Zak Malang
JF-Expert Member
- Dec 30, 2008
- 5,404
- 234
Nani anambeba Profesa Kapuya?
Na Ezekiel Kamwaga
Kuna watu wanazaliwa na bahati. Wengine wanakutana na bahati
wakati fulani katika kipindi cha maisha yao. Wengine
wanaitafuta na kupigana kwa ajili ya bahati - Malcolm X
WAKATI aliyekuwa Makamu wa Rais, Dk. Omar Ali Juma,
alipofariki dunia mwaka 2002, magazeti ya Tanzania
yalionyesha picha ya Profesa Juma Athumani Kapuya, akilia kwa
uchungu kuomboleza msiba huo.
Kapuya alilia kwa uchungu katika namna ambayo sijawahi kuona
kiongozi wa kitaifa akifanya hivyo hadharani. Ilibidi ndugu,
jamaa na marafiki wa marehemu, wakiwamo baadhi ya mawaziri
wenzake, waende kumshika ili kumtuliza.
Mara ya mwisho kupata taarifa za kiongozi wa kitaifa kulia
hadharani ilikuwa ni wakati wa msiba wa aliyekuwa Rais wa
Ufaransa, Charles De Gaulle, katika miaka ya sabini, pale
aliyekuwa mtawala wa Jamhuri ya Afrika ya Kati, Jean Bedel
Bokassa.
Alibubujikwa na machozi mbele ya jeneza la Gaulle uyo na
kuishia kusema, Baba .Baba Baba.
Baada ya kuona picha za Kapuya akilia, wakati ule ghafla sura
ya Bokassa ikanijia kichwani (na hawafanani hata kidogo).
Nikajiuliza: Kwa nini Profesa alie vile? Dk. Omar alikuwa
nani kwake? Au ndiye Godfather wake?
Hii ni kwa sababu, kwa maoni yangu, Profesa Juma Athumani
Kapuya, hastahili kuwa waziri wa wizara yoyote hapa nchini
kwa sababu ya rekodi yake ya utendaji tangu apewe fursa.
Kwa mambo ambayo ameyafanya katika miaka ya nyuma, Kapuya
hakukuwa na sababu ya kubaki naye serikalini.
Labda kama anayemteua pekee ndiye anayeujua uzuri wake.
Nikiwa mwanafunzi wa kidato cha nne mwaka 1998, Kapuya
alikuwa waziri wa Elimu.
Kwa mara ya kwanza katika historia ya nchi yetu, mitihani ya
taifa ilivuja kiasi kwamba baadhi ya mitihani ilionekana
ikiwa imebandikwa kwenye vituo vya daladala kabla
haijafanyika.
Mtihani ule ule uliokutana nao kwenye kituo cha daladala
kabla hujafika shuleni, ndiyo ule ule uliokuja kukutana nao
kwenye chumba cha mtihani.
Hatimaye serikali ikaamua kuifuta mitihani hiyo. Hasara
iliyopatikana wakati huo haijapata kuelezwa hata leo. Na
tangu wakati huo, ugonjwa wa kuvuja kwa mitihani umekuwa
donda ndugu kwa serikali.
Pamoja na kashfa hiyo kubwa kwa serikali, Kapuya akaendelea
kudunda tu kama kawaida. Akaendelea kuwa waziri na akasema
hatajiuzulu kwa vile eti hahusiki.
Katika nchi ambazo waziri anajua wajibu wake, na serikali
inafahamu maana ya uwajibikaji, Kapuya alikuwa ama ajiuzulu
au aliyemteua alipaswa kumtema katika baraza lake la
mawaziri.
Hilo halikufanyika. Na matokeo ya yeye kutochukuliwa hatua
yoyote ni kwamba tatizo la wizi wa mitihani limeendelea.
Kama aliyemteua Kapuya hakumchukulia hatua, yeye angekuwa na
nguvu gani ya kuwachukulia hatua wa chini yake?
Na nakumbuka ni katika kipindi hicho ndipo alipokuwa
akifanya maamuzi ya ajabu ajabu kwenye masuala ya michezo.
Nakumbuka zaidi tukio la kushusha au kupandisha daraja tisiyostahili.
Kwa sababu ambazo ni serikali yetu pekee inazifahamu, Kapuya
akaendelea tu kupeta na kuwa waziri.
Alipopelekwa kuwa Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa,
kama kawaida yake, Kapuya akafanya jambo ambalo lilizua
mjadala katika vyombo vya habari.
