Nani analihujumu Taifa? Tusipozinduka sasa...

Nani analihujumu Taifa? Tusipozinduka sasa...

Historia haiko mbali siku hizi za utumiaji wa technology, nikimaanisha uwepesi wa kupata na kutuma taarifa n.k

Historia inaonyesha ugumu wa waliopata makaburu, wamishionari(wengi walikuwa wazungu wa ulaya) na mabeberu wa Kiarabu ambao wote walifika Africa kufanya biashara.

Historia inaonyesha ugumu waliopata sio kufanya biashara bali ni Lugha, lugha zilikuwa nyingi sana na hivyo kuwafanya wawe na ugumu wa kufikia kule ambako rasilimali zipo.
isitoshe... Udini, ukatili na udhalilishishaji ndio ilikuwa njia pekee ya kutufikia na kutuhadaa kama unavyofanya hapa

Waafrika hawakuwa wamelala kama huyu nye nyere anvotaka tuamini Tulikuwa tumeshazinduka kupindukia Waafrika na hususan Watanzania,

Nye nyere, mengi niliyotaka kusema yameshaguswa

Waganda ni mabeberu wa mda mrefu, Waganda thank Iddi Amin walishazinduka...Kiira ni ya Waganda.

Sera za Ujamaa hapa unaotaka kuaminisha, haukuwa wenye mlengo wa kikomunisti.

Unadai unduminakuwili ukiwa una maana tuchague upande- mmoja kuna siagi au soseji za moscow ukiwa una maana ya kuwa mmoja ni Mkomonisti na mwingine ni Bepari- tuchague upande au tubakie na unduminakuwili ni uwongo na ni propaganda za kibepari.
Hatuna upande.

Tatizo la nishati ni kuwa ulikuwa unahujumiwa. Wewe kama unavyojinadi na ubobezi kwenye ujasusi unalijua hili. Najua hujui.

Serikali ya Awamu ya nne kama ilivyokuwa wa tatu walikuwa na vishinikizo.

Kujengwa kwa bandari bagamoyo ina maana asilimia kubwa za mizigo inatoka na sio kuingia.

Pelekeni propaganda zenu kwenu huko kwenye Demokrasia ya uwongo. Msitulaghai.
 
Na wale waliopaswa kutoa elimu zaidi kwa raia.
Waliopaswa kuipigia CCM kelele kwa madhila wayowaona wao.

Hawafanyi hivyo na badala yake wamebaki kupiga kelele ya Katiba ambayo itawahakikishia usafi wa njia ya kuingia kwenye ulaji kwa zamu.
UNA AKILI NYINGI SANA LAKINI UNA KASORO KUBWA.
 
UNA AKILI NYINGI SANA LAKINI UNA KASORO KUBWA.
Kuingia kwenye ulaji kwa zamu !! Hii sentensi nimeipenda ! Wanasiasa wengi hawapo serious na maendeleo ya nchi na watu wake , target yao ni maendeleo yao na ya walio karibu yao !! Hii ndio shida yetu kubwa tuliyonayo !!
 
Kama taifa kila mtu ana sehemu na nafasi yake, sasa kama mahakimu na majaji wanamwachia mfungwa wa madawa ya kulevya kwenye rufaa kwa vile tu search warrant na procedure hazijafuatwa lakini kidhibiti kakutwa nacho tunategemeav nini?
Tutegemee mateja waturudishe nyuma wataiba vifaa vya magari na nguvu kazi kuishia kwenye kamari huko mbeleni.madhara ni mengi hilo ni moja
 
Aliehujumu tunamjua...la msingi hayupo tena..
Ni kweli bandari ya bagamoyo ni mhimu kwa uchumi wa nchi,lkn si kwa mkataba huo,lkn pia ktk maendeleo ni lazina yawepo maamuzi magumu,ninyi mnaita dikteta,ndio maana nchi zote zilizokuwa maskini na kwa sasa zimechumpa kimaendeleo,ziliongozwa na viongozi mnaowaita madkteta,mfano malaysia,Singapore,China,cuba,Libya Iraq,zoote hizi zimeendelea kwa kasi sana,lkn sie watu kana akina magufuli hatuwataki,kwa sababu wanatudhibiti ktk miradi yetu,kwa watu wanaopenda ten percent,ni vigumu nchi kupiga hatua,yaani uwe na viongozi sampuli ya samia,halafu wasaidizi wake wawe ni kina January makamba,nape nnauye,na ridhiwani kikwete,sahau kitu linaitwa maendeleo,wao falsafa ya ni upigaji, uporaji na kitu kinaitwa cha juu,
 
