Uwekezaji katika soko la CCM Katoro, Chama Cha Mapinduzi kimehujumiwa au kinajihujumu chenyewe?

Mkurya mweupe

JF-Expert Member
Aug 10, 2023
218
740
CCM kama taasisi inayoshika dola na taasisi yenye miradi mingi kulinganisha na taasisi nyingine hasa vyama vya siasa . CCM imempa mwekezaji kujenga soko la CCM kisasa ,kiukwel ni nia nzuri ukiangalia ramani yake linaenda kuwa soko bora na la kisasa ukilinganisha na masoko mengi yaliyopo hapa nchini.

Mwekezaji aliyepewa tenda ya kuboresha hilo soko la CCM Katoro Geita alikubaliana na chama ajenge majengo hayo kwa mkataba wa miaka 9 ,ajenge soko hilo kwa kiwango kinachostahili huku CCM wenyewe wakijiridhisha kila hatua kuwa amejenga kwa kiwango bora ,huku mwekezaji akiwa na umiliki wa hilo soko ,means baada ya miaka tisa akiachie chama ,kiendelee na soko lake.

Ila kinachoendelea kwa sasa ni aibu hasa kwa taasisi inayoshikilia dola kama inashindwa kusimamia mradi wake wenyewe ,kujengwa kwa kiwango kinachostahili ,Je CCM kama taasisi itaweza kweli kusimamia miradi ya serikali mikubwa ?

Majengo yanayojengwa na mwekezaji ni ya kiwango cha chini ,bora mwanzo alianza vizuri ,ila kwa sasa kuna uwezekano ikifika miaka tisa ,anamaliza mkataba wake atakiachia chama magofu .

Kinachoshangaza kuna siku afisa miradi wa Chama wilaya ya Geita alifika katika eneo hilo akagomba sana akilalamika tofali za block zilizokuwa zinatumika kujengea, hata mtoto akipiga ngumi zilikuwa zina uwezo wa kuvunjika ,akaenda nazo wilayani na sample za tofali kureport, lakini alipofika huko akawa mpole kabisa ,ndo maana nikajiuliza kuwa chama Cha Mapinduzi mkoa wa Geita ,kinajihujumu au kinahujumiwa?

Kuna block moja ishakamilika inavuja mpaka Gypsum board zikamwagika ,ina maana kweli chama hakioni hilo ,mpaka wakaanza kuziba upya ,jengo lina miezi 4 ,linavuja ,mpaka linaanza kuzibwa upya ,je chama kikija kuachiwa kwa miaka tisa, si yatakuwa magofu, yaan nyumba zinabomolewa ili zijengwe za kisasa cha kushangaza zinazojengwa zinazidiwa na zilizobomolewa ,hii ni aibu kwa chama kama kinashindwa kusimamia miradi yake ,je kitaweza kusimamia miradi ya serikali kweli?

Kuna majengo ndo yanaendelea kukamilishwa yametumia board za kizaman baadhi ya vyumba badala ya Gypsum board Kama ilivyopendekezwa kwenye majengo ya kisasa ,na hizo board zote si za kununua ni za kutoa kwenye majengo yaliyobomolewa ,kiukweli ni aibu kwa Chama .

Chama Cha Mapinduzi inabidi kiwe mfano katika miradi yake isionekane kina ubabaishaji hadi harufu za rushwa katika ujengaji wake ,haiwezekani Afisa miradi anakagua tofali za block zinavunjwa kwa mkono ,anaenda nazo anagomba baadae anapiga kimya na tofali hzo hzo zinaendelea kutumika hzohzo .

Ona board za kuungaunga zilizotumika View attachment 2844770View attachment 2844771

IMG_20231217_080331_115.jpg
 
Waambie warekebishe na choo, hata kama ni kwa "kulipua" kama hayo majengo mengine.
 
Msingi wa block mpya unaojengwa ,unajengwa kwa kuchapiwa kwa juu juu ,baada ya miaka tisa mwekezaji kumaliza mkataba wake ,mtaachiwa nini CCM kama Taasisi?
IMG_20231217_193610_357.jpg
 
We kwa mf: kinachokuuma ni nini?