Alitumia ndege ya jeshi kufanya ziara binafsi katika jimbo
lake la uchaguzi. Kimsingi, kwa wadhifa wake, alikuwa
anaruhusiwa kutumia ndege hiyo. Lakini tatizo akawa anatoa
lifti kwa watu. Kiutaratibu, hili ni jambo ambalo watu
hawakuwa wakilielewa.
Haya yalikuwa matumizi mabaya ya mali ya umma. Katika nchi za
wenzetu, hili lingechunguzwa na kufanyiwa kazi. Na
ingethibitika kwamba mheshimiwa alitoa lifti kushoto,kulia na
katikati, ni lazima rungu lingemwangukia.
Lakini hiyo ni nchi nyingine, si Tanzania. Hapa kwetu, hilo
likapita kama lilivyokuja. Juma Athumani Kapuya akaendelea
kuwa waziri hadi aliyemteua alipoamua kumrejesha kwenye
Wizara ya Kazi, Ajira na Maendeleo ya Vijana.
Lengo la aliyemteua kumpeleka katika wizara hiyo nyeti
silijui. Wizara hii ni nyeti kwa vile inagusa kundi lenye
watu wengi hapa nchini.
Sensa zote zilizowahi kufanyika nchini zimethibitisha pasipo
shaka kwamba nchi yetu ni ya vijana. Kwamba karibu robo tatu
ya watanzania ni vijana. Kwa hiyo waziri wa wizara hii
anashughulika na walau nusu ya watanzania.
Anatakiwa kutazama maendeleo ya kundi hilo kubwa la watu.
Katika dunia ya sasa ambayo ina tatizo kubwa la anguko la
uchumi. Ni wizara ambayo, kwa maoni yangu, inahitaji mtu
makini kwelikweli.
Cha ajabu akapelekwa Kapuya ! Na kama kawaida yake, tayari
kashaharibu na ninaweza kukuhakikishia kwamba ataendelea kuwa
waziri katika serikali hii.
Kama Kapuya angekuwa aina ya waziri anayestahili kuongoza
wizara hiyo, huu mgomo wa wafanyakazi uliopangwa kufanyika
Mei 5 mwaka huu, usingefikia katika hatua ya sasa.
Yeye angekuwa amekutana na viongozi wa Shirikisho la Vyama
vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA) kabla hawajafikia hatua
waliyofikia sasa.
Angekuwa tayari amempa rais taarifa kuhusu matatizo ya
wafanyakazi. Rais angepanga kukutana na wawakilishi wa TUCTA
kuweka mambo sawa. Kama serikali ingeona ina uwezo wa kutatua
tatizo hilo, ingelitatua mapema au ingewaeleza wafanyakazi
ukweli kuhusu hali halisi.
Lakini Kapuya hana muda wa kufanya haya. Kwake yeye, ni
afadhali aende Uwanja wa Taifa kwenda kukabidhi Kombe la
Ubingwa wa Ligi Kuu kwa klabu kipenzi chake ya Simba !
Waziri wa Kazi anapata wapi muda wa kwenda kuangalia mpira na
kukabidhi makombe wakati mgomo wa wafanyakazi ukiwa unanukia?
Hivi, kama mgomo huu utafanyika, yeye atakwepa vipi lawama za
kuhusika?
Halafu sikiliza taarifa zake kwa wana habari tangu mgomo wa
wafanyakazi ulipotangazwa. Wakati wafanyakazi wa serikali kuu
ndio hasa wanaodai kuumizwa na mishahara yao kiduchu, yeye
anakwenda kuzungumzia mishahara ya watu wa sekta binafsi
ambayo serikali haihusiki.
Mwalimu anahusika vipi na mshahara wa wachimbaji madini na
mahausigeli? Kwa nini alifanya mkutano kutangaza mishahara ya
watu ambayo serikali si inayolipa? Inachekesha. Sana tu.
Kama mgomo wa wafanyakazi utafanyika, uchumi wa nchi yetu,
ambao tayari uko taabani, utaathirika sana. Na najua hakuna
anayejali katika serikali yetu.
Na Kapuya ataendelea kuwa waziri katika serikali hii. Kwanza,
yeye si aliyegoma. Watakaogoma ndiyo wenye matatizo. Yeye
ataendelea kupeta.
Sina hakika kama ni bahati pekee ndiyo inayombakisha Kapuya
madarakani. Lakini kama ni bahati, basi pengine mwenzetu ana
bahati ya kuzaliwa.
Vinginevyo nina imani kwamba yupo anayemlinda Kapuya ndani ya
serikali yetu. Swali pekee ninalojiuliza kichwani ni kwamba;
ni nani huyo Godfather wa Kapuya?