Rais Samia anapambana kufufua mradi wa Bagamoyo na LPG ya Lindi lakini unajifanya hujui kwamba Chadomo kwa kushirikiana na Sukuma gang wanafanya kila mbinu Ili kukwamisha kwa visingizio vya kijinga lakini ukweli ni kwamba hawataki mama amfunike yule shujaa wao wa Afrika..

Mchawi mbongo mwenyewe.
Jpm hayupo tena,lkn bado unaendeleza mapambano na yeye??!!,chukua mabomu ukapige familia yake yoote uiangamize,na uwachome moto ukoo wake woote uwauwe na majivu uyanywe yoote ili yasionekane,na yeyote atakaemsema vzr jpm piga risasi,unaonyesha wewe unachuki ya nyoka,na unaweza kuwa mtu mwovu sana,,
 
Jpm hayupo tena,lkn bado unaendeleza mapambano na yeye??!!,chukua mabomu ukapige familia yake yoote uiangamize,na uwachome moto ukoo wake woote uwauwe na majivu uyanywe yoote ili yasionekane,na yeyote atakaemsema vzr jpm piga risasi,unaonyesha wewe unachuki ya nyoka,na unaweza kuwa mtu mwovu sana,,
Lazima tuwaele vizazi uhuni wake Ili wajifunze
 
Umeweka uchadema mwingi na itikadi nyingi,toa at least mapendo yako tufanyaje au tuanzie wapi?
 
Nilidhani watu watajikita kujadili, kupinga au kukubaliana na hoja kwa mantiki

Tatizo la vijana wetu mijadala ni kama 'sumu' , kwa maana hiyo wakikuatana na vijana wa nchi za jirani wakwetu wanasubiri '' kutetewa ajira na serikali''. Vijana wabadilke, jibu hoja , jenga hoja

Yericko Nyerere ana hoja nzuri sana, kwamba, sisi kama Taifa tumekosa dira na hatuwezi ushindani katika dunia ya 'uchumi' na si ya maderaya na makombora.

Miaka 20 iliyopita, tulikuwa na 'maisha bora kwa kila Mtanzania''.
Tukawa na 'elimu kwanza ' halafu 'kilimo kwanza' , ghafla tukawa na ''Viwanda''.

Nani anaweza kutueleza tathmini ya sera hizo, zimefaulu wapi na zimeshindwa wapi?

Pili, tukiwa na 'arable land' tumezungukwa na maji na mito, kwanini Tanzania isiwe kituo kikubwa cha ''FAO' na Mazao ya biashara kama Kahawa, Chai, Tangawizi, Dengu , Mbaazi n.k.

Kwanini hatuwezi kuwawezesha watu wetu kulima Dengu na Mbaazi tukilenga soko la watu Bilioni 1 India? Kwanini hatuwezi kutumia bahari na maziwa kuuza samaki nchi za 'EAC na SADCC'

Kwanini kiwanda cha TANELEC au Sahara vilivyozalisha bidhaa bora sana vilikufa na sasa tunaagiza bidhaa hizo hizo hafifu kutoka China.

Kwanini Gneral Tyre iliyokuwa na matairi bora viwango vya dunia ilikufa sasa tunaagiza mitumba !

Orodha inaendelea, lakini ukitaka kujua tatizo lipo wapi angalia hili

Rais JK alisaini Mradi wa Bagamayo . JK ni mwana CCM , katika baraza lake alikuwepo JPM.