Umeshaona ccm yenyewe inachoifanyia nchi?
 
CCM kama taasisi inayoshika dola na taasisi yenye miradi mingi kulinganisha na taasisi nyingine hasa vyama vya siasa . CCM imempa mwekezaji kujenga soko la CCM kisasa ,kiukwel ni nia nzuri ukiangalia ramani yake linaenda kuwa soko bora na la kisasa ukilinganisha na masoko mengi yaliyopo hapa nchini.

Mwekezaji aliyepewa tenda ya kuboresha hilo soko la CCM Katoro Geita alikubaliana na chama ajenge majengo hayo kwa mkataba wa miaka 9 ,ajenge soko hilo kwa kiwango kinachostahili huku CCM wenyewe wakijiridhisha kila hatua kuwa amejenga kwa kiwango bora ,huku mwekezaji akiwa na umiliki wa hilo soko ,means baada ya miaka tisa akiachie chama ,kiendelee na soko lake.
Ila kinachoendelea kwa sasa ni aibu hasa kwa taasisi inayoshikilia dola kama inashindwa kusimamia mradi wake wenyewe ,kujengwa kwa kiwango kinachostahili ,Je CCM kama taasisi itaweza kweli kusimamia miradi ya serikali mikubwa ?
Majengo yanayojengwa na mwekezaji ni ya kiwango cha chini ,bora mwanzo alianza vizuri ,ila kwa sasa kuna uwezekano ikifika miaka tisa ,anamaliza mkataba wake atakiachia chama magofu .
Kinachoshangaza kuna siku afisa miradi wa Chama wilaya ya Geita alifika katika eneo hilo akagomba sana akilalamika tofali za block zilizokuwa zinatumika kujengea ,hata mtoto akipiga ngumi zilikuwa zina uwezo wa kuvunjika ,akaenda nazo wilayani na sample za tofali kureport ,lakini alipofika huko akawa mpole kabisa ,ndo maana nikajiuliza kuwa chama Cha Mapinduzi mkoa wa Geita ,kinajihujumu au kinahujumiwa?

Kuna block moja ishakamilika inavuja mpaka Gypsum board zikamwagika ,ina maana kweli chama hakioni hilo ,mpaka wakaanza kuziba upya ,jengo lina miezi 4 ,linavuja ,mpaka linaanza kuzibwa upya ,je chama kikija kuachiwa kwa miaka tisa ,si yatakuwa magofu ,yaan nyumba zinabomolewa ili zijengwe za kisasa cha kushangaza zinazojengwa zinazidiwa na zilizobomolewa ,hii ni aibu kwa chama kama kinashindwa kusimamia miradi yake ,je kitaweza kusimamia miradi ya serikali kweli?

Kuna majengo ndo yanaendelea kukamilishwa yametumia board za kizaman baadhi ya vyumba badala ya Gypsum board Kama ilivyopendekezwa kwenye majengo ya kisasa ,na hizo board zote si za kununua ni za kutoa kwenye majengo yaliyobomolewa ,kiukweli ni aibu kwa Chama .
Chama Cha Mapinduzi inabidi kiwe mfano katika miradi yake isionekane kina ubabaishaji hadi harufu za rushwa katika ujengaji wake ,haiwezekani Afisa miradi anakagua tofali za block zinavunjwa kwa mkono ,anaenda nazo anagomba baadae anapiga kimya na tofali hzo hzo zinaendelea kutumika hzohzo .