Maoni haya binafsi yamechapishwa katika Mwanahalisi Toleo Na.
187.
Na Ezekiel Kamwaga
Kuna watu wanazaliwa na bahati. Wengine wanakutana na bahati
wakati fulani katika kipindi cha maisha yao. Wengine
wanaitafuta na kupigana kwa ajili ya bahati - Malcolm X
WAKATI aliyekuwa Makamu wa Rais, Dk. Omar Ali Juma,
alipofariki dunia mwaka 2002, magazeti ya Tanzania
yalionyesha picha ya Profesa Juma Athumani Kapuya, akilia kwa
uchungu kuomboleza msiba huo.
Kapuya alilia kwa uchungu katika namna ambayo sijawahi kuona
kiongozi wa kitaifa akifanya hivyo hadharani. Ilibidi ndugu,
jamaa na marafiki wa marehemu, wakiwamo baadhi ya mawaziri
wenzake, waende kumshika ili kumtuliza.
Mara ya mwisho kupata taarifa za kiongozi wa kitaifa kulia
hadharani ilikuwa ni wakati wa msiba wa aliyekuwa Rais wa
Ufaransa, Charles De Gaulle, katika miaka ya sabini, pale
aliyekuwa mtawala wa Jamhuri ya Afrika ya Kati, Jean Bedel
Bokassa.
Alibubujikwa na machozi mbele ya jeneza la Gaulle uyo na
kuishia kusema, Baba .Baba Baba.
Baada ya kuona picha za Kapuya akilia, wakati ule ghafla sura
ya Bokassa ikanijia kichwani (na hawafanani hata kidogo).
Nikajiuliza: Kwa nini Profesa alie vile? Dk. Omar alikuwa
nani kwake? Au ndiye Godfather wake?
Hii ni kwa sababu, kwa maoni yangu, Profesa Juma Athumani
Kapuya, hastahili kuwa waziri wa wizara yoyote hapa nchini
kwa sababu ya rekodi yake ya utendaji tangu apewe fursa.
Kwa mambo ambayo ameyafanya katika miaka ya nyuma, Kapuya
hakukuwa na sababu ya kubaki naye serikalini.
Labda kama anayemteua pekee ndiye anayeujua uzuri wake.
Nikiwa mwanafunzi wa kidato cha nne mwaka 1998, Kapuya
alikuwa waziri wa Elimu.
Kwa mara ya kwanza katika historia ya nchi yetu, mitihani ya
taifa ilivuja kiasi kwamba baadhi ya mitihani ilionekana
ikiwa imebandikwa kwenye vituo vya daladala kabla
haijafanyika.
Mtihani ule ule uliokutana nao kwenye kituo cha daladala
kabla hujafika shuleni, ndiyo ule ule uliokuja kukutana nao
kwenye chumba cha mtihani.
Hatimaye serikali ikaamua kuifuta mitihani hiyo. Hasara
iliyopatikana wakati huo haijapata kuelezwa hata leo. Na
tangu wakati huo, ugonjwa wa kuvuja kwa mitihani umekuwa
donda ndugu kwa serikali.
Pamoja na kashfa hiyo kubwa kwa serikali, Kapuya akaendelea
kudunda tu kama kawaida. Akaendelea kuwa waziri na akasema
hatajiuzulu kwa vile eti hahusiki.
Katika nchi ambazo waziri anajua wajibu wake, na serikali
inafahamu maana ya uwajibikaji, Kapuya alikuwa ama ajiuzulu
au aliyemteua alipaswa kumtema katika baraza lake la
mawaziri.
Hilo halikufanyika. Na matokeo ya yeye kutochukuliwa hatua
yoyote ni kwamba tatizo la wizi wa mitihani limeendelea.
Kama aliyemteua Kapuya hakumchukulia hatua, yeye angekuwa na
nguvu gani ya kuwachukulia hatua wa chini yake?
Na nakumbuka ni katika kipindi hicho ndipo alipokuwa
akifanya maamuzi ya ajabu ajabu kwenye masuala ya michezo.
Nakumbuka zaidi tukio la kushusha au kupandisha daraja tisiyostahili.
Kwa sababu ambazo ni serikali yetu pekee inazifahamu, Kapuya
akaendelea tu kupeta na kuwa waziri.
Alipopelekwa kuwa Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa,
kama kawaida yake, Kapuya akafanya jambo ambalo lilizua
mjadala katika vyombo vya habari.
Alitumia ndege ya jeshi kufanya ziara binafsi katika jimbo
lake la uchaguzi. Kimsingi, kwa wadhifa wake, alikuwa
anaruhusiwa kutumia ndege hiyo. Lakini tatizo akawa anatoa
lifti kwa watu. Kiutaratibu, hili ni jambo ambalo watu
hawakuwa wakilielewa.