Mwezi mmoja tu baada ya JPM kuingia madarakani, mradi wa Bagamoyo ukafutwa kwasababu 'eti hatutakusanya kodi''. Anayetuambia hayo ni rAIS JPM Waziri wa Rais JK

Katika mazingira ya kawaida wawili hawa wangekutana na tungekuwa na kauli moja.

Hivi Bagamoyo kama sera ya CCM na Marais ni wa CCM mkanganyiko unatoka wapi?

Watu wanadhani tatizo ni CCM, la hasha! Chadema wakichukua madaraka yatatokea haya haya.

Tatizo letu ni mfumo usioruhusu kufikiri sawa sawa, mfumo usioruhusu fikra mbadala , mfumo wenye taasisi zisizojua majukumu, mfumo usiozawadia ubunifu bali siasa.

Tuandike utaratibu utakaotuwajibisha na kujenga mifumo sawa sawa , KATIBA

JokaKuu Pascal Mayalla
Naona umeitaja mbaazi hapo, kilichowafanya watu kwenyw mbaazi sijui kama watarudia tena kulima.
 
Naona kama Kwa HOJA za kufichua uovu zimeanzia Kwa mbali natamani Dr.Slaa balozi mstaafu aendelee kumwaga madini aliishia pale alipotoa taarifa ya madawa ya kulevya ikaangukia mikononi mwa Baba!! Mwili umenisisimka naona ugumu wa kutoka hapa tulipokwama.

Hivi si tulikubaliana kwamba ili tutoke hapa tutumie udikteta SASA tulikwama wapi? Any way tunaweza kubadili mbinu tutengeneza Alina DR.Slaa wa kutosha ili wawaambie watu Wetu tulikotoka,tulipo na tunakoelekea.
 
Mtu akiongea kitu kuhusu maendeleo ya nchi watu wanaingizia Uchadema Uccm hatar sana hii tabia sijui itaachwa lini
Jamani Ndugai mbona haionekani? Yaani aliposema tu nchi itapigwa mnada, akapigwa mnada yeye?
 
Je!
Mleta bandiko amewahi kuisaidia nini Chadema kiushauri kama jasusi na kada mtiifu.

Mbona anawaacha viongozi wake wakifoka foka majukwaani bila sera zaidi ya Piiipoooziii!

Hatuwaoni wakisimama kidete kuipinga CCM kwa hoja na sera.

Badala yake ni kudandia matukio kila uchao na kujadili watu binafsi huku wakiwaombea vifo opponents wao!
Miaka 60 ya Uhuru, CCM wanaogopa chaguzi huru na za haki badala yake wanategemea TISS na Polisi kuwaweka madarakani. Sanduku la kura halisi liachwe liongee, tuone watu wanataka viongozi gani.
 
Ni kweli bandari ya bagamoyo ni mhimu kwa uchumi wa nchi,lkn si kwa mkataba huo,lkn pia ktk maendeleo ni lazina yawepo maamuzi magumu,ninyi mnaita dikteta,ndio maana nchi zote zilizokuwa maskini na kwa sasa zimechumpa kimaendeleo,ziliongozwa na viongozi mnaowaita madkteta,mfano malaysia,Singapore,China,cuba,Libya Iraq,zoote hizi zimeendelea kwa kasi sana,lkn sie watu kana akina magufuli hatuwataki,kwa sababu wanatudhibiti ktk miradi yetu,kwa watu wanaopenda ten percent,ni vigumu nchi kupiga hatua,yaani uwe na viongozi sampuli ya samia,halafu wasaidizi wake wawe ni kina January makamba,nape nnauye,na ridhiwani kikwete,sahau kitu linaitwa maendeleo,wao falsafa ya ni upigaji, uporaji na kitu kinaitwa cha juu,
Je ulifanikiwa kuuona mkataba wa bandari ya Bagamoyo? na kipengele gani unadhani hakikuwa sawa!
 
Upinzani wa kweli haupo, upo upinzani wa kimatumbo
Fikria nje ya boksi mbuzimalaya wewe, ukute hata makala halijasoma linakimbilia kuropoka upinzani sijui umefanyaje...!

Siyo kwamba CCM kuna wajinga tu walevu tupo na tunakerwa na huu ujinga...!
 
Back
Top Bottom