ajili ya kufanya biashara katika eneo hilo mfano wapo waliokuwa wamelipia pembezoni mwa kuta lakini baadae yeye amevunja makubaliano na kuamua kuwakata hela za miezi iliyotumika na kuwaambia watafute maeneo mengine na kuweka watu wengine kwa bei kubwa zaidi, wakati mkataba nao haujaisha , Je kisheria ipo sawa kuvunja mkataba kabla ya Kodi haijaisha au kumpandishia Kodi mteja wako katikati ya mkataba akiwa hajamaliza mwaka wake?

3. Mwekezaji alipewa ajenge soko kwa kufata ramani iliyokuwa imetolewa ,lakini cha kushangaza ramani imekiukwa ameamua kuongeza baadhi ya vyumba ambavyo vingine vinaingia kwenye road reserves ,je wasimamizi wa miradi hawaoni kinachofanyika ,nani yupo nyuma ya Mwekezaji hadi kumfanya akiuke ramani ya soko na kufata maslahi yake binafsi?

martin Shigela dorothy Gwajima ccm TAKUKURU
 
Yani mtu awekeze pesa alafu wanazengo waje kupigana pesa bila kulipia hata mia ya uhuru??? Hii ni dhulma sasa. Mwacheni mwekezaji ajirudishie pesa yake n faida. Maana ccm wanachukua kodi kwake, tra kama kawa, anatakiwa kuzingatia usafi n other maintenance costs, alafu mchuuzi na machinga wanataka kuingia sokoni kupiga pesa bila mwekezaji kuingiza hata mia. Embu tuache kuyafanya maisha ya wawekezaji yawe magumu kwenye nchi ngumu kama yetu. Sio ya baba ile
 
Yani mtu awekeze pesa alafu wanazengo waje kupigana pesa bila kulipia hata mia ya uhuru??? Hii ni dhulma sasa. Mwacheni mwekezaji ajirudishie pesa yake n faida. Maana ccm wanachukua kodi kwake, tra kama kawa, anatakiwa kuzingatia usafi n other maintenance costs, alafu mchuuzi na machinga wanataka kuingia sokoni kupiga pesa bila mwekezaji kuingiza hata mia. Embu tuache kuyafanya maisha ya wawekezaji yawe magumu kwenye nchi ngumu kama yetu. Sio ya baba ile
Machinga hao wamelipia ishu anakuwa anawabadilikia ,kulipia yupo sawa kwenye eneo lake ishu Ni mfano akuambie kodi yako ni laki tano kwa mwaka ,halafu baada ya miez minne akuambie inabid uongeze laki tano Kodi yako iwe milioni ,je hii ni sawa?

Na hao aliowasema mkuu wa mkoa wenyewe hawapo eneo la soko bali wapo kwenye hifadhi ya barabara kwaiyo alisema hawa walioko kwenye hifadhi wao wasitozwe ,maana hawako eneo la mwekezaji.

Pia yeye inabid atoze kodi kwenye eneo lililo kwenye mradi wako ,sasa wapo hawa wamama wanaotandaza bado hajawajengea eneo lao ili awatoze ,sasa inakuwaje awatoze kinyume na mkataba ? Wakati eneo lao bado hajawajengea?
 
Jamaa katumia hela nyingi kujenga lile soko wakae nae vizuru kila mtu apate
Upo sahihi kabisa ishu ni kukosekana uaminifu kati yake na wajasiriamali ,wapo aliowaambia kodi ni laki tano kujipachika baadae akawaambia ninawaongezea Kodi na ni ndani ya miez michache ,ni sawa sawa na mwenye nyumba akupandishie kodi katikati ya mwaka kuwa uongezee ulikuwa unampunja au utoke ,je ni sahihi .....ishu hiko hv akisema kodi ni kiasi fulani iwe hvo sio watu walipie then abadilike.
 
Mwekezaji nimesimama nae kipindi anapambana na madiwani kwa kuwa walikosa mgao Ila kwa hili na yeye anakosea , abadilike
 
Machinga hao wamelipia ishu anakuwa anawabadilikia ,kulipia yupo sawa kwenye eneo lake ishu Ni mfano akuambie kodi yako ni laki tano kwa mwaka ,halafu baada ya miez minne akuambie inabid uongeze laki tano Kodi yako iwe milioni ,je hii ni sawa?
Na hao aliowasema mkuu wa mkoa wenyewe hawapo eneo la soko bali wapo kwenye hifadhi ya barabara kwaiyo alisema hawa walioko kwenye hifadhi wao wasitozwe ,maana hawako eneo la mwekezaji.
Pia yeye inabid atoze kodi kwenye eneo lililo kwenye mradi wako ,sasa wapo hawa wamama wanaotandaza bado hajawajengea eneo lao ili awatoze ,sasa inakuwaje awatoze kinyume na mkataba ? Wakati eneo lao bado hajawajengea?
Kwanini wafanye biashara kwenye hifadhi ya barabara?
 