Ona board za kuungaunga zilizotumika View attachment 2844770View attachment 2844771View attachment 2844772
We kumbe ni poyoyo nimepoteza muda wangu, kwa hiyo miradi ya serikali tangi uhuru amesimamia nani. We bwege tu huna hoja
 
We kumbe ni poyoyo nimepoteza muda wangu, kwa hiyo miradi ya serikali tangi uhuru amesimamia nani. We bwege tu huna hoja
Ishu hapo ni uwajibikaji ,kwa sababu wewe ni blank slate huwezi elewa hicho kitu ,ukisoma mkataba wao ulivo na kinachofanyika ni tofauti ,means kama Kuna watu wanakagua na kupitisha hayo maovu ,what next .....means kuna harufu ya rushwa katika mradi hao ,try to think beyond the black box ......Kama wamesimamia miradi tangu uhuru kwaiyo hawapaswi kuulizwa chochote kisa wamesimamia miradi hiyo tangu uhuru ,Watanzania tujifunze kuhoji na kuwajibika wote bila kujali itikadi zetu .Hii nchi ya kwetu wote ,tatizo watu wapo kivyama zaid badala ya kusimama kama Watanzania kwenye jambo la kitaifa .Kuna kitu inaitwa " State of mind " Watanzania hatuna kitu hicho ,
 
Ishu hapo ni uwajibikaji ,kwa sababu wewe ni blank slate huwezi elewa hicho kitu ,ukisoma mkataba wao ulivo na kinachofanyika ni tofauti ,means kama Kuna watu wanakagua na kupitisha hayo maovu ,what next .....means kuna harufu ya rushwa katika mradi hao ,try to think beyond the black box ......Kama wamesimamia miradi tangu uhuru kwaiyo hawapaswi kuulizwa chochote kisa wamesimamia miradi hiyo tangu uhuru ,Watanzania tujifunze kuhoji na kuwajibika wote bila kujali itikadi zetu .Hii nchi ya kwetu wote ,tatizo watu wapo kivyama zaid badala ya kusimama kama Watanzania kwenye jambo la kitaifa .Kuna kitu inaitwa " State of mind " Watanzania hatuna kitu hicho ,your suppose to be proud to be a part and parcel of Tanzanian. Na je wakisimamia miradi wakaharibu hawapaswi kuhojiwa na kuwajibika kisa tangu uhuru wanasimamia ? Miradi mingapi ilifanyika bila kuhojiwa au ilipohojiwa CCM ikashupaza shingo ikaliingiza taifa katika hasara ya kizazi hadi kizazi ,mpaka makaburi ya babu zetu yanastahili fimbo kwa kutokuchukua hatua ,je na sisi tuwe wa kutohoji maovu yakitokea kisa CCM inasimamia miradi tokea zamani?
 
We kwa mf: kinachokuuma ni nini?

Umeshaona ccm yenyewe inachoifanyia nchi?
Kama Mtanzania ndugu yangu jifunze kupaza sauti ukiona maovu yakitawala hata kama hakikuhusu kabisa ,kama taifa tukiwa na mind kama hizo hata viongozi wetu watahofu kuwa awareness ya Watanzania wengi ni kubwa ............Ni kosa kubwa kunyamaza kuona kitu kinaenda kinyume hata kama hakikuhusu ,maana ukinyamaza wakitoka kwa wengine watakuja kwako ,na kwakuwa wewe ulikaa kimya wakati maovu yanatendeka kwa wengine ukawa kimya ,utashughulikiwa ipasavyo ,hutapata wa kukutetea .......
 
Kinachokusumbua wewe ni njaa na wivu wa maendeleo na ungekuwa unaweza ungejenga wewe kama kweli ni mwana ccm wa haki na kama unahisi ni kazi ndogo iliyofanyika mtu kujitoa mhanga kwa masilahi ya chama chetu
 
Majengo ni ya kisasa sana na yanakizi viwango vyote bora kabisa kinachofanyika tu ni kwenda na mda ili wafanyabiashara waendelee kufanya kazi na kulipa kodi kwa taifa letu siku zote sio kila kinachofanyika kila mtu anakifurahia wengine mnasumbuliwa na wivu na ungekuwa mkosoaji kweli na unavithibitisho ungeenda kwenye mamlaka husika
 
Mwanzo alivyokuwa anatafutwa mwekezaji wote mlikimbia kwa kuhofia kupoteza pesa kwenye chama lakini mmeona wenye uthubutu na imani na chama wamewekeza na imewezekana mnaanza maneno
 
Back
Top Bottom