Haya yalikuwa matumizi mabaya ya mali ya umma. Katika nchi za
wenzetu, hili lingechunguzwa na kufanyiwa kazi. Na
ingethibitika kwamba mheshimiwa alitoa lifti kushoto,kulia na
katikati, ni lazima rungu lingemwangukia.
Lakini hiyo ni nchi nyingine, si Tanzania. Hapa kwetu, hilo
likapita kama lilivyokuja. Juma Athumani Kapuya akaendelea
kuwa waziri hadi aliyemteua alipoamua kumrejesha kwenye
Wizara ya Kazi, Ajira na Maendeleo ya Vijana.
Lengo la aliyemteua kumpeleka katika wizara hiyo nyeti
silijui. Wizara hii ni nyeti kwa vile inagusa kundi lenye
watu wengi hapa nchini.
Sensa zote zilizowahi kufanyika nchini zimethibitisha pasipo
shaka kwamba nchi yetu ni ya vijana. Kwamba karibu robo tatu
ya watanzania ni vijana. Kwa hiyo waziri wa wizara hii
anashughulika na walau nusu ya watanzania.
Anatakiwa kutazama maendeleo ya kundi hilo kubwa la watu.
Katika dunia ya sasa ambayo ina tatizo kubwa la anguko la
uchumi. Ni wizara ambayo, kwa maoni yangu, inahitaji mtu
makini kwelikweli.
Cha ajabu akapelekwa Kapuya ! Na kama kawaida yake, tayari
kashaharibu na ninaweza kukuhakikishia kwamba ataendelea kuwa
waziri katika serikali hii.
Kama Kapuya angekuwa aina ya waziri anayestahili kuongoza
wizara hiyo, huu mgomo wa wafanyakazi uliopangwa kufanyika
Mei 5 mwaka huu, usingefikia katika hatua ya sasa.
Yeye angekuwa amekutana na viongozi wa Shirikisho la Vyama
vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA) kabla hawajafikia hatua
waliyofikia sasa.
Angekuwa tayari amempa rais taarifa kuhusu matatizo ya
wafanyakazi. Rais angepanga kukutana na wawakilishi wa TUCTA
kuweka mambo sawa. Kama serikali ingeona ina uwezo wa kutatua
tatizo hilo, ingelitatua mapema au ingewaeleza wafanyakazi
ukweli kuhusu hali halisi.
Lakini Kapuya hana muda wa kufanya haya. Kwake yeye, ni
afadhali aende Uwanja wa Taifa kwenda kukabidhi Kombe la
Ubingwa wa Ligi Kuu kwa klabu kipenzi chake ya Simba !
Waziri wa Kazi anapata wapi muda wa kwenda kuangalia mpira na
kukabidhi makombe wakati mgomo wa wafanyakazi ukiwa unanukia?
Hivi, kama mgomo huu utafanyika, yeye atakwepa vipi lawama za
kuhusika?
Halafu sikiliza taarifa zake kwa wana habari tangu mgomo wa
wafanyakazi ulipotangazwa. Wakati wafanyakazi wa serikali kuu
ndio hasa wanaodai kuumizwa na mishahara yao kiduchu, yeye
anakwenda kuzungumzia mishahara ya watu wa sekta binafsi
ambayo serikali haihusiki.
Mwalimu anahusika vipi na mshahara wa wachimbaji madini na
mahausigeli? Kwa nini alifanya mkutano kutangaza mishahara ya
watu ambayo serikali si inayolipa? Inachekesha. Sana tu.
Kama mgomo wa wafanyakazi utafanyika, uchumi wa nchi yetu,
ambao tayari uko taabani, utaathirika sana. Na najua hakuna
anayejali katika serikali yetu.
Na Kapuya ataendelea kuwa waziri katika serikali hii. Kwanza,
yeye si aliyegoma. Watakaogoma ndiyo wenye matatizo. Yeye
ataendelea kupeta.
Sina hakika kama ni bahati pekee ndiyo inayombakisha Kapuya
madarakani. Lakini kama ni bahati, basi pengine mwenzetu ana
bahati ya kuzaliwa.
Vinginevyo nina imani kwamba yupo anayemlinda Kapuya ndani ya
serikali yetu. Swali pekee ninalojiuliza kichwani ni kwamba;
ni nani huyo Godfather wa Kapuya?
Maoni haya binafsi yamechapishwa katika Mwanahalisi Toleo Na.
187.