Kwanini wafanye biashara kwenye hifadhi ya barabara?
Hilo ni swali la kuuliza ngazi za juu maana Tanzania nzima watu wanafanyia biashara kwenye road reserves ,hawa wa kutandika chini na ishapita ,ebu Survey mikoa yote Tanzania utagundua hilo ,ndo maana Hadi mkuu wa mkoa aliruhusu biashara kufanyika kwenye road reserves akijua kwa maisha ya Watanzania ni kawaida.
 
Upo sahihi kabisa ishu ni kukosekana uaminifu kati yake na wajasiriamali ,wapo aliowaambia kodi ni laki tano kujipachika baadae akawaambia ninawaongezea Kodi na ni ndani ya miez michache ,ni sawa sawa na mwenye nyumba akupandishie kodi katikati ya mwaka kuwa uongezee ulikuwa unampunja au utoke ,je ni sahihi .....ishu hiko hv akisema kodi ni kiasi fulani iwe hvo sio watu walipie then abadilike.
hakuna mikataba? Haya mambo ya makubaliano ya mdomo miaka hii yamepitwa na wakati.

Halafu inakuwaje soko linakuwa la CCM na siyo serikali? Hapa ndiyo sielewi.
 
Kwanza nipende kutoa shukrani kutokana na maboresho yaliyofanywa na mwekezaji katika kuboresha soko la ccm ,Katoro Geita ,Changamoto kubwa iliyoibuka baada ya Mwekezaji kushika hili soko ni unyanyasi mkubwa unaofanyika kwa wafanyabiashara wadogo wadogo ,ikiwemo
1.Mkuu wa mkoa wa Geita ,ndugu Martin Shigela alikuja na kuhutubia mbele ya soko akiwaambia wafanyabiashara wadogo walioko kwenye road reserves hawahusiki na mwekezaji inabidi watozwe tu hela ya ushuru ,mfano wa usafi ,lakini mwekezaji alikiuka agizo la mkuu wa mkoa akidai kuwa yeye labda atafute soko lake na watu wakatozwa kodi kubwa,kulipia meza hyo ,pia mkuu wa Mkoa aliomba wamama wauza mboga wanaotandika chini mfano wauza mchicha ,wasitozwe Kodi kubwa ambapo mwekezaji anawatoza elfu 20,000 ,lakini agizo hilo la mkuu wa mkoa lilikiukwa ? Nani yupo nyuma ya Mwekezaji huyu hadi kudharau amri ya mkuu wa mkoa ?

2,Kuna machinga waliokuwa wamewekwa na mwekezaji mwenyewe wakimlipa kodi kwa mwaka kwa ajili ya kufanya biashara katika eneo hilo mfano wapo waliokuwa wamelipia pembezoni mwa kuta lakini baadae yeye amevunja makubaliano na kuamua kuwakata hela za miezi iliyotumika na kuwaambia watafute maeneo mengine na kuweka watu wengine kwa bei kubwa zaidi ,wakati mkataba nao haujaisha , Je kisheria ipo sawa kuvunja mkataba kabla ya Kodi haijaisha au kumpandishia Kodi mteja wako katikati ya mkataba akiwa hajamaliza mwaka wake?
3 . Mwekezaji alipewa ajenge soko kwa kufata ramani iliyokuwa imetolewa ,lakini cha kushangaza ramani imekiukwa ameamua kuongeza baadhi ya vyumba ambavyo vingine vinaingia kwenye road reserves ,je wasimamizi wa miradi hawaoni kinachofanyika ,nani yupo nyuma ya Mwekezaji hadi kumfanya akiuke ramani ya soko na kufata maslahi yake binafsi ?
martin Shigela dorothy Gwajima ccm TAKUKURU
Mimi
 
Na kawaida ukivunja makubaliano inabid urudishe hela yote
kama yeye hataki mikataba inakuwaje wewe ukivunja makubaliano inabidi urudishe hela yote?

Nadhani umefika wakati kwa sasa hao wanaokodi wote washirikiane kwa umoja wao watafute mwanasheria awasimamie na siyo kwenda mmoja mmoja kufanya negotiations naye.
 
kama yeye hataki mikataba inakuwaje wewe ukivunja makubaliano inabidi urudishe hela yote?

Nadhani umefika wakati kwa sasa hao wanaokodi wote washirikiane kwa umoja wao watafute mwanasheria awasimamie na siyo kwenda mmoja mmoja kufanya negotiations naye.
Uko sahihi
 
Back
Top Bottom